< Exodus 25 >
1 Then the Lord spake vnto Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
2 Speake vnto the children of Israel, that they receiue an offring for me: of euery man, whose heart giueth it freely, ye shall take the offring for me.
“Waambie Waisraeli waniletee sadaka. Utapokea sadaka kwa niaba yangu kutoka kwa kila mtu ambaye moyo wake wapenda kutoa.
3 And this is the offring which ye shall take of them, golde, and siluer, and brasse,
Hizi ndizo sadaka utakazozipokea kutoka kwao: dhahabu, fedha na shaba;
4 And blewe silke, and purple, and skarlet, and fine linnen, and goates heare,
nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu, pamoja na kitani safi; singa za mbuzi;
5 And rammes skinnes coloured red, and the skinnes of badgers, and the wood Shittim,
ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
6 Oyle for the light, spices for anoynting oyle, and for the perfume of sweete sauour,
mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
7 Onix stones, and stones to be set in the Ephod, and in the brest plate.
na vito vya shohamu na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
8 Also they shall make me a Sanctuarie, that I may dwell among them.
“Kisha uwaamuru wanitengenezee mahali patakatifu, nami nitakaa miongoni mwao.
9 According to all that I shewe thee, euen so shall ye make the forme of the Tabernacle, and the facion of all the instruments thereof.
Tengeneza hema hili na vyombo vyake vyote sawasawa na kielelezo nitakachokuonyesha.
10 They shall make also an Arke of Shittim wood, two cubites and an halfe long, and a cubite and an halfe broade, and a cubite and an halfe hie.
“Nao watatengeneza Sanduku la mbao za mshita, lenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, upana wa dhiraa moja na nusu, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
11 And thou shalt ouerlay it with pure golde: within and without shalt thou ouerlay it, and shalt make vpon it a crowne of golde rounde about.
Utalifunika hilo Sanduku kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulifanyia ukingo wa dhahabu juu yake kulizunguka.
12 And thou shalt cast foure rings of golde for it, and put them in the foure corners thereof: that is, two rings shalbe on the one side of it, and two rings on the other side thereof.
Utalisubu kwa pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
13 And thou shalt make barres of Shittim wood, and couer them with golde.
Kisha utatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
14 Then thou shalt put the barres in the rings by the sides of the Arke, to beare the Arke with them.
Utaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
15 The barres shalbe in the rings of the Arke: they shall not be taken away from it.
Hiyo mipiko itabakia daima katika hizo pete za hilo Sanduku; haitaondolewa.
16 So thou shalt put in the Arke the Testimonie which I shall giue thee.
Kisha weka ndani ya hilo Sanduku ule Ushuhuda nitakaokupa.
17 Also thou shalt make a Mercie seate of pure golde, two cubites and an halfe long, and a cubite and an halfe broade.
“Tengeneza kifuniko cha upatanisho cha dhahabu safi, chenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, na upana wa dhiraa moja na nusu.
18 And thou shalt make two Cherubims of golde: of worke beaten out with the hammer shalt thou make the at ye two endes of the Merciseate.
Tengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
19 And the one Cherub shalt thou make at the one ende, and the other Cherub at the other ende: of the matter of the Mercieseate shall ye make the Cherubims, on the two endes thereof.
Tengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; watengeneze makerubi hao wawe kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
20 And the Cherubims shall stretche their winges on hie, couering the Mercie seate with their winges, and their faces one to another: to the Mercie seate warde shall the faces of the Cherubims be.
Makerubi hao watakuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, yakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao wataelekeana, wakitazama hicho kifuniko.
21 And thou shalt put the Mercieseate aboue vpon the Arke, and in the Arke thou shalt put the Testimonie, which I will giue thee,
Weka huo Ushuhuda nitakaokupa ndani ya hilo Sanduku la Agano, na uweke hicho kifuniko juu ya hilo Sanduku.
