< Daniel 8 >
1 In the thirde yeere of the reigne of King Belshazzar, a vision appeared vnto mee, euen vnto me Daniel, after that which appeared vnto mee at the first.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mfalme Belshaza, mimi Danieli niliona maono (baada ya maono ya awali yaliyonipata).
2 And I saw in a vision, and when I sawe it, I was in the palace of Shushan, which is in the prouince of Elam, and in a vision me thought I was by the riuer of Vlai.
Nilipokuwa nikiangalia katika ndoto, niliona kwamba nilikuwa katika mji wa Shushani wenye ngome katika jimbo la Elamu. Niliona katika ndoto kuwa nilikuwa karibu na mfereji wa Ulai.
3 Then I looked vp and sawe, and beholde, there stoode before the riuer a ramme, which had two hornes: and these two hornes were hie: but one was hier then another, and the hyest came vp last.
Nilitazama juu na nikaona mbele yangu kondoo dume lenye mapembe mawili, limesimama pembeni mwa mfereji. Pembe moja lilikuwa refu kuliko jingine, lakini pembe ndefu ilikuwa inakua pole pole kuliko ile fupi na pembe fupi ilirefuka na kuizidi nyingine.
4 I sawe the ramme pusshing against ye West, and against the North, and against the South: so that no beastes might stande before him, nor could deliuer out of his hand, but he did what he listed, and became great.
Niliona kondoo mme akiishambulia magharibi, kisha kaskazini, na baadaye kusini; hakuna mnyama mwingine aliyeweza kusimama mbele yake. Hakuna yeyote aliyeweza kumwokoa yeyote katika mkono wake. Alifanya chochote kile alichokitaka, na alikuwa mtu mkubwa sana.
5 And as I considered, beholde, a goate came from the West ouer the whole earth, and touched not the grounde: and this goate had an horne that appeared betweene his eyes.
Na nilipokuwa natafakari juu ya haya, niliona beberu akitoka magharibi, na kuvuka katika uso wa dunia yote, akikimbia kwa kasi kana kwamba hakuonekana kama aligusa ardhini. Mbuzi huyo alikuwa na pembe kubwa katikati ya macho yake.
6 And he came vnto the ramme that had the two hornes, whome I had seene standing by the riuer, and ranne vnto him in his fierce rage.
Alienda mpaka kwa kondoo aliyekuwa na pembe mbili, nilikuwa nimemwona kondoo dume amesimama katika ukingo wa mfereji na mbuzi alikimbia kumwelekea kondoo dume kwa hasira kali.
7 And I saw him come vnto the ramme, and being moued against him, he smote the ramme, and brake his two hornes: and there was no power in the ramme to stand against him, but he cast him downe to the grounde, and stamped vpon him, and there was none that coulde deliuer the ramme out of his power.
Niliiona mbuzi ikija karibu na kondoo. Mbuzi alikuwa na hasira na kondoo, alimpiga kondoo na alizivunja pembe zake mbili. Kondoo hakuwa na nguvu za kusimama mbele zake. Mbuzi alimgonga kondoo akaanguka chini na akamkanyaga. Hapakuwa na yeyote wa kumwokoa kutoka katika nguvu zake.
8 Therefore the goate waxed exceeding great, and when he was at the strongest, his great horne was broken: and for it came vp foure that appeared toward the foure windes of ye heauen.
Ndipo mbuzi alikua akawa mkubwa, lakini alipokuwa na nguvu, pembe kubwa ilivunjwa, na katika sehemu yake zilichipuka na kukua pembe nne kubwa zilizochomoza kuelekea pepo nne za mbingu.
9 And out of one of them came foorth a litle horne, which waxed very great toward the South, and toward the East, and towarde the pleasant land.
Kutoka katika pembe moja ilichipuka pembe nyingine, ilikuwa ndogo hapo awali, lakini baadaye ilikuwa pembe kubwa upande wa kusini, na mashariki, na katika nchi ya uzuri.
10 Yea, it grewe vp vnto the hoste of heauen, and it cast downe some of the hoste, and of the starres to the ground, and trode vpon them,
Pembe ilikuwa kubwa na matokeo yake iliinua vita dhidi ya jeshi la mbinguni. Baadhi ya jeshi na nyota kadhaa zilitupwa chini duniani, na zilikanyagwa.
11 And extolled himselfe against the prince of the hoste from whome the dayly sacrifice was taken away, and the place of his Sanctuarie was cast downe.
Alizidi kuwa mkubwa, mkubwa kama kamanda wa jeshi la kimungu. Sadaka za kuteketezwa za kila siku ziliondolewa mbali na yeye, na sehemu yake takatifu zilitiwa unajisi.
12 And a time shall be giuen him ouer the dayly sacrifice for the iniquitie: and it shall cast downe the trueth to the ground, and thus shall it doe, and prosper.
Kwasababu ya uasi, pembe ya mbuzi ilipewa jeshi, na sadaka za kuteketezwa zitasitishwa. Pembe itautupa ukweli chini ardhini, na itafanikiwa katika kila jambo ilifanyalo.
