< Daniel 1 >

1 In the thirde yeere of the reigne of Iehoiakim king of Iudah, came Nebuchad-nezzar King of Babel vnto Ierusalem and besieged it.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuja akazingira Yerusalemu kwa jeshi.
2 And ye Lord gaue Iehoiakim king of Iudah into his hand; with parte of the vessels of the house of God, which he caryed into the land of Shinar, to the house of his god, and he brought the vessels into his gods treasurie.
Bwana akamtia Yehoyakimu mfalme wa Yuda mkononi mwa Nebukadneza, pamoja na baadhi ya vyombo kutoka Hekalu la Mungu. Hivi akavichukua hadi kwenye hekalu la mungu wake huko Shinari, naye akaviweka nyumbani ya hazina ya mungu wake.
3 And the King spake vnto Ashpenaz the master of his Eunuches, that he shoulde bring certeine of the children of Israel, of the Kings seede, and of the princes:
Kisha mfalme akamwagiza Ashpenazi, mkuu wa maafisa wa mfalme, kumletea baadhi ya Waisraeli kutoka jamaa ya mfalme na kutoka jamaa kuu,
4 Children in whome was no blemish, but well fauoured, and instruct in all wisedome, and well seene in knowledge, and able to vtter knowledge, and such as were able to stande in the kings palace, and whome they might teach the learning, and the tongue of the Caldeans.
vijana wanaume wasio na dosari mwilini, wenye sura nzuri, wanaoonyesha kipaji katika kila aina ya elimu, wenye ufahamu mzuri, wepesi kuelewa, na waliofuzu kuhudumu katika jumba la kifalme. Alikuwa awafundishe lugha na maandiko ya Wakaldayo.
5 And the King appointed them prouision euery day of a portion of the Kings meate, and and of the wine, which he dranke, so nourishing them three yeere, that at the ende thereof, they might stande before the King.
Mfalme akawaagizia kiasi cha chakula na divai ya kila siku kutoka meza ya mfalme. Walikuwa wafundishwe kwa miaka mitatu, na hatimaye waingie kwenye utumishi wa mfalme.
6 Nowe among these were certeine of the children of Iudah, Daniel, Hananiah, Mishael and Azariah.
Baadhi ya hawa vijana walitoka Yuda: nao ni Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria.
7 Vnto whome the chiefe of the Eunuches gaue other names: for hee called Daniel, Belteshazzar, and Hananiah, Shadrach, and Mishael, Meshach, and Azariah, Abednego.
Mkuu wa maafisa akawapa majina mapya: Danieli akamwita Belteshaza, Hanania akamwita Shadraki, Mishaeli akamwita Meshaki, na Azaria akamwita Abednego.
8 But Daniel had determined in his heart, that hee woulde not defile him selfe with the portion of the Kings meate, nor with the wine which he dranke: therefore he required the chiefe of the Eunuches that he might not defile himselfe.
Lakini Danieli alikusudia kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme na divai, naye akamwomba mkuu wa maafisa ruhusa ili asijinajisi kwa njia hii.
9 (Nowe God had brought Daniel into fauour, and tender loue with the chiefe of the Eunuches)
Basi Mungu alikuwa amemfanya huyo mkuu wa maafisa kuonyesha upendeleo na huruma kwa Danieli,
10 And the chiefe of the Eunuches sayd vnto Daniel, I feare my lord the King, who hath appointed your meate and your drinke: therefore if he see your faces worse liking then the other children, which are of your sort, then shall you make me lose mine head vnto the King.
lakini huyo mkuu wa maafisa akamwambia Danieli, “Ninamwogopa bwana wangu mfalme, aliyeagizia chakula na kinywaji chenu. Kwa nini aone nyuso zenu zikiwa mbaya kuliko za vijana wengine wa rika lenu? Mfalme atakata kichwa changu kwa sababu yenu.”
11 Then sayd Daniel to Melzar, whome the chiefe of the Eunuches had set ouer Daniel, Hananiah, Mishael, and Azariah,
Ndipo Danieli akamwambia mlinzi aliyeteuliwa na huyo mkuu wa maafisa kuwasimamia Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria,
12 Proue thy seruants, I beseeche thee, ten dayes, and let them giue vs pulse to eate, and water to drinke.
“Tafadhali wajaribu watumishi wako kwa siku kumi. Usitupe chochote ila nafaka na mboga za majani tule, na maji ya kunywa.
13 Then let our countenances bee looked vpon before thee, and the countenances of the children that eate of the portion of the Kings meate: and as thou seest, deale with thy seruantes.
Baadaye ulinganishe sura zetu na vijana wanaokula chakula cha mfalme, ukawatendee watumishi wako kulingana na unachoona.”
14 So hee consented to them in this matter, an proued them ten dayes.
Basi akakubali jambo hili, akawajaribu kwa siku kumi.
15 And at the end of ten dayes, their countenances appeared fayrer, and in better liking then all the childrens, which did eate the portion of the Kings meate.
Mwisho wa zile siku kumi, walionekana kuwa na afya na kunawiri zaidi kuliko yeyote kati ya wale vijana waliokula chakula cha mfalme.
16 Thus Melzar tooke away the portion of their meat, and the wine that they should drinke, and gaue them pulse.
Hivyo mlinzi wao akaondoa chakula chao na divai yao waliopangiwa kula na kunywa, akawapa nafaka na mboga za majani badala yake.
17 As for these foure children, God gaue them knowledge, and vnderstanding in al learning and wisedome: also he gaue Daniel vnderstanding of all visions and dreames.
Mungu akawapa hawa vijana wanne maarifa na ufahamu wa kila aina ya maandiko na elimu. Naye Danieli aliweza kufahamu maono na aina zote za ndoto.
18 Nowe when the time was expired, that the King had appoynted to bring them in, the chiefe of the Eunuches brought them before Nebuchad-nezzar.
Mwisho wa muda uliowekwa na mfalme kuwaingiza kwake, mkuu wa maafisa akawaleta mbele ya Mfalme Nebukadneza.
19 And the King communed with them: and among them al was found none like Daniel, Hananiah, Mishael, and Azariah: therefore stoode they before the king.
Mfalme akazungumza nao, akaona hakuna aliyelingana na Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria. Hivyo wakaingia katika utumishi wa mfalme.
20 And in all matters of wisedome, and vnderstanding that the King enquired of them, hee founde them tenne times better then all the inchanters and astrologians, that were in all his realme.
Katika kila jambo la hekima na ufahamu kuhusu kile mfalme alichowauliza, aliwaona bora mara kumi zaidi kuliko waganga na wasihiri wote katika ufalme wake wote.
21 And Daniel was vnto the first yeere of king Cyrus.
Naye Danieli akabaki huko mpaka mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi.

< Daniel 1 >