< Daniel 4 >

1 Nebuchad-nezzar King vnto all people, nations and languages, that dwell in all the world, Peace be multiplied vnto you:
Mfalme Nebukadneza, Kwa kabila za watu, mataifa na watu wa kila lugha, wanaoishi katika ulimwengu wote: Mafanikio yawe kwenu sana!
2 I thought it good to declare the signes and wonders, that the hie God hath wrought toward me.
Ni furaha yangu kuwaambia kuhusu ishara za miujiza na maajabu ambayo Mungu Aliye Juu Sana amenifanyia.
3 How great are his signes, and how mightie are his wonders! his kingdome is an euerlasting kingdome, and his dominion is from generation to generation.
Ishara zake ni kuu aje, na maajabu yake yana nguvu aje! Ufalme wake ni ufalme wa milele; enzi yake hudumu kutoka kizazi hadi kizazi.
4 I Nebuchad-nezzar being at rest in mine house, and flourishing in my palace,
Mimi, Nebukadneza, nilikuwa nyumbani katika jumba langu la kifalme, nikiwa ninaishi kwa raha na hali ya kufanikiwa.
5 Saw a dreame, which made me afraide, and the thoughtes vpon my bed, and the visions of mine head troubled me.
Niliota ndoto iliyoniogopesha. Nilipokuwa nimelala kitandani mwangu, njozi na maono yaliyopita mawazoni mwangu vilinitisha.
6 Therefore made I a decree, that they should bring all the wise men of Babel before mee, that they might declare vnto me the interpretation of the dreame.
Hivyo nikaagiza kwamba watu wote wenye hekima wa Babeli waletwe mbele yangu kunifasiria ndoto yangu.
7 So came the inchanters, the astrologians, the Caldeans and the sothsayers, to whom I tolde the dreame, but they could not shew me the interpretation thereof,
Walipokuja waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi, niliwaambia ndoto yangu, lakini hawakuweza kunifasiria.
8 Till at the last Daniel came before mee, (whose name was Belteshazzar, according to the name of my god, which hath the spirite of the holy gods in him) and before him I tolde the dreame, saying,
Mwishoni, Danieli alikuja mbele yangu nikamweleza hiyo ndoto. (Danieli anaitwa Belteshaza, kwa jina la mungu wangu, nayo roho ya miungu mitakatifu inakaa ndani yake.)
9 O Belteshazzar, chiefe of the enchanters, because I know, that the spirit of the holy gods is in thee, and no secret troubleth thee, tell mee the visions of my dreame, that I haue seene and the interpretation thereof.
Nilisema, “Belteshaza, mkuu wa waganga, ninajua kuwa roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, wala hakuna siri iliyo ngumu kwako. Hii ndiyo ndoto yangu, nifasirie.
10 Thus were the visions of mine head in my bed. And beholde, I sawe a tree in the middes of the earth and the height thereof was great:
Haya ndiyo maono niliyoona nilipokuwa nimelala kitandani mwangu: Nilitazama, na mbele yangu ulisimama mti katikati ya nchi. Ulikuwa mrefu sana.
11 A great tree and strong, and the height thereof reached vnto heauen, and the sight thereof to the endes of all the earth.
Mti ule ulikua, ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga; ulionekana mpaka miisho ya dunia.
12 The boughes thereof were faire and the fruite thereof much, and in it was meate for all: it made a shadow vnder it for the beastes of the fielde, and the foules of the heauen dwelt in the boughes thereof, and all flesh fedde of it.
Majani yake yalikuwa ya kupendeza, matunda yake yalikuwa mengi, na juu yake kulikuwa na chakula kwa ajili ya wote. Chini ya kivuli chake wanyama wa kondeni walipata hifadhi, na ndege wa angani waliishi katika matawi yake. Kila kiumbe kililishwa kutokana na mti huo.
13 I sawe in the visions of mine head vpon my bed, and beholde, a watchman and an holy one came downe from heauen,
“Katika maono niliyoyaona nikiwa nimelala kitandani mwangu, nilitazama, na mbele yangu alikuwepo mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni.
14 And cried aloude, and said thus, Hew downe the tree, and breake off his branches: shake off his leaues, and scatter his fruite, that the beastes may flee from vnder it, and the foules from his branches.
Akaita kwa sauti kubwa: ‘Kateni mti huu, myafyeke matawi yake; yaondoeni majani yake na kuyatawanya matunda yake. Wanyama na wakimbie kutoka chini yake na ndege waondoke kutoka matawi yake.
15 Neuerthelesse leaue the stumpe of his rootes in the earth, and with a band of yron and brasse binde it among the grasse of the fielde, and let it be wet with the dewe of heauen, and let his portion be with the beastes among the grasse of the fielde.
Lakini acheni kisiki chake na mizizi, kikiwa kimefungwa kwa chuma na shaba, kibaki ardhini, kwenye majani ya kondeni. “‘Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, naye aachwe aishi pamoja na wanyama miongoni mwa mimea ya dunia.
