< Acts 27 >

1 Now when it was concluded, that we should sayle into Italie, they deliuered both Paul, and certaine other prisoners vnto a Centurion named Iulius, of the band of Augustus.
Ilipoamuliwa kwamba tunatakiwa tusafiri kwa maji kwenda Italia, walimkabidhi Paulo na wafungwa wengine kwa afisa mmoja wa jeshi la Kiroma aliyeitwa Julio, wa Kikosi cha Agustani.
2 And we entred into a ship of Adramyttium purposing to saile by the coastes of Asia, and launched foorth, and had Aristarchus of Macedonia, a Thessalonian, with vs.
Tukapanda meli kutoka Adramitamu, ambayo ilikuwa isafiri kandokando ya pwani ya Asia. Hivyo tukaingia baharini. Aristaka kutoka Thesolanike ya Makedonia akaenda pamoja nasi.
3 And the next day we arriued at Sidon: and Iulius courteously entreated Paul, and gaue him libertie to go vnto his friends, that they might refresh him.
Siku iliyofuata tukatua nanga katika mji wa Sidoni, ambapo Julio alimtendea Paulo kwa ukarimu na akamruhusu kwenda kwa rafiki zake kupokea ukarimu wao.
4 And from thence we launched, and sayled hard by Cyprus, because ye windes were contrarie.
Kutoka hapo tukaenda baharini tukasafiri kuzunguka kisiwa cha Kipro ambacho kilikuwa kimeukinga upepo, kwa sababu upepo ulikuwa ukitukabili.
5 Then sayled we ouer the sea by Cilicia, and Pamphilia, and came to Myra, a citie in Lycia.
Baada ya kuwa tumesafiri katika maji yaliyo karibu na Kilikia na Pamfilia, tukaja Mira, mji wa Lisia.
6 And there the Centurion found a ship of Alexandria, sayling into Italie, and put vs therein.
Pale yule afisa wa jeshi la Kiroma, akaikuta meli kutoka Alexandria ambayo ilikuwa isafiri kuelekea Italia. Akatupandisha ndani yake.
7 And when we had sayled slowly many dayes, and scarce were come against Gnidum, because the winde suffered vs not, we sailed hard by Candie, neere to Salmone,
Baada ya kuwa tumesafiri polepole kwa siku nyingi na hatimaye tukawa tumefika kwa taabu karibu na Kinidas, upepo haukuturuhusu tena kuelekea njia hiyo, hivyo tukasafiri kandokando ya kivuli cha Krete tukiukinga upepo, mkabala na Salmone.
8 And with much adoe sayled beyond it, and came vnto a certaine place called the Faire hauens, neere vnto the which was the citie Lasea.
Tukasafiri kandokando ya pwani kwa ugumu, mpaka tukafika mahali palipoitwa Fari Haveni ambayo iko karibu na mji wa Lasi.
9 So when much time was spent, and sayling was now ieopardous, because also the Fast was nowe passed, Paul exhorted them,
Tulikuwa tumechukua muda mwingi sana, na muda wa mfungo wa Kiyahudi ulikuwa umepita pia, na sasa ilikuwa ni hatari kuendelea kusafiri. Hivyo Paulo akatuonya,
10 And sayde vnto them, Syrs, I see that this voiage will be with hurt and much damage, not of the lading and ship onely, but also of our liues.
na kusema, “Wanaume, naona safari ambayo tunataka tuichukue itakuwa na madhara na hasara nyingi, siyo tu ya mizigo na meli, lakini pia ya maisha yetu.”
11 Neuertheles the Centurion beleeued rather the gouernour and the master of the ship, then those things which were spoken of Paul.
Lakini afisa wa jeshi la Kiroma akamsikiliza zaidi bwana wake na mmiliki wa meli, kuliko mambo yale ambayo yalizungumzwa na Paulo.
12 And because the hauen was not commodious to winter in, many tooke counsell to depart thence, if by any meanes they might attaine to Phenice, there to winter, which is an hauen of Candie, and lyeth toward the Southwest and by West, and Northwest and by West.
Kwa sababu bandari haikuwa sehemu rahisi kukaa wakati wa baridi, mabaharia wengi wakashauri tusafiri kutoka pale, ili kwa namna yoyote tukiweza kuufikia mji wa Foinike, tukae pale wakati wa baridi. Foinike ni bandari huko Krete, na inatazama kaskazini mashariki na kusini mashariki.
13 And when the Southerne winde blew softly, they supposing to atteine their purpose, loosed neerer, and sailed by Candie.
