< Acts 3 >
1 Nowe Peter and Iohn went vp together into the Temple, at the ninth houre of prayer.
Sasa Peter na Yohana walikuwa wanaelekea katika hekalu wakati wa maombi, saa tisa.
2 And a certaine man which was a creeple from his mothers wombe, was caried, whom they layde dayly at the gate of the Temple called Beautifull, to aske almes of them that entred into ye Temple.
Mtu fulani, kiwete tangu kuzaliwa, alikuwa akibebwa kila siku na alikuwa akilazwa katika mlango wa hekalu uitwao mzuri, ili aweze kuomba sadaka kutoka kwa watu waliokuwa wakielekea hekaluni.
3 Who seeing Peter and Iohn, that they would enter into the Temple, desired to receiue an almes.
Alipowaona Petro na Yohana wanakaribia kuingia hekaluni, aliomba sadaka.
4 And Peter earnestly beholding him with Iohn, said, Looke on vs.
Petro, akimkazia macho, pamoja na Yohana, alisema,”tutazame sisi.”
5 And hee gaue heede vnto them, trusting to receiue some thing of them.
Kiwete akawatazama, akitazamia kupokea kitu fulani kutoka kwao.
6 Then said Peter, Siluer and gold haue I none, but such as I haue, that giue I thee: In the Name of Iesus Christ of Nazareth, rise vp and walke.
Lakini Petro akasema, “fedha na dhahabu mimi sina, lakini kile nilichonacho nitatoa kwako. Katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth, tembea.”
7 And hee tooke him by the right hand, and lift him vp, and immediately his feete and ankle bones receiued strength.
Petro akamchukua kwa mkono wake wa kulia, na akamwinua juu: mara moja miguu yake na vifundo vya mifupa yake vikapata nguvu.
8 And he leaped vp, stoode, and walked, and entred with them into the Temple, walking and leaping, and praysing God.
Akiruka juu, mtu kiwete alisimama na akaanza kutembea; akaingia hekaluni pamoja na Petro na Yohana, akitembea, akiruka, na kumsifu Mungu.
9 And all the people sawe him walke, and praysing God.
Watu wote walimwona akitembea na akimsifu Mungu.
10 And they knewe him, that it was he which sate for the almes at the Beautifull gate of the Temple: and they were amased, and sore astonied at that, which was come vnto him.
Wakatambua kwamba alikuwa ni yule mtu ambaye alikuwa akikaa akiomba sadaka kwenye mlango mzuri wa hekalu; walijawa na mshangao na kustaajabu kwa sababu ya kile kilichotokea kwake.
11 And as the creeple which was healed, held Peter and Iohn, all the people ranne amased vnto them in the porch which is called Salomons.
Namna alivyokuwa amewashikilia Petro na Yohana, watu wote kwa pamoja wakakimbilia kwenye ukumbi uitwao wa Sulemani, wakishangaa sana.
12 So when Peter saw it, he answered vnto the people, Ye me of Israel, why marueile ye at this? or why looke ye so stedfastly on vs, as though by our owne power or godlines, we had made this man go?
Petro alipoliona hili, yeye akawajibu watu, “Enyi watu wa Israel, kwa nini mnashangaa? Kwa nini mnayaelekeza macho yenu kwetu, kama kwamba tumemfanya huyu atembee kwa nguvu zetu wenyewe au uchaji wetu?”
13 The God of Abraham, and Isaac, and Iacob, the God of our fathers hath glorified his Sonne Iesus, whom ye betrayed, and denied in the presence of Pilate, when he had iudged him to be deliuered.
Mungu wa Ibrahimu, na wa Isaka, na wa Yakobo, Mungu wa Baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu. Huyu ndiye ambaye ninyi mlimkabidhi na kumkataa mbele ya uso wa Pilato, japo yeye alikuwa ameamua kumwachia huru.
14 But ye denied the Holy one and the Iust, and desired a murtherer to be giuen you,
Mlimkataa Mtakatifu na Mwenye Haki, na badala yake mkataka muuaji aachwe huru.
15 And killed the Lord of life, whome God hath raised from the dead, whereof we are witnesses.
Ninyi mlimuua Mfalme wa uzima, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu - Sisi ni mashahidi wa hili.
16 And his Name hath made this man sound, whom ye see, and know, through faith in his Name: and the faith which is by him, hath giuen to him this perfite health of his whole body in the presence of you all.
Sasa, kwa imani katika jina lake, mtu huyu ambaye mnamwona na kujua, alifanywa kuwa na nguvu. Imani ambayo inapitia kwa Yesu imempa yeye afya hii kamilifu, mbele yenu ninyi nyote.
17 And now brethren, I know that through ignorance ye did it, as did also your gouernours.
Sasa, Ndugu, najua kwamba mlitenda katika ujinga, ndivyo pia walivyofanya viongozi wenu.
18 But those thinges which God before had shewed by the mouth of all his Prophets, that Christ should suffer, he hath thus fulfilled.
Lakini mambo ambayo Mungu aliwaambia mapema kwa vinywa vya manabii wote, kwamba huyu Kristo atateseka, sasa ameyatimiza.
19 Amend your liues therefore, and turne, that your sinnes may be put away, whe the time of refreshing shall come from the presence of the Lord.
Kwa hiyo, tubuni na mgeuke, ili kwamba dhambi zenu ziweze kuondolewa kabisa, kusudi zije nyakati za kuburudika kutokana na uwepo wa Bwana;
20 And he shall sende Iesus Christ, which before was preached vnto you,
na kwamba aweze kumtuma Kristo ambaye ameshateuliwa kwa ajili yenu, Yesu.
21 Whome the heauen must containe vntill the time that all thinges be restored, which God had spoken by the mouth of all his holy Prophets since the world began. (aiōn )
Yeye ndiye ambaye lazima mbingu zimpokee mpaka wakati wa kurejeshwa kwa vitu vyote, ambavyo Mungu alizungumzia zamani za kale kwa vinywa vya manabii watakatifu. (aiōn )
22 For Moses said vnto the Fathers, The Lord your God shall raise vp vnto you a Prophet, euen of your brethren, like vnto me: ye shall heare him in all things, whatsoeuer he shall say vnto you.
Hakika Musa alisema, 'Bwana Mungu atainua nabii kama mimi kutoka katika ndugu zenu. Mtamsikiliza kila kitu ambacho atawaambia ninyi.
23 For it shalbe that euery person which shall not heare that Prophet, shall be destroyed out of the people.
Itatokea kwamba kila mtu ambaye hasikilizi kwa nabii huyo ataangamizwa kabisa atoke kati ya watu.'
24 Also all the Prophets from Samuel, and thencefoorth as many as haue spoken, haue likewise foretolde of these dayes.
Ndiyo, na manabii wote tokea Samweli na wale waliofuata baada yake, walizungumza na walitangaza siku hizi.
25 Ye are the children of the Prophets, and of the couenant, which God hath made vnto our fathers, saying to Abraham, Euen in thy seede shall all the kindreds of the earth be blessed.
Ninyi ni wana wa manabii na wa agano ambalo Mungu alilifanya pamoja na mababu, kama alivyosema kwa Abrahamu, 'Katika mbegu yako familia zote za dunia zitabarikiwa.'
26 First vnto you hath God raysed vp his Sonne Iesus, and him hee hath sent to blesse you, in turning euery one of you from your iniquities.
Baada ya Mungu kumwinua mtumishi wake, alimtuma kwenu kwanza, ili awabariki ninyi kwa kugeuka kutoka katika uovu wenu.”