16 Let his heart be changed from mans nature, and let a beasts heart be giuen vnto him, and let seuen times be passed ouer him.
Akili yake na ibadilishwe kutoka ile ya mwanadamu na apewe akili ya mnyama, mpaka nyakati saba zipite juu yake.
17 The sentence is according to the decree of the watchmen, and according to the word of the holy ones: the demaunde was answered, to the intent that liuing men may knowe, that the most High hath power ouer the kingdome of men, and giueth it to whomsoeuer he will, and appointeth ouer it the most abiect among men.
“‘Uamuzi huu umetangazwa na walinzi, hukumu imetangazwa na watakatifu, ili walio hai wajue kuwa Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme zote za wanadamu, naye humpa yeyote amtakaye na kumtawaza juu yake hata yeye aliye mnyonge sana miongoni mwa wanadamu.’
18 This is the dreame, that I King Nebuchad-nezzar haue seene: therefore thou, O Belteshazzar, declare the interpretation thereof: for all the wisemen of my kingdome are not able to shewe mee the interpretation: but thou art able, for the spirit of the holy gods is in thee.
“Hii ndiyo ndoto niliyoipata mimi, Mfalme Nebukadneza. Sasa Belteshaza, niambie maana yake, kwa maana hakuna hata mmoja wa wenye hekima katika ufalme wangu anayeweza kunifasiria. Bali wewe waweza, kwa sababu roho ya miungu mitakatifu imo ndani yako.”
19 Then Daniel (whose name was Belteshazzar) held his peace by the space of one houre, and his thoughts troubled him, and the King spake and said, Belteshazzar, let neither the dreame, nor the interpretation thereof trouble thee. Belteshazzar answered and saide, My lord, the dreame be to them that hate thee, and the interpretation thereof to thine enemies.
Ndipo Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza) alipofadhaika sana kwa muda, nayo mawazo yake yakamtia hofu. Basi mfalme akasema, “Belteshaza, usiruhusu ndoto wala maana yake kukutia hofu.” Belteshaza akamjibu, “Bwana wangu, laiti ndoto hii ingehusu adui zako, na maana yake iwahusu watesi wako!
20 The tree that thou sawest, which was great and mightie, whose height reached vnto the heauen, and the sight thereof through all the world,
Mti uliouona, uliokua ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga na kuonekana duniani kote,
21 Whose leaues were faire and the fruit thereof much, and in it was meate for all, vnder the which the beastes of the fielde dwelt, and vpon whose branches the foules of the heauen did sit,
ukiwa na majani ya kupendeza na matunda mengi, ukitoa chakula kwa wote, na ukiwapa hifadhi wanyama wa kondeni na kuwa mahali pa viota katika matawi yake kwa ajili ya ndege wa angani.
22 It is thou, O King, that art great and mightie: for thy greatnesse is growen, and reacheth vnto heauen, and thy dominion to the endes of the earth.
Ee mfalme, wewe ndiwe ule mti! Umekuwa mkubwa na mwenye nguvu, nao ukuu wako umekua mpaka kufika juu angani, nayo mamlaka yako yameenea mpaka miisho ya dunia.
23 Where as the King sawe a watchman, and an holy one, that came downe from heauen, and said, Hew downe the tree and destroy it, yet leaue the stumpe of the rootes thereof in the earth, and with a bande of yron and brasse binde it among the grasse of the fielde, and let it be wette with the dewe of heauen, and let his portion be with the beastes of the fielde, till seuen times passe ouer him,
“Ee mfalme, wewe ulimwona mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni na kusema, ‘Ukateni mti na kuuangamiza, lakini kiacheni kisiki kikiwa kimefungwa kwa chuma na kwa shaba, kwenye majani ya kondeni, wakati mizizi yake inabaki ardhini. Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, mwacheni aishi kama wanyama pori mpaka nyakati saba zipite juu yake.’
24 This is the interpretation, O King, and it is the decree of the most High, which is come vpon my lord the King,
“Ee mfalme, hii ndiyo tafsiri, na hii ni amri ya Aliye Juu Sana aliyoitoa dhidi ya bwana wangu mfalme:
25 That they shall driue thee from men, and thy dwelling shalbe with the beasts of the fielde: they shall make thee to eate grasse as the oxen, and they shall wet thee with the dewe of heauen: and seuen times shall passe ouer thee, till thou knowe, that the most High beareth rule ouer the kingdome of men, and giueth it to whom so euer he will.
Wewe utafukuzwa mbali na wanadamu, nawe utaishi pamoja na wanyama pori; utakula manyasi kama ngʼombe, na kuloana kwa umande wa mbinguni. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.
26 Where as they sayd, that one should leaue the stumpe of the tree rootes, thy kingdome shall remaine vnto thee: after that, thou shalt knowe, that the heauens haue the rule.
