< Exodus 13 >
1 And the Lord spake vnto Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
2 Sanctifie vnto me all the first borne: that is, euery one that first openeth the wombe among the children of Israel, as well of man as of beast: for it is mine.
“Niwekeeni wakfu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume. Kila mtoto wa kwanza aliye kifungua tumbo miongoni mwa Waisraeli ni mali yangu, akiwa wa mwanadamu au wa mnyama.”
3 Then Moses sayd vnto the people, Remember this day in the which ye came out of Egypt, out of the house of bondage: for by a mightie hande the Lord brought you out from thence: therefore no leauened bread shall bee eaten.
Ndipo Mose akawaambia watu, “Ikumbukeni siku hii, siku ambayo mlitoka katika nchi ya Misri, katika nchi ya utumwa, kwa sababu Bwana aliwatoa humo kwa mkono wenye nguvu. Msile chochote kilichotiwa chachu.
4 This day come yee out in the moneth of Abib.
Leo, katika mwezi wa Abibu, mnatoka.
5 Now when the Lord hath brought thee into the land of the Canaanites, and Hittites, and Amorites, and Hiuites, and Iebusites (which he sware vnto thy fathers, that he woulde giue thee, a land flowing with milke and honie) then thou shalt keepe this seruice in this moneth.
Bwana atakapokuleta katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Wahivi na Wayebusi, nchi aliyowaapia baba zako kukupa, nchi itiririkayo maziwa na asali, utaiadhimisha sikukuu hii katika mwezi huu:
6 Seuen dayes shalt thou eate vnleauened bread, and the seuenth day shall be the feast of the Lord.
Kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu na katika siku ya saba utamfanyia Bwana sikukuu.
7 Vnleauened bread shall bee eaten seuen dayes, and there shall no leauened bread be seene with thee, nor yet leauen be seene with thee in all thy quarters.
Kwa muda wa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu, pasionekane kitu chochote kilicho na chachu miongoni mwako, wala chachu yoyote isionekane popote ndani ya mipaka yako.
8 And thou shalt shew thy sonne in that day, saying, This is done, because of that which the Lord did vnto me, when I came out of Egypt.
Siku ile utamwambia mwanao, ‘Nafanya hivi kwa sababu ya jambo ambalo Bwana alinitendea nilipotoka katika nchi ya Misri.’
9 And it shalbe a signe vnto thee vpon thine hande, and for a remembrance betweene thine eyes, that the Lawe of the Lord may be in thy mouth: for by a strong hand the Lord brought thee out of Egypt.
Adhimisho hili, litakuwa kama alama kwenye mkono wako na ukumbusho katika paji lako la uso, kwamba sheria ya Bwana inapaswa iwe kinywani mwako. Kwa kuwa Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.
10 Keepe therefore this ordinance in his season appoynted from yeere to yeere.
Ni lazima uishike amri hii kwa wakati uliopangwa mwaka baada ya mwaka.
11 And when the Lord shall bring thee into the lande of the Canaanites, as hee sware vnto thee and to thy fathers, and shall giue it thee,
“Baada ya Bwana kukuingiza katika nchi ya Wakanaani na kukupa nchi hiyo, kama alivyokuahidi kwa kiapo na kwa baba zako,
12 Then thou shalt set apart vnto the Lord all that first openeth the wombe: also euery thing that first doeth open the wombe, and commeth forth of thy beast: the males shalbe the Lordes.
inakupasa kumtolea Bwana mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo. Wazaliwa wote wa kwanza wa kiume wa mifugo yako ni mali ya Bwana.
13 But euery first foale of an asse, thou shalt redeeme with a lambe: and if thou redeeme him not, then thou shalt breake his necke: likewise all the first borne of man among thy sonnes shalt thou bye out.
Kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa mwana-kondoo, lakini kama hukumkomboa, utamvunja shingo yake. Kila mzaliwa wa kwanza mwanaume miongoni mwa wana wenu utamkomboa.
14 And when thy sonne shall aske thee to morowe, saying, What is this? thou shalt then say vnto him, With a mightie hande the Lord brought vs out of Egypt, out of the house of bondage.
“Katika siku zijazo, mwanao akikuuliza, ‘Hii ina maana gani?’ Mwambie, ‘Kwa mkono wenye nguvu Bwana alitutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
15 For when Pharaoh was harde hearted against our departing, the Lord then slewe all the first borne in the lande of Egypt: from the first borne of man euen to the first borne of beast: therefore I sacrifice vnto the Lord all the males that first open the wombe, but all the first borne of my sonnes I redeeme.
Farao alipokataa kwa ukaidi kuturuhusu kuondoka, Bwana aliua kila mzaliwa wa kwanza wa Wamisri, mwanadamu na wa mnyama. Hii ndiyo sababu ninatoa dhabihu kwa Bwana mzaliwa wa kwanza wa kiume, wa kila tumbo na kumkomboa kila mzaliwa wa kwanza wa wana wangu.’
16 And it shalbe as a token vpon thine hand, and as frontlets betweene thine eyes, that the Lord brought vs out of Egypt by a mightie hande.
Jambo hili litakuwa kama ishara kwenye mkono wako na kama alama kwenye paji la uso wako, kwamba Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.”
17 Nowe when Pharaoh had let the people go, God caried them not by the way of the Philistims countrey, though it were neerer: (for God sayd, Lest the people repent whe they see warre, and turne againe to Egypt)
Farao alipowaachia watu waende, Mungu hakuwaongoza kufuata njia ipitiayo katika nchi ya Wafilisti, ingawa njia hiyo ilikuwa fupi zaidi. Kwa maana Mungu alisema, “Wakikabiliana na vita, wanaweza kubadili mawazo yao na kurudi Misri.”
18 But God made the people to go about by the way of the wildernesse of the red sea: and the children of Israel went vp armed out of the land of Egypt.
Kwa hiyo Mungu akawaongoza watu kupitia njia ya kuzunguka kupitia jangwani, kuelekea Bahari ya Shamu. Waisraeli walipanda kutoka nchi ya Misri wakiwa wamejiandaa kwa vita.
19 (And Moses tooke the bones of Ioseph with him: for he had made the children of Israel sweare, saying, God will surely visite you, and ye shall take my bones away hence with you)
Mose akachukua mifupa ya Yosefu kwa sababu Yosefu alikuwa amewaapisha wana wa Israeli. Alikuwa amewaambia, “Hakika Mungu atakuja kuwasaidia, nanyi ni lazima mwiichukue mifupa yangu mwende nayo kutoka mahali hapa.”
20 So they tooke their iourney from Succoth, and camped in Etham in the edge of the wildernesse.
Baada ya Waisraeli kuondoka Sukothi wakapiga kambi huko Ethamu pembeni mwa jangwa.
21 And the Lord went before them by day in a pillar of a cloude to leade them the way, and by night in a pillar of fire to giue them light, that they might go both by day and by night.
Wakati wa mchana Bwana aliwatangulia kwa nguzo ya wingu kuwaongoza katika njia yao, na wakati wa usiku aliwatangulia kwa nguzo ya moto kuwaangazia, ili waweze kusafiri mchana au usiku.
22 He tooke not away the pillar of ye cloude by day, nor the pillar of fire by night from before the people.
Ile nguzo ya wingu wakati wa mchana au ile nguzo ya moto wakati wa usiku haikuondoka mahali pake mbele ya watu.