< Colossians 4 >

1 Ye masters, doe vnto your seruants, that which is iust, and equall, knowing that ye also haue a master in heauen.
Ninyi mabwana, watendeeni watumwa wenu yaliyo haki na yanayostahili, mkitambua ya kwamba ninyi pia mnaye Bwana mbinguni.
2 Continue in prayer, and watch in the fame with thankesgiuing,
Dumuni sana katika maombi, mkikesha katika hayo pamoja na kushukuru.
3 Praying also for vs, that God may open vnto vs the doore of vtterance, to speake ye mysterie of Christ: wherefore I am also in bonds,
Pia tuombeeni na sisi ili Mungu atufungulie mlango wa kunena, ili tupate kuitangaza siri ya Kristo, ambayo kwa ajili yake pia mimi nimefungwa.
4 That I may vtter it, as it becommeth mee to speake.
Ombeni ili nipate kuitangaza Injili kwa udhahiri kama ipasavyo kunena.
5 Walke wisely towarde them that are without, and redeeme the season.
Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati.
6 Let your speach be gracious alwayes, and powdred with salt, that ye may know how to answere euery man.
Maneno yenu yawe yamejaa neema siku zote, yanayofaa, ili mjue jinsi iwapasavyo na inavyofaa kumjibu kila mtu.
7 Tychicus our beloued brother and faithfull minister, and fellow seruant in the Lord, shall declare vnto you my whole state:
Tikiko atawaambia habari zangu zote. Yeye ni ndugu mpendwa, mtendakazi mwaminifu na mtumishi mwenzangu katika Bwana.
8 Whom I haue sent vnto you for the same purpose that he might know your state, and might comfort your hearts,
Nimemtuma kwenu kwa madhumuni haya ili mpate kufahamu hali yetu, na pia awatie moyo.
9 With Onesimus a faithfull and a beloued brother, who is one of you. They shall shew you of all things here.
Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpendwa na mwaminifu, ambaye ni mmoja wenu. Watawaambia mambo yote yanayotendeka hapa kwetu.
10 Aristarchus my prison fellow saluteth you, and Marcus, Barnabas cousin (touching whom ye receiued commandements. If he come vnto you, receiue him)
Aristarko aliye mfungwa pamoja nami anawasalimu, vivyo hivyo Marko, binamu yake Barnaba. (Mmeshapata maagizo yanayomhusu; akija kwenu, mpokeeni.)
11 And Iesus which is called Iustus, which are of the circumcision. These onely are my worke fellowes vnto the kingdome of God, which haue bene vnto my consolation.
Yesu, yeye aitwaye Yusto, pia anawasalimu. Hawa peke yao ndio Wayahudi miongoni mwa watendakazi wenzangu kwa ajili ya Ufalme wa Mungu, nao wamekuwa faraja kwangu.
12 Epaphras the seruant of Christ, which is one of you, saluteth you, and alwayes striueth for you in prayers, that ye may stand perfect, and full in all the will of God.
Epafra, ambaye ni mmoja wenu na mtumishi wa Kristo Yesu, anawasalimu. Yeye siku zote anawaombea kwa bidii kwamba msimame imara katika mapenzi yote ya Mungu, mkiwa wakamilifu na thabiti.
13 For I beare him record, that he hath a great zeale for you, and for them of Laodicea, and them of Hierapolis.
Ninashuhudia kumhusu kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, na kwa ajili ya ndugu wa Laodikia na wale wa Hierapoli.
14 Luke the beloued physician greeteth you, and Demas.
Rafiki yetu mpenzi Luka yule tabibu, pamoja na Dema, wanawasalimu.
15 Salute the brethren which are of Laodicea, and Nymphas, and the Church which is in his house.
Wasalimuni ndugu wote wa Laodikia, na pia Nimfa, pamoja na kanisa linalokutana katika nyumba yake.
16 And when this Epistle is read of you, cause that it be read in the Church of the Laodiceans also, and that ye likewise reade the Epistle written from Laodicea.
Baada ya barua hii kusomwa kwenu, hakikisheni kwamba inasomwa pia katika kanisa la Walaodikia. Nanyi pia msome barua inayotoka Laodikia.
17 And say to Archippus, Take heede to the ministerie, that thou hast receiued in the Lord, that thou fulfill it.
Mwambieni Arkipo hivi: “Hakikisha kuwa unakamilisha ile huduma uliyopokea katika Bwana.”
18 The salutation by the hand of me Paul. Remember my bands. Grace be with you, Amen. ‘Written from Rome to the Colossians, and sent by Tychicus, and Onesimus.’
Mimi, Paulo, naandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Kumbukeni minyororo yangu. Neema iwe nanyi. Amen.

< Colossians 4 >