< Ephesians 1 >
1 Pavl an Apostle of Jesvs Christ by the will of God, to the Saints, which are at Ephesus, and to ye faithfull in Christ Iesus:
Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, nawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Efeso, mlio waaminifu katika kuungana na Kristo Yesu.
2 Grace be with you, and peace from God our Father, and from the Lord Iesus Christ.
Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
3 Blessed be God, and the Father of our Lord Iesus Christ, which hath blessed vs with all spirituall blessing in heauenly thinges in Christ,
Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Maana, katika kuungana na Kristo ametubariki kwa kutujalia zawadi zote za kiroho mbinguni.
4 As hee hath chosen vs in him, before the foundation of the worlde, that we should be holy, and without blame before him in loue:
Kabla ya kuumbwa ulimwengu, Mungu alituteua tuwe wake katika kuungana na Kristo ili tuwe watakatifu na bila hitilafu mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake,
5 Who hath predestinate vs, to be adopted through Iesus Christ in him selfe, according to the good pleasure of his will,
Mungu alikuwa ameazimia tangu zamani kutuleta kwake kama watoto wake kwa njia ya Yesu Kristo. Ndivyo alivyopenda na kunuia.
6 To the prayse of the glory of his grace, wherewith he hath made vs freely accepted in his beloued,
Basi, tumsifu Mungu kwa sababu ya neema yake tukufu katika Mwanae mpenzi!
7 By whom we haue redemption through his blood, euen the forgiuenes of sinnes, according to his rich grace:
Maana kwa damu yake Kristo sisi tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa. Ndivyo ulivyo ukuu wa neema yake
8 Whereby he hath bene aboundant toward vs in all wisedome and vnderstanding,
aliotukirimia bila kipimo! Kwa hekima na ujuzi wake wote
9 And hath opened vnto vs the mysterie of his will according to his good pleasure, which he had purposed in him,
Mungu alitekeleza kile alichonuia, akatujulisha mpango wake uliofichika, ambao alikuwa ameazimia kuutekeleza kwa njia ya Kristo.
10 That in the dispensation of the fulnesse of the times, he might gather together in one all things, both which are in heauen, and which are in earth, euen in Christ:
Mpango huo ambao angeutimiza wakati utimiapo ni kukusanya pamoja viumbe vyote, kila kitu mbinguni na duniani, chini ya Kristo.
11 In whom also we are chosen when we were predestinate according to ye purpose of him, which worketh all things after the counsell of his owne will,
Kila kitu hufanywa kufuatana na mpango na uamuzi wa Mungu; naye Mungu ametuteua sisi tuwe watu wake kwa mapenzi yake katika kuungana na Kristo, kufuatana na azimio alilofanya tangu mwanzo.
12 That we, which first trusted in Christ, should be vnto the praise of his glorie:
Basi, sisi tuliotangulia kumtumainia Kristo tunapaswa kuusifu utukufu wa Mungu!
13 In whom also ye haue trusted, after that ye heard the worde of trueth, euen the Gospel of your saluation, wherein also after that ye beleeued, ye were sealed with the holy Spirite of promise,
Nanyi pia watu wa mataifa mengine, mliusikia ujumbe wa kweli yaani Habari Njema iliyowaletea wokovu, mkamwamini Kristo; naye Mungu, ili kuonyesha kuwa ninyi ni wake, akawapiga mhuri kwa kuwapeni yule Roho Mtakatifu aliyetuahidia.
14 Which is the earnest of our inheritance, for the redemption of that libertie purchased vnto the prayse of his glory.
Huyu Roho ni dhamana ya kurithi yote yale Mungu aliyowaahidia watu wake, na jambo hili latuhakikishia kwamba Mungu atawakomboa kabisa wote walio wake. Tuusifu utukufu wake!
15 Therefore also after that I heard of the faith, which ye haue in the Lord Iesus, and loue toward all the Saints,
Kwa sababu hiyo, tangu niliposikia juu ya imani yenu kwa Bwana Yesu na mapendo yenu kwa watu wa Mungu,
16 I cease not to giue thankes for you, making mention of you in my prayers,
sijaacha kamwe kumshukuru Mungu kwa ajili yenu. Ninawakumbuka katika sala zangu
17 That the God of our Lord Iesus Christ, that Father of glory, might giue vnto you the Spirit of wisedome, and reuelation through the acknowledging of him,
ili Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo Baba mtukufu, awajalieni Roho wake atakayewapa hekima na kuwafunulieni Mungu mpate kumjua.
18 That the eyes of your vnderstanding may be lightened, that ye may knowe what the hope is of his calling, and what the riches of his glorious inheritance is in the Saints,
Namwomba Mungu aifunue mioyo yenu iweze kuuona mwanga wake, mpate kutambua lile tumaini alilowaitieni na utukufu mkuu wa zawadi alizowawekea watu wake,
19 And what is the exceeding greatnesse of his power toward vs, which beleeue, according to the working of his mightie power,
mpate kutambua jinsi uwezo wake ulivyo mkuu mno kwa ajili yetu sisi tunaoamini. Uwezo huo unaofanya kazi ndani yetu, ni sawa na nguvu ile kuu mno
20 Which he wrought in Christ, when he raised him from the dead, and set him at his right hand in the heauenly places,
aliyomfufua nayo Kristo kutoka wafu, akamketisha kulia kwake mbinguni.
21 Farre aboue al principalitie, and power, and might, and domination, and euery Name, that is named, not in this world only, but also in that that is to come, (aiōn )
Huko, Kristo anatawala juu ya kila tawala, mamlaka, enzi na ukuu; anatawala juu ya kila cheo kiwezacho kutajwa katika ulimwengu huu na katika ulimwengu ujao. (aiōn )
22 And hath made all things subiect vnder his feete, and hath giuen him ouer all things to be the head to the Church,
Mungu ameweka vitu vyote chini ya miguu yake, akamkabidhi kwa kanisa akiwa mkuu wa vitu vyote.
23 Which is his body, euen the fulnesse of him that filleth all in all things.
Kanisa ni mwili wa Kristo, na ukamilifu wake yeye anayekamilisha vitu vyote kila mahali.