< Daniel 11 >
1 Also I, in ye first yere of Darius of ye Medes, euen I stood to incourage and to strengthen him.
Nami katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario Mmedi, nilisimama kumsaidia na kumlinda.)
2 And now wil I shew thee ye trueth, Behold, there shall stand vp yet three Kings in Persia, and the fourth shall be farre richer then they all: and by his strength, and by his riches he shall stirre vp all against the realme of Grecia.
“Sasa basi, ninakuambia kweli: Wafalme watatu zaidi watatokea Uajemi, kisha atatokea mfalme wa nne, ambaye atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Wakati atakapokuwa amekwisha kujipatia nguvu kwa utajiri wake, atamchochea kila mmoja dhidi ya ufalme wa Uyunani.
3 But a mightie King shall stand vp, that shall rule with great dominion, and doe according to his pleasure.
Ndipo mfalme mwenye nguvu atatokea, ambaye atatawala kwa nguvu nyingi na kufanya anavyopenda.
4 And when he shall stand vp, his kingdome shall be broken, and shall be deuided towarde the foure windes of heauen: and not to his posteritie, nor according to his dominion, which he ruled: for his kingdome shall be pluckt vp, euen to be for others besides those.
Baada ya kujitokeza, milki yake itavunjwa na kugawanyika katika pande nne za mbinguni. Hautakwenda kwa wazao wake, wala hautakuwa na nguvu alizotumia, kwa sababu milki yake itangʼolewa na kupewa wengine.
5 And ye King of ye South shalbe mightie, and one of his princes, and shall preuaile against him, and beare rule: his dominio shalbe a great dominion.
“Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja wa majemadari wake atakuwa na nguvu zaidi kuliko mfalme, naye atatawala ufalme wake mwenyewe kwa nguvu nyingi.
6 And in the ende of yeeres they shalbe ioyned together: for the Kings daughter of ye South shall come to the King of the North to make an agreement, but she shall not reteine the power of the arme, neither shall he continue, nor his arme: but she shall be deliuered to death, and they that brought her, and he that begate her, and he that comforted her in these times.
Baada ya miaka kadha, wataungana. Binti wa mfalme wa Kusini ataolewa kwa mfalme wa Kaskazini ili kuimarisha mapatano, lakini huyo binti nguvu zake hazitadumu; hata mfalme hatadumu wala nguvu zake. Katika siku hizo atafukuzwa, pamoja na hao wasindikizaji wake wa kifalme, watoto wake, na yeyote aliyemuunga mkono.
7 But out of the bud of her rootes shall one stand vp in his stead, which shall come with an armie, and shall enter into the fortresse of the King of the North, and doe with them as he list, and shall preuaile,
“Mmoja kutoka jamaa ya huyo binti atainuka na kuchukua nafasi yake. Atashambulia majeshi ya mfalme wa Kaskazini na kuingia katika ngome yake; atapigana dhidi yao naye atashinda.
8 And shall also carie captiues into Egypt their gods with their molten images, and with their precious vessels of siluer and of golde, and he shall continue more yeeres then the King of the North.
Tena ataitwaa miungu yao, vinyago vyao vya chuma, na vitu vyao vya thamani vya fedha na dhahabu, na kuvichukua hadi Misri. Kwa miaka kadha atamwacha mfalme wa Kaskazini bila kumsumbua.
9 So the King of ye South shall come into his kingdome, and shall returne into his owne land.
Kisha mfalme wa Kaskazini atashambulia nchi ya mfalme wa Kusini, lakini atarudi nyuma hadi kwenye nchi yake.
10 Wherefore his sonnes shall be stirred vp, and shall assemble a mightie great armie: and one shall come, and ouerflowe, and passe through: then shall he returne, and be stirred vp at his fortresse.
Wana wa mfalme wa Kaskazini watajiandaa kwa vita na kukusanya jeshi kubwa, ambalo litafagia nchi kama mafuriko yasiyozuilika na kuendelea na vita hadi kwenye ngome ya mfalme wa Kusini.
11 And the King of the South shall be angrie, and shall come foorth, and fight with him, euen with the King of the North: for he shall set foorth a great multitude, and the multitude shall be giuen into his hand.
