< Acts 14 >

1 And it came to passe in Iconium, that they went both together into the Synagogue of the Iewes, and so spake, that a great multitude both of the Iewes and of the Grecians beleeued.
Ikatokea ndani ya Ikonio kwamba Paulo na Barnaba waliingia pamoja ndani ya sinagogi la Wayahudi nakuongea namna ambayo kundi kubwa la watu Wayahudi na Wayunani waliamini.
2 And the vnbeleeuing Iewes stirred vp, and corrupted the mindes of the Gentiles against the brethren.
Lakini wayahudi wasiotii waliwachochea akili wamataifa na kuwafanya kuwa wabaya dhidi ya ndugu.
3 So therefore they abode there a long time, and spake boldly in the Lord, which gaue testimonie vnto the woord of his grace, and caused signes and woders to be done by their hands.
Kwa hiyo walikaa huko kwa muda mrefu, wakiongea kwa ujasiri kwa nguvu ya Bwana, huku akitoa uthibitisho kuhusu ujumbe wa neema yake. Alifanya hivi kwa kutoa ishara na majaabu vifanywe kwa mikono ya Paulo na Barnaba.
4 But the multitude of the city was deuided: and some were with the Iewes, and some with the Apostles.
Lakini eneo kubwa la mji liligawanyika: baadhi ya watu walikuwa pamoja na Wayahudi, na baadhi pamoja na mitume.
5 And when there was an assault made both of the Gentiles, and of the Iewes with their rulers, to doe them violence, and to stone them,
Wakati wamataifa na Wayahudi walipojaribu kuwashawishi viongozi wao kuwatendea vibaya na kuwaponda mawe Paulo na Barnaba,
6 They were ware of it, and fled vnto Lystra, and Derbe, cities of Lycaonia, and vnto the region round about,
wakalitambua hilo na kukimbilia katika miji ya Likaonia, Listra na Derbe, na maeneo yanayozunguka pale,
7 And there preached the Gospel.
na huko waliihubiri injili.
8 Nowe there sate a certaine man at Lystra, impotent in his feete, which was a creeple from his mothers wombe, who had neuer walked.
Na huko Listra palikuwa na mtu mmoja aliyekaa, hakuwa na nguvu miguuni mwake, kilema kutoka tumboni mwa mama yake, hajawahi kutembea.
9 He heard Paul speake: who beholding him, and perceiuing that he had faith to be healed,
Mtu huyu alimsikia Paulo akiongea. Paulo alimkazia macho na akaona kwamba alikuwa na imani ya kuponywa.
10 Said with a loude voyce, Stand vpright on thy feete. And he leaped vp, and walked.
Hivyo alisema kwake kwa sauti ya juu, “Simama kwa miguu yako.” Na yule mtu aliruka juu na kuanza kutembea.
11 Then when the people sawe what Paul had done, they lift vp their voyces, saying in ye speach of Lycaonia, Gods are come downe to vs in the likenesse of men.
Umati ulipoona alichokifanya Paulo, waliinua sauti zao, wakisema katika lahaja ya Kilikaonio, “miungu imetushukia kwa namna ya binadamu.”
12 And they called Barnabas, Iupiter: and Paul, Mercurius, because hee was the chiefe speaker.
Walimwita Barnaba “Zeu,” na Paulo “Herme” kwa sababu alikuwa msemaji mkuu.
13 Then Iupiters priest, which was before their citie, brought bulles with garlands vnto the gates, and would haue sacrificed with the people.
Kuhani wa Zeu, ambaye hekalu lake lilikuwa nje ya mji, alileta fahari la ng'ombe na mtungo wa maua mpaka kwenye lango la mji, yeye na umati walitaka kutoa sadaka.
