< Acts 20 >

1 Nowe after the tumult was appeased, Paul called the disciples vnto him, and embraced them, and departed to goe into Macedonia.
Baada ya ghasia kumalizika, Paulo aliwaita wanafunzi na kuwatia moyo. Kisha kuwaaga na akaondoka kwenda Makedonia.
2 And when hee had gone through those parts, and had exhorted them with many words, he came into Grecia.
Naye akiishakupita mikoa hiyo na alikuwa akiwatia moyo waamuni, akaingia Uyunani.
3 And hauing taried there three moneths, because the Iewes layde waite for him, as hee was about to saile into Syria, hee purposed to returne through Macedonia.
Baada ya yeye kuwa pale kwa muda wa miezi mitatu, njama ziliundwa dhidi yake na Wayahudi alipokuwa akikaribia kusafiri kwa njia ya bahari kuelekea Shamu, hivyo aliazimu kurudi kupitia Makedonia.
4 And there accompanied him into Asia, Sopater of Berea, and of them of Thessalonica, Aristarchus, and Secundus, and Gaius of Derbe, and Timotheus, and of them of Asia, Tychicus, and Trophimus.
Walioandamana naye hadi Asia walikuwa Sopatro, mwana wa Pirho kutoka Berea; Aristariko na Sekundo, wote kutoka waamini wa Wathesalonike; Gayo wa Derbe; Timotheo; Tikiko na Trofimo kutoka Asia.
5 These went before, and taried vs at Troas.
Lakini watu hawa wamekwisha tangulia na walikuwa wanatungojea kule Troa.
6 And we sailed forth from Philippi, after the dayes of vnleauened bread, and came vnto them to Troas in fiue dayes, where we abode seuen dayes.
kwa njia ya Bahari kutoka Filipi baada ya siku za mikate isiyotiwa chachu, na katika siku tano tukawafikia huko Troa. Tulikaa huko kwa siku saba.
7 And the first day of the weeke, the disciples being come together to breake bread, Paul preached vnto them, ready to depart on the morrow, and continued the preaching vnto midnight.
Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekusanyika pamoja ili kuumega mkate, Paulo alizungumza na Waamini. Alikuwa akipanga kuondoka kesho yake, hivyo akaendelea kuongea hadi usiku wa manane.
8 And there were many lightes in an vpper chamber, where they were gathered together.
Kulikuwa na taa nyingi katika chumba cha juu ambapo tulikuwa tumekusanyika pamoja.
9 And there sate in a windowe a certaine yong man, named Eutychus, fallen into a dead sleepe: and as Paul was long preaching, hee ouercome with sleepe, fell downe from the thirde loft, and was taken vp dead.
Katika dirisha alikuwa amekaa kijana mmoja jina lake Utiko, ambaye alielemewa na usingizi mzito. Hata Paulo alipokuwa akihutubu kwa muda mrefu, kijana huyu, akiwa amelala, akaanguka chini kutoka ghorofa ya tatu na aliokotwa akiwa amekufa.
10 But Paul went downe, and layde himselfe vpon him, and embraced him, saying, Trouble not your selues: for his life is in him.
Lakini Paulo alishuka chini, alijinyoosha yeye mwenyewe juu yake, akamkumbatia. Kisha akasema, “Msikate tamaa, kwa kuwa yu hai.”
11 Then when Paul was come vp againe, and had broken bread, and eaten, hauing spoken a long while till the dawning of the day, hee so departed.
Kisha akapanda tena ghorofani na akaumega mkate, akala. Baada ya kuzungumza nao kwa muda mrefu hadi alfajiri, akaondoka.
12 And they brought the boye aliue, and they were not a litle comforted.
Wakamleta yule kijana akiwa hai wakafarijika sana.
13 Then we went before to shippe, and sailed vnto the citie Assos, that wee might receiue Paul there: for so had hee appointed, and would himselfe goe afoote.
Sisi wenyewe tulitangulia mbele ya Paul kwa meli na tukaelekea Aso, ambapo sisi tulipanga kumchukua Paul huko. Hiki ndicho yeye mwenyewe alitaka kufanya, kwa sababu alipanga kwenda kupitia nchi kavu.
14 Now when he was come vnto vs to Assos, and we had receiued him, we came to Mitylenes.
Alipotufikia huko Aso, tukampakia kwenye Meli tukaenda Mitilene.
15 And wee sailed thence, and came the next day ouer against Chios, and the next day we arriued at Samos, and tarried at Trogyllium: the next day we came to Miletum.
Kisha sisi tukatweka kutoka huko na siku ya pili tulifika upande wa pili wa kisiwa cha Kio. Siku iliyofuata, tukawasili kisiwa cha Samo, na kesho yake tukafika mji wa Mileto.
16 For Paul had determined to saile by Ephesus, because hee woulde not spend the time in Asia: for he hasted to be, if hee could possible, at Hierusalem, at the day of Pentecost.
Kwa sababu Paulo alikuwa ameamua kusafiri kupitia Efeso, ili kwamba asitumie muda wowote katika Asia; kwa maana alikuwa na haraka ya kuwahi Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu ya Pentekoste, kama ingeliwezekana yeye kufanya hivyo.
17 Wherefore from Miletum, hee sent to Ephesus, and called the Elders of the Church.
Kutoka Mileto akatuma watu hadi Efeso na akawaita wazee wa Kanisa.
18 Who when they were come to him, hee said vnto them, Ye know from the first day that I came into Asia, after what maner I haue bene with you at all seasons,
Walipofika kwake, akawaambia, ninyi wenyewe mwajua tangu siku ya kwanza nilipokanyaga hapa Asia, jinsi nilivyokuwa kwenu muda wote.