“Kisha mfalme wa Kusini atatoka kwa ghadhabu na kupigana dhidi ya mfalme wa Kaskazini, ambaye ataunda jeshi kubwa, lakini litashindwa.
12 Then the multitude shall be proude, and their heart shall be lifted vp: for hee shall cast downe thousands: but he shall not still preuaile.
Wakati jeshi litakapokuwa limechukuliwa, mfalme wa Kusini atajawa na kiburi na atachinja maelfu mengi, hata hivyo hatabaki na ushindi.
13 For the King of the North shall returne, and shall set foorth a greater multitude then afore, and shall come foorth (after certeine yeeres) with a mightie armie, and great riches.
Kwa maana mfalme wa Kaskazini atakusanya jeshi jingine kubwa kuliko lile la kwanza; na baada ya miaka kadha, atasonga mbele na jeshi kubwa mno lililoandaliwa vizuri.
14 And at the same time there shall many stand vp against the King of the South: also the rebellious children of thy people shall exalt them selues to establish the vision, but they shall fall.
“Katika nyakati hizo wengi watainuka dhidi ya mfalme wa Kusini. Watu wenye ghasia miongoni mwa watu wako mwenyewe wataasi ili kutimiza maono, lakini bila mafanikio.
15 So the King of the North shall come, and cast vp a mount, and take the strong citie: and the armes of the South shall not resist, neither his chosen people, neither shall there be any strength to withstand.
Ndipo mfalme wa Kaskazini atakuja na kuuzunguka mji kwa majeshi, na kuuteka mji wa ngome. Majeshi ya Kusini yatakosa nguvu za kuyazuia; naam, hata vikosi vyao vya askari vilivyo bora zaidi, havitakuwa na nguvu ya kuwakabili.
16 But he that shall come, shall doe vnto him as he list, and none shall stand against him: and he shall stand in the pleasant land, which by his hand shalbe consumed.
Huyo mvamia nchi atafanya apendavyo; hakuna yeyote atakayeweza kumpinga. Atajiimarisha katika Nchi ya Kupendeza, na atakuwa na uwezo wa kuiangamiza.
17 Againe he shall set his face to enter with the power of his whole kingdome, and his confederates with him: thus shall he doe, and he shall giue him the daughter of women, to destroy her: but she shall not stande on his side, neither bee for him.
Ataamua kuja na nguvu za ufalme wake wote na kufanya mapatano ya amani na mfalme wa Kusini. Naye atamtoa binti yake aolewe naye ili kuuangusha ufalme, lakini mipango yake haitafanikiwa wala kumsaidia.
18 After this shall he turne his face vnto the yles, and shall take many, but a prince shall cause his shame to light vpon him, beside that he shall cause his owne shame to turne vpon himselfe.
Ndipo atabadili nia yake kupigana na nchi za pwani na ataziteka nyingi, lakini jemadari mmoja atakomesha ufidhuli wake na kurudisha ufidhuli wake juu yake.
19 For he shall turne his face toward the fortes of his owne land: but he shall be ouerthrowen and fall, and be no more founde.
Baada ya hili atazigeukia ngome za nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena.
20 Then shall stand vp in his place in the glorie of the kingdome, one that shall raise taxes: but after fewe dayes he shall be destroyed, neither in wrath, nor in battell.
“Atakayetawala baada yake atamtuma mtoza ushuru ili kudumisha fahari ya kifalme. Hata hivyo, baada ya miaka michache ataangamizwa, lakini si katika hasira wala katika vita.
21 And in his place shall stand vp a vile person, to whom they shall not giue the honour of the kingdome: but he shall come in peaceably, and obteine the kingdome by flatteries.
“Atakayetawala baada yake atakuwa mtu wa kudharauliwa ambaye hajapewa heshima ya kifalme. Atauvamia ufalme wakati watu wake wanapojiona wako salama, naye atautwaa kwa hila.
22 And the armes shall be ouerthrowen with a flood before him, and shall be broken: and also the prince of the couenant.
Ndipo jeshi kubwa litafagiliwa mbele yake; jeshi pamoja na mkuu mmoja wa agano wataangamizwa.
