< Colossians 4 >

1 Ye masters, doe vnto your seruants, that which is iust, and equall, knowing that ye also haue a master in heauen.
Mabwana, toeni kwa watumwa mambo yaliyo haki na ya adili. Mnajua pia kwamba mnaye Bwana mbinguni.
2 Continue in prayer, and watch in the fame with thankesgiuing,
Endeleeni kuwa thabiti katika maombi. Kaeni macho katika hilo kwa shukrani.
3 Praying also for vs, that God may open vnto vs the doore of vtterance, to speake ye mysterie of Christ: wherefore I am also in bonds,
Ombeni pamoja kwa ajili yetu pia, ili kwamba Mungu afungue mlango kwa ajili ya neno, kunena siri ya ukweli ya Kristo. Kwa sababu ya hili nimefungwa minyororo.
4 That I may vtter it, as it becommeth mee to speake.
Na ombeni kwamba niweze kuliweka wazi, kama inavyonipasa kusema.
5 Walke wisely towarde them that are without, and redeeme the season.
Enenda kwa hekima kwa wale walioko nje, na muukomboe wakati.
6 Let your speach be gracious alwayes, and powdred with salt, that ye may know how to answere euery man.
Maneno yenu na yawe na neema wakati wote, na yakolee chumvi majira yote, ili kwamba mweze kujua jinsi inavyowapasa kumjibu kila mtu.
7 Tychicus our beloued brother and faithfull minister, and fellow seruant in the Lord, shall declare vnto you my whole state:
Kwa mambo yanayonihusu mimi, Tikiko atayafanya yajulikane kwenu. Yeye ni ndugu mpendwa, mtumishi mwaminifu, na mtumwa mwenzetu katika Bwana.
8 Whom I haue sent vnto you for the same purpose that he might know your state, and might comfort your hearts,
Namtuma kwenu kwa ajili ya hili, kwamba mweze kujua mambo kuhusu sisi na pia kwamba aweze kuwatia moyo.
9 With Onesimus a faithfull and a beloued brother, who is one of you. They shall shew you of all things here.
Namtuma pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpendwa mwaminifu, na mmoja wenu. Watawaambia kila kitu kilichotokea hapa.
10 Aristarchus my prison fellow saluteth you, and Marcus, Barnabas cousin (touching whom ye receiued commandements. If he come vnto you, receiue him)
Aristarko, mfungwa mwenzangu, anawasalimu, pia na Marko binamu yake na Barnaba mliyepokea utaratibu kutoka kwake, “kama akija kwenu, mpokeeni,”
11 And Iesus which is called Iustus, which are of the circumcision. These onely are my worke fellowes vnto the kingdome of God, which haue bene vnto my consolation.
Na pia Yesu aitwaye Yusto. Hawa peke yao wa tohara ni watendakazi wenzangu kwa jili ya ufalme wa Mungu. Wamekuwa ni faraja kwangu.
12 Epaphras the seruant of Christ, which is one of you, saluteth you, and alwayes striueth for you in prayers, that ye may stand perfect, and full in all the will of God.
Epafra anawasalimu. Yeye ni mmoja wenu na mtumwa wa Kristo Yesu. Yeye hufanya bidii katika maombi kwa ajili, ili kwamba mweze kusimama kwa ukamilifu na kuhakishwa kikamilifu katika mapenzi yote ya Mungu.
13 For I beare him record, that he hath a great zeale for you, and for them of Laodicea, and them of Hierapolis.
Kwa kuwa ninamshuhudia, kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, kwa hao walioko Laodekia, na kwa hao walioko Hierapoli.
14 Luke the beloued physician greeteth you, and Demas.
Luka yule tabibu mpendwa, na Dema wanawasalimu.
15 Salute the brethren which are of Laodicea, and Nymphas, and the Church which is in his house.
Wasalimu ndugu zangu walioko Laodekia, na Nimfa, na kanisa lile lililoko nyumbani kwake.
16 And when this Epistle is read of you, cause that it be read in the Church of the Laodiceans also, and that ye likewise reade the Epistle written from Laodicea.
Barua hii itakapokuwa imesomwa miongoni mwenu, isomwe pia kwa kanisa la walaodekia, nanyi pia hakikisheni mnaisoma ile barua kutoka Laodekia.
17 And say to Archippus, Take heede to the ministerie, that thou hast receiued in the Lord, that thou fulfill it.
Sema kwa Arkipo, ''Angalia ile huduma ambayo umeipokea katika Bwana, kwamba unapaswa kuitimiza.”
18 The salutation by the hand of me Paul. Remember my bands. Grace be with you, Amen. ‘Written from Rome to the Colossians, and sent by Tychicus, and Onesimus.’
Salamu hii ni kwa mkono wangu mwenyewe - Paulo. Ikuumbukeni minyororo yangu. Neema na iwe nanyi.

< Colossians 4 >