Upepo wa kusini ulipoanza kuvuma polepole, mabaharia wakafikiri wamepata kile ambacho walikuwa wanakihitaji. Wakang'oa nanga na kusafiri kandokando ya Krete karibu na pwani.
14 But anon after, there arose by it a stormy winde called Euroclydon.
Lakini baada ya muda mfupi upepo mkali, ulioitwa Wa kaskazini mashariki, ukaanza kutupiga kutoka ng'ambo ya kisiwa.
15 And when the ship was caught, and could not resist the winde, we let her goe, and were caried away.
Wakati meli ilipolemewa na kushindwa kuukabili upepo, tukakubaliana na hali hiyo, tukasafirishwa nao.
16 And we ran vnder a litle Yle named Clauda, and had much a doe to get the boat.
Tukakimbia kupitia ule upande uliokuwa unaukinga upepo wa kisiwa kiitwacho Kauda; na kwa taabu sana tulifanikiwa kuuokoa mtumbwi.
17 Which they tooke vp and vsed all helpe, vndergirding the ship, fearing least they should haue fallen into Syrtes, and they strake saile, and so were caried.
Baada ya kuwa wameivuta, walitumia kamba kuifunga meli. Waliogopa kwamba tungeweza kwenda kwenye eneo la mchanga mwingi la Syiti, hivyo wakashusha nanga na waliendeshwa kandokando.
18 The next day when we were tossed with an exceeding tempest, they lightened the ship.
Tulipigwa kwa nguvu sana na dhoruba, hivyo siku iliyofuata mabaharia wakaanza kutupa mizigo kutoka melini.
19 And the third day we cast out with our owne hands the tackling of the ship.
Siku ya tatu, mabaharia wakaanza kuyatoa maji kwa mikono yao wenyewe.
20 And when neither sunne nor starres in many dayes appeared, and no small tempest lay vpon vs, all hope that we should be saued, was then taken away.
Wakati ambapo jua na nyota hazikutuangazia kwa siku nyingi, bado dhoruba kubwa ilitupiga, na matumaini kwamba tungeokolewa yalitoweka.
21 But after long abstinece, Paul stood forth in the mids of them, and said, Syrs, ye should haue hearkened to me, and not haue loosed from Candie: so should ye haue gained this hurt and losse.
Baada ya kuwa wameenda muda mrefu bila chakula, hapo Paulo akasimama katikati ya mabaharia akasema, “Wanaume, mlipaswa mnisikilize, na tusingengo'a nanga kutoka Krete, ili kupata haya madhara na hasara.
22 But now I exhort you to be of good courage: for there shalbe no losse of any mans life among you, saue of the ship onely.
Na sasa nawafariji mjitie moyo, kwa sababu hakutakuwa upotevu maisha kati yenu, isipokuwa hasara ya meli tu.
23 For there stood by me this night the Angel of God, whose I am, and whome I serue,
Kwa sababu usiku uliopita malaika wa Mungu, ambaye huyo Mungu mimi ni wake, na ambaye ninamwabudu pia - malaika wake alisimama pembeni mwangu
24 Saying, Feare not, Paul: for thou must be brought before Cesar: and lo, God hath giuen vnto thee freely all that sayle with thee.
na kusema, “Usiogope Paulo. Lazima usimame mbele ya Kaisari, na tazama, Mungu katika wema wake amekupa hawa wote ambao wanasafiri pamoja nawe.
25 Wherefore, sirs, be of good courage: for I beleeue God, that it shall be so as it hath bene tolde me.
Hivyo, wanaume, jipeni moyo, kwa sababu namwamini Mungu, kwamba itakuwa kama nilivyoambiwa.
26 Howbeit, we must be cast into a certaine Iland.
Lakini lazima tuumie kwa kupigwa katika baadhi ya visiwa.”
27 And when ye fourteenth night was come, as we were caried to and from in the Adriaticall sea about midnight, the shipmen deemed that some countrey approched vnto them,
Ulipofika usiku wa kumi na nne, tulipokuwa tukiendeshwa huko na huko kwenye bahari ya Adratik, kama usiku wa manane hivi, mabaharia walifikiri kwamba wamekaribia nchi kavu.
28 And sounded, and found it twentie fathoms: and when they had gone a litle further, they sounded againe, and found fifteene fathoms.
Walitumia milio kupima kina cha maji na wakapata mita thelathini na sita, baada ya muda mfupi wakapima tena wakapata mita ishirini na saba.
29 Then fearing least they should haue fallen into some rough places, they cast foure ancres out of the sterne, and wished that the day were come.
Waliogopa kwanza tunaweza kugonga miamba, hivyo wakashusha nanga nne kutoka katika sehemu ya kuwekea nanga na wakaomba kwamba asubuhi ingekuja mapema.