13 Then I heard one of the Saints speaking, and one of the Saints spake vnto a certaine one, saying, Howe long shall endure the vision of the dayly sacrifice, and the iniquitie of the desolation to treade both the Sanctuarie and the armie vnder foote?
Kisha nilimsikia mtakatifu mmoja akiongea na mtakatifu mwingine akamjibu, “Mambo haya yatadumu kwa muda gani, maono haya ya sadaka ya kuteketezwa, dhambi ile iletayo uharibifu, ukabidhiajia wa sehemu takatifu, na jeshi la mbinguni kukanyagwa?
14 And he answered me, Vnto the euening and the morning, two thousand and three hundreth: then shall the Sanctuarie be clensed.
Aliniambia, “Itadumu kwa jioni na asubuhi zipatazo 2, 300. Baada ya hapo, mahali patakatifu patawekwa sawa.”
15 Nowe when I Daniel had seene the vision, and sought for the meaning, beholde, there stoode before me like the similitude of a man.
Wakati mimi Danieli, nilipoona maono, nilijaribu kuyaelewa. na hapo mbele yangu alisimama yule aliyeoneakana kama mtu.
16 And I heard a mans voyce betweene the bankes of Vlai, which called, and sayde, Gabriel, make this man to vnderstand the vision.
Niliisikia sauti ya mtu ikiita katikati ya kingo za mfereji wa Ulai. Alisema, “Gabrieli, msaidie mtu huyu kuelewa maono.”
17 So he came where I stood: and when hee came, I was afraide, and fell vpon my face: but he sayd vnto me, Vnderstand, O sonne of man: for in the last time shalbe the vision.
Basi alikuja karibu na mahali niliposimama. Na alipokuja, niliogopa na nilisujudia hadi chini. Aliniambia,”Fahamu, mwana wa mtu, kwamba maono ni kwa ajili ya wakati wa mwisho.”
18 Nowe as he was speaking vnto me, I being a sleepe fell on my face to the ground: but he touched me, and set me vp in my place.
Alipokuwa anaongea na mimi, nilipata usiingizi mzito nikiwa nimelala kifudifudi. Kisha alinishika na kunisimamisha.
19 And he sayde, Beholde, I will shewe thee what shalbe in the last wrath: for in the end of the time appointed it shall come.
Akaniambia, “Tazama, nitakuonyesha kile kitachotokea baadaye katika kipindi cha ghadhabu, kwasababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho uliopangwa.
20 The ramme which thou sawest hauing two hornes, are the Kings of the Medes and Persians.
Na kuhusu kondoo mme uliyemwona, yule mwenye pembe mbili - ni wafalme wawili wa Umedi na Uajemi.
21 And the goate is the King of Grecia, and the great horne that is betweene his eyes, is the first King.
Mbuzi dume ni mfalme wa Ugiriki. Pembe kubwa katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
22 And that that is broken, and foure stoode vp for it, are foure kingdomes, which shall stand vp of that nation, but not in his strength.
Na kuhusu pembe iliyovunjika, ambayo katika nafasi yake pembe zingine nne zilichipuka - hizi ni falme nne zitakazoinuka kutoka katika taifa lake, lakini hazitakuwa na nguvu kubwa.
23 And in the end of their kingdome, when the rebellious shalbe consumed, a King of fierce countenance, and vnderstanding darke sentences, shall stand vp.
Katika siku zijazo za falme hizo, wakati ambapo wahalifu watakuwa wamefikia kikomo chao, mfalme mwenye uso katili, na yeye mwenye akili sana, atainuka.
24 And his power shalbe mightie, but not in his strength: and hee shall destroy wonderfully, and shall prosper, and practise, and shall destroy the mightie, and the holy people.
Nguvu zake zitakuwa kubwa, lakini si kwa nguvu zake mwenyewe. Atakuwa wa kustaajabisha kwa kile atakachokuwa anakiharibu; atafanya na kufanikiwa. Atawaangamiza watu wenye nguvu, watu miongoni wa watakatifu.
25 And through his policie also, hee shall cause craft to prosper in his hand, and he shall extoll himselfe in his heart, and by peace shall destroy many: hee shall also stande vp against the prince of princes, but he shalbe broken downe without hand.
Ataufanya udanganyifu usitawi chini ya mkono wake kwasababu ya ujanja wake. Atawaangamiza watu wengi bila kutegemea. Atainuka pia hata kinyume cha Mfalme wa wafalme, na atavunjwa, lakini si kwa mkono wowote wa binadamu.
26 And the vision of the euening and the morning, which is declared, is true: therefore seale thou vp the vision, for it shall be after many dayes.
Maono kuhusu jioni na asubuhi ulizoambiwa ni ya kweli. Lakini uyafunge maono haya, kwa kuwa yanahusu siku nyingi za wakati ujao.
27 And I Daniel was striken and sicke certaine dayes: but when I rose vp, I did the Kings busines, and I was astonished at the vision, but none vnderstood it.
Ndipo mimi, Danieli nilichoka sana na nikalala nikiwa dhaifu kwa siku kadhaa. Kisha nikainuka na nikaenda kufanya kazi za mfalme. Lakini nilikuwa nimetishwa sana na maono, na hapakuwa na mtu yeyote aliyeweza kuyaelewa.