23 And after the league made with him, he shall worke deceitfully: for he shall come vp, and ouercome with a small people.
Baada ya kufanya mapatano naye, atatenda kwa udanganyifu, na akitumia watu wachache tu ataingia madarakani.
24 He shall enter into the quiet and plentifull prouince, and he shall doe that which his fathers haue not done, nor his fathers fathers: he shall deuide among them the pray and the spoyle, and the substance, yea, and he shall forecast his deuises against the strong holdes, euen for a time.
Wakati majimbo yaliyo tajiri sana yanajiona salama, atayavamia, naye atafanikisha kile ambacho baba zake wala babu zake hawakuweza. Atagawa nyara, mateka na utajiri miongoni mwa wafuasi wake. Atafanya hila ya kupindua miji yenye maboma, lakini kwa muda mfupi tu.
25 Also he shall stirre vp his power and his courage against the King of the South with a great armie, and the King of the South shall be stirred vp to battell with a very great and mightie armie: but he shall not stand: for they shall forecast and practise against him.
“Pamoja na jeshi kubwa atachochea nguvu zake na ushujaa wake dhidi ya mfalme wa Kusini. Mfalme wa Kusini atafanya vita na jeshi lenye nguvu sana, lakini hataweza kusimama kwa sababu ya kwa hila zilizofanywa dhidi yake.
26 Yea, they that feede of the portion of his meate, shall destroy him: and his armie shall ouerflowe: and many shall fall, and be slaine.
Wale wanaokula kutoka kwenye ruzuku za mfalme watajaribu kumwangamiza; jeshi lake litafagiliwa mbali, nao wengi watakufa vitani.
27 And both these Kings hearts shall be to do mischiefe, and they shall talke of deceite at one table: but it shall not auaile: for yet the ende shall be at the time appointed.
Wafalme hawa wawili, mioyo yao ikiwa imekusudia mabaya, wataketi kwenye meza moja na kudanganyana wao kwa wao, lakini pasipo faida, kwa sababu bado mwisho utakuja katika wakati ulioamriwa.
28 Then shall he returne into his land with great substance: for his heart shall be against the holy couenant: so shall he doe and returne to his owne land.
Mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake na utajiri mwingi, lakini atakuwa ameukaza moyo wake kinyume na agano takatifu. Atachukua hatua dhidi ya hilo agano, kisha atarudi nchi yake.
29 At the time appointed he shall returne, and come toward the South: but the last shall not be as the first.
“Wakati ulioamriwa, atavamia tena Kusini, lakini wakati huu matokeo yake yatakuwa tofauti na yale ya wakati wa kwanza.
30 For the shippes of Chittim shall come against him: therefore he shalbe sorie and returne, and freat against the holy couenant: so shall he doe, he shall euen returne and haue intelligence with them that forsake the holy couenant.
Meli za nchi ya Kitimu zitampinga, naye atavunjika moyo. Ndipo atarudi nyuma na kutoa wazi hasira yake dhidi ya agano takatifu. Atarudi na kuonyesha fadhili kwa wale waliachao agano takatifu.
31 And armes shall stand on his part, and they shall pollute the Sanctuarie of strength, and shall take away the dayly sacrifice, and they shall set vp the abominable desolation.
“Majeshi yake yenye silaha yatainuka ili kunajisi ngome ya Hekalu, na kuondolea mbali sadaka ya kuteketezwa ya kila siku. Ndipo watalisimamisha chukizo la uharibifu lisababishalo ukiwa.
32 And such as wickedly breake ye couenant, shall he cause to sinne by flatterie: but the people that do know their God, shall preuaile and prosper.
Kwa udanganyifu atapotosha wale walionajisi agano, lakini watu wanaomjua Mungu wao watampinga kwa uthabiti.
33 And they that vnderstand among the people, shall instruct many: yet they shall fall by sword, and by flame, by captiuitie and by spoile many dayes.
“Wenye hekima watawafundisha wengi, ingawa kwa kitambo watauawa kwa upanga au kuchomwa moto, au kukamatwa au kufanywa mateka.
