< Acts 2 >

1 And when the day of Pentecost was come, they were al with one accord in one place.
Siku ya Pentekoste ilipowadia, waamini wote walikuwa mahali pamoja.
2 And suddenly there came a sounde from heauen, as of a russhing and mightie winde, and it filled all the house where they sate.
Ghafula sauti kama mvumo mkubwa wa upepo mkali uliotoka mbinguni ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi.
3 And there appeared vnto them clouen tongues, like fire, and it sate vpon eche of them.
Zikatokea ndimi kama za moto zilizogawanyika na kukaa juu ya kila mmoja wao.
4 And they were all filled with the holy Ghost, and began to speake with other tongues, as the Spirit gaue them vtterance.
Wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, wakaanza kunena kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia.
5 And there were dwelling at Hierusalem Iewes, men that feared God, of euery nation vnder heauen.
Basi walikuwepo Yerusalemu Wayahudi wanaomcha Mungu kutoka kila taifa chini ya mbingu.
6 Nowe when this was noised, the multitude came together and were astonied, because that euery man heard them speake his owne language.
Waliposikia sauti hii, umati wa watu ulikusanyika pamoja wakistaajabu, kwa sababu kila mmoja wao aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
7 And they wondered al, and marueiled, saying among themselues, Beholde, are not all these which speake, of Galile?
Wakiwa wameshangaa na kustaajabu wakauliza, “Je, hawa wote wanaozungumza si Wagalilaya?
8 How then heare we euery man our owne language, wherein we were borne?
Imekuwaje basi kila mmoja wetu anawasikia wakinena kwa lugha yake ya kuzaliwa?
9 Parthians, and Medes, and Elamites, and the inhabitants of Mesopotamia, and of Iudea, and of Cappadocia, of Pontus, and Asia,
Wapathi, Wamedi, Waelami, wakazi wa Mesopotamia, Uyahudi, Kapadokia, Ponto na Asia,
10 And of Phrygia, and Pamphylia, of Egypt, and of the partes of Libya, which is beside Cyrene, and strangers of Rome, and Iewes, and Proselytes,
Frigia, Pamfilia, Misri na pande za Libya karibu na Kirene na wageni kutoka Rumi,
11 Creetes, and Arabians: wee hearde them speake in our owne tongues the wonderful works of God.
Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu, sote tunawasikia watu hawa wakisema mambo makuu ya ajabu ya Mungu katika lugha zetu wenyewe.”
12 They were all then amased, and douted, saying one to another, What may this be?
Wakiwa wameshangaa na kufadhaika wakaulizana, “Ni nini maana ya mambo haya?”
13 And others mocked, and saide, They are full of newe wine.
Lakini wengine wakawadhihaki wakasema, “Hawa wamelewa divai!”
14 But Peter standing with ye Eleuen, lift vp his voice, and said vnto them, Ye men of Iudea, and ye all that inhabite Hierusalem, be this knowen vnto you, and hearken vnto my woordes.
Ndipo Petro akasimama pamoja na wale mitume kumi na mmoja, akainua sauti yake na kuhutubia ule umati wa watu, akasema: “Wayahudi wenzangu na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, jueni jambo hili mkanisikilize.
15 For these are not drunken, as yee suppose, since it is but the third houre of the day.
Hakika watu hawa hawakulewa kama mnavyodhania, kwa kuwa sasa ni saa tatu asubuhi!
16 But this is that, which was spoken by the Prophet Ioel,
La, hili ni jambo lililotabiriwa na nabii Yoeli, akisema:
17 And it shalbe in the last daies, saith God, I wil powre out of my Spirite vpon al flesh, and your sonnes, and your daughters shall prophecie, and your yong men shall see visions, and your old men shall dreame dreames.
“‘Katika siku za mwisho, asema Mungu, nitamimina Roho wangu juu ya wote wenye mwili. Wana wenu na binti zenu watatabiri, vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
18 And on my seruauntes, and on mine handmaides I will powre out of my Spirite in those daies, and they shall prophecie.
Hata juu ya watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile nitamimina Roho wangu, nao watatabiri.
19 And I wil shew wonders in heauen aboue, and tokens in the earth beneath, blood, and fire, and the vapour of smoke.
Nami nitaonyesha maajabu juu mbinguni, na ishara chini duniani: damu, moto, na mawimbi ya moshi.
20 The Sunne shalbe turned into darkenesse, and the moone into blood, before that great and notable day of the Lord come.
Jua litakuwa giza na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kuja siku ile kuu ya Bwana iliyo tukufu.
21 And it shalbe, that whosoeuer shall call on the Name of the Lord, shalbe saued.
Na kila mtu atakayeliitia jina la Bwana, ataokolewa.’
22 Yee men of Israel, heare these woordes, JESUS of Nazareth, a man approued of God among you with great workes, and wonders, and signes, which God did by him in the middes of you, as yee your selues also knowe:
“Enyi Waisraeli, sikilizeni maneno haya nisemayo: Yesu wa Nazareti alikuwa mtu aliyethibitishwa kwenu na Mungu kwa miujiza, maajabu na ishara, ambayo Mungu alitenda miongoni mwenu kupitia kwake, kama ninyi wenyewe mjuavyo.
23 Him, I say, being deliuered by the determinate counsell, and foreknowledge of God, after you had taken, with wicked handes you haue crucified and slaine.
Huyu mtu akiisha kutolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa kwa kujua kwake Mungu tangu zamani, ninyi, kwa mikono ya watu wabaya, mlimuua kwa kumgongomea msalabani.
24 Whome God hath raised vp, and loosed the sorrowes of death, because it was vnpossible that he should be holden of it.
Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu akamwondolea uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana yeye kushikiliwa na nguvu za mauti.