19 Seruing the Lord with all modestie, and with many teares, and tentations, which came vnto me by the layings awaite of the Iewes,
Nimemtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote na kwa machozi, na mateso yaliyonipata mimi kwa hila za Wayahudi.
20 And how I kept backe nothing that was profitable, but haue shewed you, and taught you openly and throughout euery house,
Mwajua jinsi ambavyo sikujizuia kutangaza kwenu kitu chochote ambacho kilikuwa muhimu, na jinsi mimi nilivyowafundisha wazi wazi na pia kwenda nyumba kwa nyumba.
21 Witnessing both to the Iewes, and to the Grecians the repentance towarde God, and faith toward our Lord Iesus Christ.
Mnajua jinsi mimi nilivyoendelea kuwaonya Wayahudi na Wayunani juu ya toba kwa Mungu na imani katika Bwana wetu Yesu.
22 And nowe beholde, I goe bound in the Spirit vnto Hierusalem, and know not what things shall come vnto me there,
Na sasa, angalieni, mimi, nikiwa ninamtii Roho Mtakatifu kuelekea Yerusalemu, nisiyajue mambo ambayo yatanitokea mimi huko,
23 Saue that ye holy Ghost witnesseth in euery citie, saying, that bondes and afflictions abide me.
ila kwa kuwa Roho Mtakatifu hunishuhudia mimi katika kila mji na anasema kwamba minyororo na mateso ndivyo vinavyoningojea.
24 But I passe not at all, neither is my life deare vnto my selfe, so that I may fulfill my course with ioye, and the ministration which I haue receiued of the Lord Iesus, to testifie the Gospell of the grace of God.
Lakini mimi si kufikiria kwamba maisha yangu ni kwa njia yoyote ya thamani kwangu, ili niweze kumaliza mwendo wangu na huduma niliyopokea kutoka kwa Bwana Yesu, kuishuhudia injili ya neema ya Mungu.
25 And now behold, I know that henceforth ye all, through whome I haue gone preaching the kingdome of God, shall see my face no more.
Na sasa, tazama, najua kwamba wote, miongoni mwa wale nilioenda kuwahubiri Ufalme, hamtaniona uso tena.
26 Wherefore I take you to recorde this day, that I am pure from the blood of all men.
Kwa hiyo nawashuhudia leo hii, kwamba sina hatia kwa damu ya mtu yeyote.
27 For I haue kept nothing backe, but haue shewed you all the counsell of God.
Kwa maana sikujizuia kuwatangazia mapenzi yote ya Mungu.
28 Take heede therefore vnto your selues, and to all the flocke, whereof the holy Ghost hath made you Ouerseers, to feede the Church of God, which hee hath purchased with that his owne blood.
Kwa hiyo iweni waangalifu juu yenu ninyi wenyewe, na juu ya kundi lolote ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi. Iweni waangalifu kulichunga kusanyiko la Bwana, ambalo alilinunua kwa damu yake mwenyewe.
29 For I knowe this, that after my departing shall grieuous wolues enter in among you, not sparing the flocke.
Najua kwamba baada ya kuondoka kwangu, mbwa mwitu wakali wataingia kwenu, na wasilihurumie kundi.
30 Moreouer of your owne selues shall men arise speaking peruerse thinges, to drawe disciples after them.
Najua kwamba hata miongoni mwenu wenyewe baadhi ya watu watakuja na kusema mambo mapotovu, ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao.
31 Therefore watche, and remember, that by the space of three yeres I ceased not to warne euery one, both night and day with teares.
Kwa hiyo muwe macho. Kumbukeni kwamba kwa miaka mitatu sikuweza kuacha kuwafundisha kila mmoja wenu kwa machozi usiku na mchana.
32 And nowe brethren, I commend you to God, and to the worde of his grace, which is able to build further, and to giue you an inheritance, among all them, which are sanctified.
Na sasa mimi nawakabidhi kwa Mungu, na kwa neno la neema yake, ambalo laweza kuwajenga na kuwapa urithi pamoja nao wote waliowekwa wakfu kwa Mungu.
33 I haue coueted no mans siluer, nor gold, nor apparell.
Sikutamani fedha, dhahabu, au mavazi.
34 Yea, ye knowe, that these handes haue ministred vnto my necessities, and to them that were with me.
Mnajua ninyi wenyewe kwamba mikono hii imenipatia mahitaji yangu mwenyewe na mahitaji ya wale waliokuwa pamoja nami.
35 I haue shewed you all things, howe that so labouring, ye ought to support the weake, and to remember the wordes of the Lord Iesus, howe that hee saide, It is a blessed thing to giue, rather then to receiue.
Katika mambo yote niliwapa mfano wa jinsi inavyopasa kuwasaidia wanyonge kwa kufanya kazi, na jinsi mnavyopaswa kukumbuka maneno ya Bwana Yesu, maneno ambayo yeye mwenyewe alisema: “Ni heri kutoa kuliko kupokea.”
36 And when he had thus spoken, he kneeled downe, and prayed with them all.
Baada ya kusema namna hii, alipiga magoti akaomba pamoja nao.
37 Then they wept all abundantly, and fell on Pauls necke, and kissed him,
Wote wakalia sana na kumwangukia Paulo shingoni na kumbusu.
38 Being chiefly sorie for the words which he spake, That they should see his face no more. And they accompanied him vnto the shippe.
Walihuzunika zaidi ya yote kwa sababu ya kile ambacho alikuwa amesema, kwamba kamwe hawatauona uso wake tena. Kisha wakamsindikiza merikebuni.

< Acts 20 >