14 But when the Apostles, Barnabas and Paul heard it, they rent their clothes, and ran in among the people, crying,
Lakini mitume, Barnaba na Paulo, walipolisikia hili, walirarua mavazi yao na kwa haraka walikwenda nje kwenye umati, wakilia
15 And saying, O men, why doe yee these things? We are euen men subiect to the like passions that yee be, and preache vnto you, that yee shoulde turne from these vaine things vnto the liuing God, which made heauen and earth, and the sea, and all things that in them are:
na kusema, “Enyi watu, kwanini mnafanya mambo haya? Na sisi pia ni binadamu wenye hisia kama za kwenu. Tunawaletea habari njema, kwamba mgeuke kutoka kwenye vitu hivi visivyofaa na kumwelekea Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu, dunia na bahari na kila kitu kilichomo.
16 Who in times past suffered all the Gentiles to walke in their owne waies.
Katika nyakati zilizopita, aliwaruhusu mataifa kutembea katika njia zao wenyewe.
17 Neuerthelesse, hee left not him selfe without witnes, in that hee did good and gaue vs raine from heauen, and fruitful seasons, filling our hearts with foode, and gladnesse.
Lakini bado, hakuondoka pasipo shahidi, katika hilo alifanya vizuri na akawapatia mvua kutoka mbinguni na nyakati za mazao, akiwajaza mioyo yenu kwa vyakula na furaha”
18 And speaking these things, scarce appeased they the multitude, that they had not sacrificed vnto them.
Hata kwa maneno haya, Paulo na Barnaba kwa shida waliuzuia umati kuwatolea sadaka.
19 Then there came certaine Iewes from Antiochia and Iconium, which when they had persuaded the people, stoned Paul, and drewe him out of the citie, supposing he had bene dead.
Lakini baadhi ya Wayahudi kutoka Antiokia na Ikonio walikuja kuushawishi umati. Wakampiga mawe Paulo na kumburuta hadi nje ya mji, wakidhani alikuwa amekufa.
20 Howbeit, as the disciples stoode rounde about him, hee arose vp, and came into the citie, and the next day hee departed with Barnabas to Derbe.
Hata hivyo wanafunzi walikuwa wamesimama karibu naye, aliamka, wakaingia mjini. Siku ya pili, aliende Derbe na Barnaba.
21 And after they had preached the glad tidings of the Gospel to that citie, and had taught many, they returned to Lystra, and to Iconium, and to Antiochia,
Baada ya kufundisha injili katika mji ule na kuwafanya wanafunzi wengi, walirudi Listra, hadi Ikoniamu, na hadi Antiokia.
22 Confirming the disciples hearts, and exhorting them to continue in the faith, affirming that we must through many afflictions enter into the kingdome of God.
Waliendelea kuimarisha nafsi za wanafunzi na kutiwa moyo kuendelea katika imani, akasema, “Lazima tuingie katika ufalme wa Mungu kwa kupitia mateso mengi.”
23 And when they had ordeined them Elders by election in euery Church, and prayed, and fasted, they commended them to the Lord in whome they beleeued.
Walipo wateua kwa ajili yao wazee wa kila kusanyiko la waaminio, na wakiwa wameomba na kufunga, waliwakabidhi kwa Bwana, ambaye wao walimwamini.
24 Thus they went throughout Pisidia, and came to Pamphylia.
Kisha walipita katika Pisidia, walifika Pamfilia.
25 And when they had preached the woorde in Perga, they came downe to Attalia,
Wakati walipoongea maneno katika Perga, waliteremka kwenda Atalia.
26 And thence sailed to Antiochia, from whence they had bene comended vnto the grace of God, to the woorke, which they had fulfilled.
Kutoka huko walipanda meli hadi Antiokia ambako walikuwa wamejitoa kwa neema ya Mungu kwa ajili ya kazi ambayo sasa walikuwa wameikamilisha.
27 And when they were come and had gathered the Church together, they rehearsed all the things that God had done by them, and howe he had opened the doore of faith vnto the Gentiles.
Walipofika huko Antiokia, na kulikusanya kusanyiko la pamoja, wakatoa taarifa ya mambo ambayo Mungu amefanya kwao, na jinsi alivyowafungulia mlango wa imani kwa watu wa Mataifa.
28 So there they abode a long time with the disciples.
Walikaa kwa muda mrefu na wanafunzi.

< Acts 14 >