34 Nowe when they shall fall, they shall be holpen with a litle helpe: but many shall cleaue vnto them fainedly.
Watakapoanguka, watapokea msaada kidogo, nao wengi ambao si waaminifu wataungana nao.
35 And some of the of vnderstanding shall fall to trie them, and to purge, and to make them white, till the time be out: for there is a time appointed.
Baadhi ya wenye hekima watajikwaa, ili waweze kusafishwa, kutakaswa na kufanywa wasio na waa mpaka wakati wa mwisho, kwa maana bado litakuja kwa wakati ulioamriwa.
36 And the King shall doe what him list: he shall exalt himselfe, and magnifie himselfe against all, that is God, and shall speake marueilous things against ye God of gods, and shall prosper, till ye wrath be accomplished: for ye determination is made.
“Mfalme atafanya apendavyo. Atajikweza na kujitukuza juu ya kila mungu, naye atasema mambo ambayo hayajasikiwa dhidi ya Mungu wa miungu. Atafanikiwa hadi wakati wa ghadhabu utimie, kwa maana kile kilichokusudiwa lazima kitokee.
37 Neither shall he regard the God of his fathers, nor the desires of women, nor care for any God: for he shall magnifie himselfe aboue all.
Hataonyesha heshima kwa miungu ya baba zake au kwa yule aliyetamaniwa na wanawake, wala hatajali mungu yeyote, bali atajikweza mwenyewe juu yao wote.
38 But in his place shall he honour the god Mauzzim, and the god whom his fathers knewe not, shall he honour with golde and with siluer, and with precious stones, and pleasant things.
Badala ya kuwajali miungu, ataheshimu mungu wa ngome; mungu ambaye hakujulikana na baba zake ndiye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa vito vya thamani na zawadi za thamani kubwa.
39 Thus shall he do in the holdes of Mauzzim with a strange god whom he shall acknowledge: he shall increase his glory, and shall cause them to rule ouer many and shall deuide ye land for gaine.
Atashambulia ngome zenye nguvu mno kwa msaada wa mungu wa kigeni naye atawaheshimu sana wale watakaomkubali yeye. Atawafanya watawala juu ya watu wengi, na atagawa nchi kwa gharama.
40 And at ye end of time shall the King of the South push at him, and the king of the North shall come against him like a whirlewind with charets, and with horsemen, and with many ships, and he shall enter into ye countreis, and shall ouerflow and passe through.
“Katika wakati wa mwisho, mfalme wa Kusini atapigana naye vita, naye mfalme wa Kaskazini atamshambulia kwa magari ya vita, askari wapanda farasi, na idadi kubwa ya meli. Atavamia nchi nyingi na kuzikumba nchi hizo kama mafuriko.
41 He shall enter also into the pleasant land, and many countreis shalbe ouerthrowen: but these shall escape out of his hand, euen Edom and Moab, and the chiefe of the children of Ammon.
Pia ataivamia Nchi ya Kupendeza. Nchi nyingi zitapinduliwa, bali Edomu, Moabu na viongozi wa Amoni wataokolewa kutoka mkono wake.
42 He shall stretch foorth his hands also vpon the countreis, and ye land of Egypt shall not escape.
Atapanua mamlaka yake juu ya nchi nyingi; hata Misri haitaepuka.
43 But he shall haue power ouer the treasures of golde and of siluer, and ouer all the precious things of Egypt, and of the Lybians, and of the blacke Mores where he shall passe.
Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na utajiri wote wa Misri, pamoja na Walibia na Wakushi kwa kujisalimisha.
44 But the tidings out of the East and the North shall trouble him: therefore he shall goe foorth with great wrath to destroy and roote out many.
Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamshtua, naye ataondoka kwa ghadhabu nyingi ili kuangamiza na kuharibu kabisa wengi.
45 And he shall plant the tabernacles of his palace betweene the seas in the glorious and holy mountaine, yet he shall come to his end, and none shall helpe him.
Atasimika hema zake za ufalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa kupendeza. Hata hivyo, atafikia mwisho wake, wala hakuna yeyote atakayemsaidia.