30 Nowe as the mariners were about to flee out of the ship, and had let downe the boat into the sea vnder a colour as though they would haue cast ankers out of the foreship,
Wale mabaharia walikuwa wanatafuta namna ya kuitelekeza ile meli na walizishusha majini boti ndogo ndogo za kuokolea maisha, na wakajifanya kwamba wanatupa nanga kutoka sehemu ya mbele ya boti.
31 Paul sayde vnto the Centurion and the souldiers, Except these abide in the ship, ye can not be safe.
Lakini Paulo akamwambia yule askari wa jeshi la Kiroma na wale askari, “Hamuwezi kuokoka isipokuwa hawa watu wanabaki kwenye meli”.
32 Then the souldiers cut off the ropes of the boat, and let it fall away.
Kisha wale askari wakakata kamba za ile boti na ikaachwa ichukuliwe na maji.
33 And when it began to be day, Paul exhorted them all to take meate, saying, This is the fourteenth day that ye haue taried, and continued fasting, receiuing nothing:
Wakati mwanga wa asubuhi ulipokuwa unajitokeza, Paulo akawasihi wote angalau wale kidogo. Akasema, “Hii ni siku ya kumi na nne mnasuburi bila kula, hamjala kitu.
34 Wherefore I exhort you to take meate: for this is for your safegarde: for there shall not an heare fall from the head of any of you.
Hivyo nawasihi mchukue chakula kidogo, kwa sababu hii ni kwa ajili ya kuishi kwenu; na hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
35 And when he had thus spoken, hee tooke bread and gaue thankes to God, in presence of them all, and brake it, and began to eate.
Alipokwisha kusema hayo, akachukua mkate akamshukuru Mungu mbele ya macho ya kila mtu. Kisha akaumega mkate akaanza kula.
36 Then were they all of good courage, and they also tooke meate.
Kisha wote wakatiwa moyo na wao wakachukua chakula.
37 Nowe we were in the ship in all two hundreth three score and sixteene soules.
Tulikuwa watu 276 ndani ya meli.
38 And whe they had eaten ynough, they lightened the ship, and cast out the wheat into the sea.
Walipokwisha kula vya kutosha, waliifanya meli nyepesi kwa kutupa ngano ndani ya bahari.
39 And when it was day, they knewe not the countrey, but they spied a certaine creeke with a banke, into the which they were minded (if it were possible) to thrust in the ship.
Ilipokuwa mchana, hawakuitambua nchi kavu, lakini wakaona sehemu ya nchi kavu iliyoingia majini iliyokuwa na mchanga mwingi. wakajadiliana kama wanaweza kuiendesha meli kuelekea hapo.
40 So when they had taken vp the ankers, they committed the ship vnto the sea, and loosed the rudder bonds, and hoised vp the maine saile to the winde, and drewe to the shore.
Hivyo wakazilegeza nanga wakaziacha baharini. Katika muda huo huo wakazilegeza kamba za tanga na wakaiinua sehemu ya mbele kuelekea kwenye upepo, hivyo wakaelekea kwenye hiyo sehemu ya mchanga mwingi.
41 And when they fell into a place, where two seas met, they thrust in the ship: and the forepart stucke fast, and could not be moued, but the hinderpart was broken with the violence of the waues.
Lakini wakaja mahali ambapo mikondo miwili ya maji inakutana, na meli ikaelekea mchangani. Na ile sehemu ya mbele ya meli ikakwama pale na haikuweza kutoka, lakini sehemu ya mbele ya meli ikaanza kuvunjika kwa sababu ya ukali wa mawimbi.
42 Then the souldiers counsell was to kill the prisoners, least any of them, when he had swomme out, should flee away.
Mpango wa wale askari ulikuwa ni kuwaua wafungwa, ili kwamba hakuna ambaye angeogelea na kutoroka.
43 But the Centurion willing to saue Paul, stayed them from this counsell, and commanded that they that coulde swimme, shoulde cast them selues first into the sea, and goe out to land:
Lakini yule askari wa jeshi la Kiroma alitaka kumwokoa Paulo, hivyo akausimamisha mpango wao; na akawaamuru wale ambao wanaweza kuogelea, waruke kutoka melini kwanza na waende nchi kavu.
44 And the other, some on boardes, and some on certaine pieces of the ship: and so it came to passe that they came all safe to land.
Kisha wanaume wengine watafuata, wengine juu ya vipande vya mbao na wengine juu ya vitu vingine kutoka kwenye meli. Kwa njia hii ikatokea kwamba wote tutafika salama nchi kavu.

< Acts 27 >