< Deuteronomy 30 >
1 Nowe when all these things shall come vpon thee, either the blessing or the curse which I haue set before thee, and thou shalt turne into thine heart, among all the nations whither the Lord thy God hath driuen thee,
Vitu hivi vitakavyokuja juu yako, baraka na laana nilizoziweka mbele yako, na utakapozirejea akilini miongoni mwa mataifa mengine ambapo Yahwe Mungu wako kawapeleka,
2 And shalt returne vnto the Lord thy God, and obey his voyce in all that I commaund thee this day: thou, and thy children with all thine heart and with all thy soule,
na utakapomrudia Yahwe Mungu wako na kutii sauti yake, na kufuata yote ambayo nayokuamuru leo – wewe na watoto wako – kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote,
3 Then the Lord thy God wil cause thy captiues to returne, and haue compassion vpon thee, and wil returne, to gather thee out of all the people, where the Lord thy God had scattered thee.
kisha Yahwe Mungu wako atageuza kutekwa kwako na kukuhurumia; atawarudisha na kuwakusanya kutoka kwa watu wote ambapo Yahwe Mungu wako aliwatawanya.
4 Though thou werest cast vnto the vtmost part of heauen, from thence will the Lord thy God gather thee, and from thence wil he take thee,
Iwapo yeyote ya watu walio uhamishoni wapo katika sehemu za mbali sana chini ya mbingu, kutoka huko Yawhe Mungu wako atawakusanya, na kutoka huko atawarejesha.
5 And the Lord thy God will bring thee into the land which thy fathers possessed, and thou shalt possesse it, and he will shewe thee fauour, and will multiplie thee aboue thy fathers.
Yahwe Mungu wako atawaleta katika nchi ambayo mababu zenu walimiliki, nanyi mtaimiliki tena; atawatendea mema na kuwazidisha zaidi ya alivyofanya kwa mababu zenu.
6 And the Lord thy God will circumcise thine heart, and the heart of thy seede, that thou mayest loue the Lord thy God with all thine heart, and with al thy soule, that thou maiest liue.
Yahwe Mungu wako atatahiri moyo wako na moyo wa uzao wako, ili umpende Yahwe Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote, ili kwamba uweze kuishi.
7 And the Lord thy God will lay all these curses vpon thine enemies, and on them, that hate thee, and that persecute thee.
Yahwe Mungu wako ataweka laana hizi zote kwa maadui zako na kwa wote wakuchukiayo, wale waliokutesa.
8 Returne thou therefore, and obey the voyce of the Lord, and do all his commandements, which I commaund thee this day.
Utarudi na kutii sauti ya Yahwe, nawe utatenda amri zake zote ambazo ninakuamuru leo.
9 And the Lord thy God will make thee plenteous in euery worke of thine hande, in the fruite of thy bodie, and in the fruite of thy cattel, and in the fruite of the lande for thy wealth: for the Lord will turne againe, and reioyce ouer thee to do thee good, as he reioyced ouer thy fathers,
Yahwe Mungu wako atakufanikisha katika kazi yote ya mkono wako, katika matunda ya mwili wako, katika matunda ya mifugo yako, na katika matunda ya nchi yako, kwa mafanikio; kwa maana Yahwe atafurahia tena mafanikio yako, kama alivyofurahia kwa baba zako.
10 Because thou shalt obey the voyce of the Lord thy God, in keeping his comandements, and his ordinances, which are written in the booke of this Law, when thou shalt returne vnto the Lord thy God with all thine heart and with al thy soule.
Atafanya hivi iwapo utatii sauti ya Yahwe Mungu wako, ili kuzishika amri zake na kanuni zake zilizoandikwa katika kitabu hiki cha sheria, iwapo utamgeukia Yahwe Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote.
11 For this commandement which I commande thee this day, is not hid from thee, neither is it farre off.
Kwa maana amri hii nayokuamuru leo sio ngumu sana, wala haipo nje ya uwezo wako kufikia.
12 It is not in heauen, that thou shouldest say, Who shall go vp for vs to heauen, and bring it vs, and cause vs to heare it, that we may doe it?
Haipo mbinguni, ili usije ukasema, “Nani atayekwenda kwa ajili yetu mbinguni na kutuletea kwetu na kutufanya tuisikie, ili tuweze kutekeleza?”
13 Neither is it beyonde the sea, that thou shouldest say, Who shall go ouer the sea for vs, and bring it vs, and cause vs to heare it, that we may do it?
Wala haipo ng’ambo ya bahari, ili usije ukasema, “Nani atakwenda ng’ambo ya pili ya bahari kwa ajili yetu na kutuletea kwetu na kutufanya tuisikie, ili tuweze kuifanya?”.
14 But the word is very neere vnto thee: euen in thy mouth and in thine heart, for to do it.
Lakini neno lipo karibu sana kwako, katika kinywa chako na moyo wako, ili uweze kutekeleza.
15 Beholde, I haue set before thee this day life and good, death and euill,
Tazama, leo nimeweka mbele yako uzima na wema, mauti na uovu.
16 In that I commaund thee this day, to loue the Lord thy God, to walke in his wayes, and to keepe his commandements, and his ordinances, and his lawes, that thou mayest liue, and be multiplied, and that the Lord thy God may blesse thee in the land, whither thou goest to possesse it.
Iwapo utatii maagizo ya Yahwe Mungu wako, ambayo ninakuamuru leo kumpenda Yahwe Mungu wako, kutembea katika njia zake, na kushikilia amri zake, kanuni zake, na sheria zake, utaishi na kuongezeka, na Yahwe Mungu wako atakubariki katika nchi ambayo unaingia kumiliki.
17 But if thine heart turne away, so that thou wilt not obey, but shalt be seduced and worship other gods, and serue them,
Lakini moyo wako ukigeuka, na usisikilize na badala yake unavutwa na kusujudia miungu mingine na kuwaabudu,
18 I pronounce vnto you this day, that ye shall surely perish, ye shall not prolong your dayes in the lande, whither thou passest ouer Iorden to possesse it.
basi leo nakutangazia kwako ya kwamba hakika utaangamia; siku zako hazitaongezeka katika nchi unayoipita juu ya Yordani kuingia na kumiliki.
19 I call heauen and earth to recorde this day against you, that I haue set before you life and death, blessing and cursing. therefore chuse life, that both thou and thy seede may liue,
Naziita mbingu na nchi kushuhudia dhidi yako ya kuwa nimeweka mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; kwa hiyo chagua uzima ili kwamba uweze kuishi, wewe na uzao wako.
20 By louing the Lord thy God, by obeying his voyce, and by cleauing vnto him: for he is thy life, and the length of thy dayes: that thou mayest dwell in the lande which the Lord sware vnto thy fathers, Abraham, Izhak, and Iaakob, to giue them.
Fanya hivi ili umpende Yahwe Mungu wako, kutii sauti yake, na kung’ang’ania kwake. Kwa maana yeye ni uzima wako na urefu wa siku zako; fanya hivi ili kwamba uweze kuishi katika nchi ambayo Yahwe aliapa kwa mababu zako, kwa Abrahamu, kwa Isaka, na kwa Yakobo, kuwapatia.