25 For Dauid sayeth concerning him, I beheld the Lord alwaies before me: for hee is at my right hand, that I should not be shaken.
Kwa maana Daudi asema kumhusu yeye: “‘Nalimwona Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.
26 Therefore did mine heart reioyce, and my tongue was glad, and moreouer also my flesh shall rest in hope,
Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika kwa tumaini.
27 Because thou wilt not leaue my soule in graue, neither wilt suffer thine Holy one to see corruption. (Hadēs g86)
Kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Aliye Mtakatifu wako kuona uharibifu. (Hadēs g86)
28 Thou hast shewed me the waies of life, and shalt make me full of ioy with thy countenance.
Umenionyesha njia za uzima, utanijaza na furaha mbele zako.’
29 Men and brethren, I may boldly speake vnto you of the Patriarke Dauid, that hee is both dead and buried, and his sepulchre remaineth with vs vnto this day.
“Ndugu zangu Waisraeli, nataka niwaambie kwa uhakika kwamba baba yetu Daudi alikufa na kuzikwa, nalo kaburi lake lipo hapa mpaka leo.
30 Therefore, seeing hee was a Prophet, and knewe that God had sworne with an othe to him, that of the fruite of his loynes hee woulde raise vp Christ concerning the flesh, to set him vpon his throne,
Lakini alikuwa nabii na alijua ya kuwa Mungu alikuwa amemwahidi kwa kiapo kwamba angemweka mmoja wa wazao wake penye kiti chake cha enzi.
31 Hee knowing this before, spake of the resurrection of Christ, that his soule shoulde not bee left in graue, neither his flesh shoulde see corruption. (Hadēs g86)
Daudi, akiona mambo yaliyoko mbele, akanena juu ya kufufuka kwa Kristo, kwamba hakuachwa kaburini, wala mwili wake haukuona uharibifu. (Hadēs g86)
32 This Iesus hath God raised vp, whereof we all are witnesses.
Mungu alimfufua huyu Yesu na sisi sote ni mashahidi wa jambo hilo.
33 Since then that he by the right hande of God hath bene exalted, and hath receiued of his Father the promise of the holy Ghost, hee hath shed foorth this which yee nowe see and heare.
Basi ikiwa yeye ametukuzwa kwa mkono wa kuume wa Mungu, amepokea kutoka kwa Baba ahadi ya Roho Mtakatifu, naye amemimina kile mnachoona sasa na kusikia.
34 For Dauid is not ascended into heauen, but he sayth, The Lord sayd to my Lord, Sit at my right hande,
Kwa kuwa Daudi hakupaa kwenda mbinguni, lakini anasema, “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
35 Vntill I make thine enemies thy footestoole.
hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
36 Therefore, let all the house of Israel know for a suretie, that God hath made him both Lord, and Christ, this Iesus, I say, whome yee haue crucified.
“Kwa hiyo Israeli wote na wajue jambo hili kwa uhakika kwamba: Mungu amemfanya huyu Yesu, ambaye ninyi mlimsulubisha, kuwa Bwana na Kristo.”
37 Now when they heard it, they were pricked in their heartes, and said vnto Peter and the other Apostles, Men and brethren, what shall we doe?
Watu waliposikia maneno haya yakawachoma mioyo yao, wakawauliza Petro na wale mitume wengine, “Ndugu zetu tufanye nini?”
38 Then Peter said vnto them, Amend your liues, and bee baptized euery one of you in the Name of Iesus Christ for the remission of sinnes: and ye shall receiue the gift of the holy Ghost.
Petro akawajibu, “Tubuni, mkabatizwe kila mmoja wenu kwa jina la Yesu Kristo, ili mpate kusamehewa dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 For the promise is made vnto you, and to your children, and to all that are a farre off, euen as many as the Lord our God shall call.
Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu na watoto wenu, na kwa wote walio mbali, na kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita amjie.”
40 And with many other words he besought and exhorted them, saying, Saue your selues from this froward generation.
Petro akawaonya kwa maneno mengine mengi na kuwasihi akisema, “Jiepusheni na kizazi hiki kilichopotoka.”
41 Then they that gladly receiued his word, were baptized: and the same day there were added to the Church about three thousand soules.
Wale wote waliopokea ujumbe wa Petro kwa furaha wakabatizwa na siku ile waliongezeka watu wapatao 3,000.
42 And they continued in the Apostles doctrine, and fellowship, and breaking of bread, and prayers.
Nao wakawa wanadumu katika mafundisho ya mitume, katika ushirika, katika kumega mkate na katika kusali.
43 And feare came vpon euery soule: and many wonders and signes were done by ye Apostles.
Kila mtu akaingiwa na hofu ya Mungu, nayo miujiza mingi na ishara zikafanywa na mitume.
44 And all that beleeued, were in one place, and had all things common.
Walioamini wote walikuwa mahali pamoja, nao walikuwa na kila kitu shirika.
45 And they sold their possessions and goods, and parted them to all me, as euery one had need.
Waliuza mali zao na vitu walivyokuwa navyo, kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.
46 And they continued dayly with one accord in the Temple, and breaking bread at home, did eate their meate together with gladnesse and singlenesse of heart,
Siku zote kwa moyo mmoja walikutana ndani ya ukumbi wa Hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, wakila chakula chao kwa furaha na moyo mweupe,
47 Praysing God, and had fauour with all the people: and the Lord added to the Church from day to day, such as should be saued.
wakimsifu Mungu na kuwapendeza watu wote. Kila siku Bwana akaliongeza kanisa wale waliokuwa wakiokolewa.

< Acts 2 >