< Amos 4 >

1 Heare this worde, ye kine of Bashan that are in the mountaine of Samaria, which oppresse the poore, and destroy the needie, and they say to their masters, Bring, and let vs drinke.
Lisikilizeni neno hili, ninyi ng'ombe wa Bashani, ninyi mliomo katika mlima wa Samaria, ninyi mnaowakandamiza maskini, ninyi mnaowaponda wahitaji, ninyi muwaambiao waume zenu, “Tuleteeni vinywaji.”
2 The Lord God hath sworne by his holines, that loe, the dayes shall come vpon you, that hee wil take you away with thornes, and your posteritie with fish hookes.
Bwana Yahwe ameapa kwa utukufu wake, “Tazama, siku zitakuja kwenu wakati watakapowaondoa kwa ndoana, wa mwisho wenu na ndoana za kuvulia samaki.
3 And ye shall goe out at the breaches euery kow forward: and ye shall cast your selues out of the palace, saith the Lord.
Mtatoka kupitia mahali palipo bomolewa kwenye kuta za mji, kila mmoja wenu kwenda moja kwa moja kupitia hapo, na mtajitupa mbele ya Harmoni -hivi ndivyo asemavyo Yahwe.”
4 Come to Beth-el, and transgresse: to Gilgal, and multiplie transgression, and bring your sacrifices in the morning, and your tithes after three yeres.
“Nendeni Betheli na uovu, hata Gilgali mkaongeza dhambi, leteni dhabihu zenu kila asubuhi, zaka zenu kila baada ya siku tatu.
5 And offer a thankesgiuing of leauen, publish and proclaime the free offrings: for this liketh you, O ye children of Israel, saith the Lord God.
Toeni dhabihu za shukurani pamoja na mkate; tangazeni sadaka za hiari; watangazieni, kwa kuwa hii ndiyo iwapendezayo, ninyi watu wa Israeli -hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe.
6 And therefore haue I giuen you cleannes of teeth in all your cities, and scarcenesse of bread in all your places, yet haue ye not returned vnto me, saith the Lord.
Nawapatia usafi wa meno katika miji yenu na na kupungukiwa na mkate katika sehemu zenu zote. Bado hamkurudi kwangu -hivi ndivyo Yahwe asemavyo.
7 And also I haue withholden the raine from you, when there were yet three moneths to the haruest, and I caused it to raine vpon one citie, and haue not caused it to raine vpon another citie: one piece was rained vpon, and the piece whereupon it rained not, withered.
Pia nimeizuia mvua kutoka kwenu wakati bado kulikuwa na miezi mitatu kwa mavuno. Nikaifanya inyeshe juu ya mji, na kuifanya isinyeshe katika mji mwingine. Kipande kimoja cha nchi ilinyesha, lakini kipande kingine cha nchi ambapo haikunyesha palikuwa pakavu.
8 So two or three cities wandred vnto one citie to drinke water, but they were not satisfied: yet haue ye not returned vnto me, saith the Lord.
Walizunguka miji miwili au mitatu kwenda mji mwingine kunywa maji, lakini hawakutosheka. Bado hawakunirudia mimi -asema Yahwe.
9 I haue smitten you with blasting, and mildewe: your great gardens and your vineyardes, and your figtrees, and your oliue trees did the palmer worme deuoure: yet haue ye not returned vnto me, saith the Lord.
Nimewapiga kwa maradhi yanayosababisha kuvu. Wingi wa bustani, mashamba yenu ya zabibu, mitini yenu, na mizaituni-kuteketeza yote. Bado hamkunirudia hivi ndivyo Yahwe asemavyo.
10 Pestilence haue I sent among you, after the maner of Egypt: your yong men haue I slaine with the sworde, and haue taken away your horses: and I haue made the stinke of your tentes to come vp euen into your nostrels: yet haue yee not returned vnto me, saith the Lord.
Nimetuma tauni kwenu kama ya Misri. Nimewaua watoto wenu kwa upanga, kubeba farasi zenu, na kuufanya uvundo wa kambi zenu na kuingiza kwenye pua zenu. Bado hamkunirudia mimi -hivi ndivyo asemavyo Yahwe.
11 I haue ouerthrowe you, as God ouerthrew Sodom and Gomorah: and ye were as a firebrand pluckt out of the burning: yet haue ye not returned vnto me, saith the Lord.
Nimeiangamiza miji miongoni mwenu, kama wakati Mungu alipoiangamiza Sodoma na Gomora. Mlikuwa kama kijinga kilichonyakuliwa kutoka kwenye moto. Bado hamkunirudia - asema Yahwe.
12 Therefore, thus wil I do vnto thee, O Israel: and because I wil doe this vnto thee, prepare to meete thy God, O Israel.
Kwa hiyo nitafanya jambo baya kwako, Israeli; na kwa sababu nitafanya jambo baya kwako, jiandae kukutana na Mungu, Israeli!
13 For lo, he that formeth the mountaines, and createth the winde, and declareth vnto man what is his thought: which maketh the morning darkenesse, and walketh vpon the hie places of the earth, the Lord God of hostes is his Name.
Kwa kuwa, tazama, yeye atangenezaye milima pia ndiye aumbaye upepo, humfunulia mawazo yake mwanadamu, hufanya asubuhi kuwa giza, na kupakanyaga mahala pa juu ya dunia. Yahwe, Mungu wa majeshi, ndilo jina lake.”

< Amos 4 >