< Ezekiel 11 >

1 Moreover, the Spirite lift me vp, and brought me vnto the East gate of the Lordes house, which lyeth Eastwarde, and beholde, at the entrie of the gate were fiue and twentie men: among whome I sawe Iaazaniah the sonne of Azur, and Pelatiah the sonne of Benaiah, the princes of the people.
Ndipo Roho akaniinua na kunileta mpaka kwenye lango la nyumba ya Bwana linalotazama upande wa mashariki. Pale kwenye ingilio la lango kulikuwepo wanaume ishirini na watano, nami nikaona miongoni mwao Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu.
2 Then said he vnto me, Sonne of man, these are the men that imagine mischiefe, and deuise wicked counsell in this citie.
Bwana akaniambia, “Mwanadamu, hawa ndio wafanyao hila na kutoa mashauri potovu katika mji huu.
3 For they say, It is not neere, let vs builde houses: this citie is the caldron, and wee be the flesh.
Wao husema, ‘Je, hivi karibuni hautakuwa wakati wa kujenga nyumba? Mji huu ni chungu cha kupikia, nasi ndio nyama.’
4 Therefore prophesie against them, sonne of man, prophesie.
Kwa hiyo toa unabii dhidi yao, tabiri, Ewe mwanadamu.”
5 And the Spirite of the Lord fell vpon me, and said vnto me, Speake, Thus saith the Lord, O ye house of Israel, this haue ye said, and I know that which riseth vp of your mindes.
Kisha Roho wa Bwana akaja juu yangu, naye akaniambia niseme: “Hili ndilo Bwana asemalo: Hili ndilo ninyi mnalosema, ee nyumba ya Israeli, lakini ninajua mnalowaza mioyoni mwenu.
6 Many haue ye murthered in this citie, and ye haue filled the streets thereof with the slaine.
Mmewaua watu wengi katika mji huu na kujaza barabara zake maiti.
7 Therefore thus saith the Lord God, They that ye haue slaine, and haue layed in the middes of it, they are the flesh, and this citie is the caldron, but I wil bring you foorth of the mids of it.
“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: maiti ulizozitupa huko ni nyama na mji huu ni chungu, lakini nitawaondoa mtoke huko.
8 Ye haue feared the sworde, and I wil bring a sworde vpon you, saith the Lord God.
Mnaogopa upanga, nao upanga huo ndio nitakaouleta juu yenu, asema Bwana Mwenyezi.
9 And I will bring you out of the middes thereof, and deliuer you into the hands of strangers, and will execute iudgements among you.
Nitawaondoa mtoke katika mji na kuwatia mikononi mwa wageni nami nitawaadhibu.
10 Ye shall fall by the sworde, and I wil iudge you in the border of Israel, and ye shall knowe that I am the Lord.
Mtaanguka kwa upanga, nami nitatimiza hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana.
11 This citie shall not be your caldron, neyther shall ye be the flesh in the middes thereof, but I will iudge you in the border of Israel.
Mji huu hautakuwa chungu kwa ajili yenu, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitatoa hukumu dhidi yenu katika mipaka ya Israeli.
12 And ye shall knowe that I am the Lord: for ye haue not walked in my statutes, neither executed my iudgements, but haue done after the maners of the heathen, that are round about you.
Nanyi mtajua ya kuwa Mimi ndimi Bwana, kwa kuwa hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu, bali mmefuata mwenendo wa mataifa yanayowazunguka.”
13 And when I prophesied, Pelatiah the sonne of Benaiah dyed: then fell I downe vpon my face, and cryed with a loude voyce, and saide, Ah Lord God, wilt thou then vtterly destroy all the remnant of Israel?
Basi nilipokuwa ninatoa unabii, Pelatia mwana wa Benaya akafa. Ndipo nikaanguka kifudifudi, nikalia kwa sauti kuu nikasema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je utaangamiza kabisa mabaki ya Israeli?”
14 Againe the worde of the Lord came vnto me, saying,
Neno la Bwana likanijia kusema:
15 Sonne of man, thy brethren, euen thy brethren, the men of thy kindred, and all the house of Israel, wholy are they vnto whome the inhabitants of Ierusalem haue said, Depart ye farre from the Lord: for the lande is giuen vs in possession.
“Mwanadamu, ndugu zako, ndugu zako ambao ni wa uhusiano wa damu na nyumba yote ya Israeli, ndio wale ambao watu wa Yerusalemu wamesema, ‘Wako mbali na Bwana; nchi hii tulipewa sisi kuwa milki yetu.’
16 Therefore say, Thus saith the Lord God, Although I haue cast them farre off among the heathen, and although I haue scattered them among the countreis, yet wil I be to them as a litle Sanctuarie in ye countreis where they shall come.
“Kwa hiyo sema, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ingawa niliwapeleka mbali miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbalimbali, lakini kwa kitambo kidogo mimi nimekuwa mahali patakatifu kwao katika nchi walizokwenda.’
17 Therefore say, Thus saith the Lord God, I will gather you againe from the people, and assemble you out of the countreis where ye haue bene scattered, and I will giue you ye land of Israel.
“Kwa hiyo sema: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitawakusanyeni kutoka mataifa na kuwarudisha kutoka nchi ambazo mmetawanywa, nami nitawarudishia nchi ya Israeli.’
18 And they shall come thither, and they shall take away all the idoles thereof, and all the abominations thereof from thence.
“Watairudia nchi na kuondoa vinyago vyote vya upotovu na sanamu zote za machukizo.
19 And I will giue them one heart, and I will put a newe spirit within their bowels: and I will take the stonie heart out of their bodies, and will giue them an heart of flesh,
Nitawapa moyo mmoja na kuweka roho mpya ndani yao, nitaondoa kutoka ndani yao moyo wa jiwe na kuwapa moyo wa nyama.
20 That they may walke in my statutes, and keepe my iudgements, and execute them: and they shall be my people, and I will be their God.
Kisha watafuata amri zangu na kuwa waangalifu kutii sheria zangu. Watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
21 But vpon them, whose heart is towarde their idoles, and whose affection goeth after their abominations, I will lay their way vpon their owne heades, saith the Lord God.
Lakini kwa wale ambao mioyo yao imeambatana na vinyago vyao vya upotovu na sanamu zao za machukizo, nitaleta juu ya vichwa vyao yale waliyotenda asema Bwana Mwenyezi.”
22 Then did the Cherubims lift vp their wings, and the wheeles besides them, and the glorie of the God of Israel was vpon them on hie.
Ndipo wale makerubi, wenye magurudumu pembeni mwao, wakakunjua mabawa yao, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
23 And the glorie of the Lord went vp from the middes of the citie, and stoode vpon the moutaine which is towarde the East side of the citie.
Basi utukufu wa Bwana ukapaa juu kutoka mji, ukatua juu ya mlima ulio upande wa mashariki ya mji.
24 Afterwarde the Spirite tooke me vp, and brought me in a vision by the Spirit of God into Caldea to them that were led away captiues: so the vision that I had seene, went vp from me.
Roho akaniinua na kunileta mpaka kwa watu wa uhamisho huko Ukaldayo nikiwa katika yale maono niliyopewa na Roho wa Mungu. Ndipo maono niliyokuwa nimeyaona yakanitoka,
25 Then I declared vnto them that were led away captiues, all the things that the Lord had shewed me.
nami nikawaeleza wale watu wa uhamisho kila kitu Bwana alichokuwa amenionyesha.

< Ezekiel 11 >