22 And there I will declare my selfe vnto thee, and from aboue ye Mercieseate betweene ye two Cherubims, which are vpon ye Arke of ye Testimonie, I wil tel thee al things which I wil giue thee in comandement vnto ye children of Israel.
Hapo juu ya hicho kifuniko, kati ya hao makerubi wawili walioko juu ya hilo Sanduku la Ushuhuda, hapo ndipo nitakapokutana nawe na kukupa maagizo yangu kwa ajili ya Waisraeli.
23 Thou shalt also make a Table of Shittim wood, of two cubites long, and one cubite broade, and a cubite and an halfe hie:
“Tengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
24 And thou shalt couer it with pure gold, and make thereto a crowne of golde round about.
Ifunike kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
25 Thou shalt also make vnto it a border of foure fingers roud about and thou shalt make a golden crowne round about the border thereof.
Kisha tengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na ufanyie ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
26 After, thou shalt make for it foure ringes of golde, and shalt put the rings in the foure corners that are in the foure feete thereof:
Tengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na uzifungie kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
27 Ouer against the border shall the rings be for places for barres, to beare the Table.
Pete hizo zitakuwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko itakayotumika kuibebea hiyo meza.
28 And thou shalt make the barres of Shittim wood, and shalt ouerlay them with golde, that the Table may be borne with them.
Tengeneza mipiko hiyo kwa mbao za mshita, uifunike na dhahabu, uitumie kubeba hiyo meza.
29 Thou shalt make also dishes for it, and incense cuppes for it, and couerings for it, and goblets, wherewith it shall be couered, euen of fine golde shalt thou make them.
Tengeneza sahani zake na masinia yake kwa dhahabu safi, pamoja na bilauri na bakuli zake kwa ajili ya kumiminia sadaka.
30 And thou shalt set vpon the Table shewe bread before me continually.
Utaweka mikate ya Wonyesho juu ya meza hii iwe mbele yangu daima.
31 Also thou shalt make a Candlesticke of pure golde: of worke beaten out with the hammer shall the Candlesticke be made, his shaft, and his branches, his boules, his knops: and his floures shalbe of the same.
“Tengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vinavyofanana na ua, matovu yake na maua yake viwe kitu kimoja.
32 Six braunches also shall come out of the sides of it: three branches of the Candlesticke out of the one side of it, and three branches of the Candlesticke out of the other side of it.
Matawi sita yatatokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
33 Three boules like vnto almondes, one knop and one floure in one braunch: and three boules like almondes in the other branch, one knop and one floure: so throughout the sixe branches that come out of the Candlesticke.
Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vitakuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yanayotokeza kwenye kile kinara cha taa.
34 And in the shaft of the Candlesticke shalbe foure boules like vnto almondes, his knops and his floures.
Juu ya kinara chenyewe vitakuwepo vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
35 And there shalbe a knop vnder two branches made thereof: and a knop vnder two branches made thereof: and a knop vnder two branches made thereof, according to the sixe branches comming out of the Candlesticke.
Tovu moja litakuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani matawi sita kwa jumla.
36 Their knops and their branches shall bee thereof. all this shalbe one beaten worke of pure golde.
Matovu na matawi yote yatakuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakifuliwa kwa dhahabu safi.
37 And thou shalt make the seuen lampes thereof: and the lampes thereof shalt thou put thereon, to giue light toward that that is before it.
“Kisha tengeneza taa zake saba na uziweke juu ya kinara hicho ili ziangaze mbele yake.
38 Also the snuffers and snuffedishes thereof shalbe of pure golde.
Mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote zitakuwa za dhahabu safi.
39 Of a talent of fine gold shalt thou make it with all these instruments.
Utatumia talanta moja ya dhahabu safi kutengeneza hicho kinara na vifaa vyake vyote.
40 Looke therefore that thou make them after their facion, that was shewed thee in the mountaine.
Hakikisha kuwa umevitengeneza sawasawa na ule mfano ulioonyeshwa kule mlimani.