Amri ya kuacha kisiki pamoja na mizizi yake inamaanisha kwamba ufalme wako utarejezwa kwako utakapokubali kwamba Mbingu ndizo zitawalazo.
27 Wherefore, O King, let my counsell be acceptable vnto thee, and breake off thy sinnes by righteousnes, and thine iniquities by mercy toward the poore: lo, let there be an healing of thine errour.
Kwa hiyo, ee mfalme, uwe radhi kupokea shauri langu: Acha dhambi zako kwa kutenda yaliyo haki, ukaache uovu wako, na uwe na huruma kwa walioonewa. Hivyo itawezekana baada ya hayo, mafanikio yako yakaendelea.”
28 All these things shall come vpon the King Nebuchad-nezzar.
Haya yote yalimpata Mfalme Nebukadneza.
29 At the end of twelue moneths, he walked in the royall palace of Babel.
Miezi kumi na miwili baadaye, mfalme alipokuwa akitembea juu ya paa la jumba la kifalme la Babeli,
30 And the King spake and sayde, Is not this great Babel, that I haue built for the house of the kingdome by the might of my power, and for the honour of my maiestie?
alisema, “Je, huu si Babeli mji mkuu nilioujenga kama makao ya kifalme, kwa uwezo wangu mkubwa, na kwa ajili ya utukufu wa enzi yangu?”
31 While the worde was in the Kings mouth, a voyce came downe from heauen, saying, O King Nebuchad-nezzar, to thee be it spoken, Thy kingdome is departed from thee,
Maneno hayo yalikuwa bado katika midomo yake wakati sauti ilipokuja kutoka mbinguni, ikisema, “Mfalme Nebukadneza, hiki ndicho kilichoamriwa kwa ajili yako: Mamlaka yako ya ufalme yameondolewa kutoka kwako.
32 And they shall driue thee from men, and thy dwelling shalbe with the beastes of the fielde: they shall make thee to eate grasse, as the oxen, and seuen times shall passe ouer thee, vntill thou knowest, that the most High beareth rule ouer the kingdome of men, and giueth it vnto whomsoeuer he will.
Utafukuzwa mbali na wanadamu, ukaishi pamoja na wanyama pori, na utakula manyasi kama ngʼombe. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.”
33 The very same houre was this thing fulfilled vpon Nebuchad-nezzar, and hee was driuen from men, and did eate grasse as the oxen, and his body was wet with the dewe of heauen, till his heares were growen as eagles feathers, and his nailes like birds clawes.
Papo hapo yale yaliyokuwa yamesemwa kuhusu Nebukadneza yakatimia. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akala majani kama ngʼombe. Mwili wake uliloweshwa kwa umande wa mbinguni mpaka nywele zake zikakua kama manyoya ya tai na kucha zake kama makucha ya ndege.
34 And at the ende of these dayes I Nebuchad-nezzar lift vp mine eyes vnto heauen, and mine vnderstanding was restored vnto me, and I gaue thankes vnto the most High, and I praysed and honoured him that liueth for euer, whose power is an euerlasting power, and his kingdome is from generation to generation.
Mwisho wa huo wakati, mimi Nebukadneza, niliinua macho yangu kuelekea mbinguni, nazo fahamu zangu zikanirudia. Ndipo nikamsifu Yeye Aliye Juu Sana, nikamheshimu na kumhimidi yeye aishiye milele. Utawala wake ni utawala wa milele; ufalme wake hudumu kutoka kizazi na kizazi.
35 And all the inhabitants of the earth are reputed as nothing: and according to his will he worketh in the armie of heauen, and in the inhabitants of the earth: and none can stay his hand, nor say vnto him, What doest thou?
Mataifa yote ya dunia yanahesabiwa kuwa si kitu. Hufanya kama atakavyo kwa majeshi ya mbinguni, na kwa mataifa ya dunia. Hakuna anayeweza kuuzuia mkono wake au kumwambia, “Umefanya nini wewe?”
36 At the same time was mine vnderstanding restored vnto me, and I returned to the honour of my kingdome: my glory and my beautie was restored vnto me, and my counsellours and my princes sought vnto me, and I was established in my kingdome, and my glory was augmented toward me.
Wakati huo huo fahamu zangu ziliponirudia, nikarudishiwa heshima yangu na fahari yangu kwa ajili ya utukufu wa ufalme wangu. Washauri wangu na wakuu wangu walikuja kunitafuta, nami nikarudishwa kwenye kiti changu cha ufalme hata nikawa mkuu kuliko mwanzoni.
37 Now therefore I Nebuchad-nezzar prayse and extoll and magnifie the King of heauen, whose workes are all trueth, and his wayes iudgement, and those that walke in pride, he is able to abase.
Basi mimi, Nebukadneza, humhimidi, na humtukuza na kumsifu Mfalme wa mbinguni, kwa sababu kila kitu afanyacho ni haki, na njia zake zote ni adili. Nao waendao kwa kiburi anaweza kuwashusha.

< Daniel 4 >