< 2 Timothy 4 >

1 I charge thee therefore before God, and before the Lord Iesus Christ, which shall iudge the quicke and dead at that his appearing, and in his kingdome,
Nakuamuru mbele ya Mungu, na mbele ya Kristo Yesu atakayewahukumu watu walio hai na wafu, na kwa sababu anakuja kutawala akiwa Mfalme:
2 Preach the worde: be instant, in season and out of season: improue, rebuke, exhort with all long suffering and doctrine.
hubiri huo ujumbe, sisitiza kuutangaza (iwe ni wakati wa kufaa au wakati usiofaa), karipia, onya na himiza watu ukiwafundisha kwa uvumilivu wote.
3 For the time will come, when they will not suffer wholesome doctrine: but hauing their eares itching, shall after their owne lustes get them an heape of teachers,
Utakuja wakati ambapo watu hawatasikiliza mafundisho ya kweli, ila watafuata tamaa zao wenyewe na kujikusanyia walimu tele watakaowaambia mambo yale tu ambayo masikio yao yako tayari kusikia.
4 And shall turne their eares from the trueth, and shalbe giuen vnto fables.
Watakataa kuusikia ukweli, watageukia hadithi za uongo.
5 But watch thou in all thinges: suffer aduersitie: doe the worke of an Euangelist: cause thy ministerie to be throughly liked of.
Wewe, lakini, uwe macho katika kila hali; vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Habari Njema, timiza kikamilifu utumishi wako.
6 For I am nowe readie to be offered, and the time of my departing is at hand.
Kwa upande wangu mimi, niko karibu kabisa kutolewa dhabihu na wakati wa kufariki kwangu umefika.
7 I haue fought a good fight, and haue finished my course: I haue kept the faith.
Nimefanya bidii katika mashindano, nimemaliza safari yote na imani nimeitunza.
8 For hence foorth is laide vp for me the crowne of righteousnesse, which the Lord the righteous iudge shall giue me at that day: and not to me onely, but vnto all them also that loue that his appearing.
Na sasa imebakia tu kupewa tuzo la ushindi kwa maisha ya uadilifu, tuzo ambalo Bwana Hakimu wa haki, atanipa mimi Siku ile na wala si mimi tu, ila na wale wote wanaotazamia kwa upendo kutokea kwake.
9 Make speede to come vnto me at once:
Fanya bidii kuja kwangu karibuni.
10 For Demas hath forsaken me, and hath embraced this present world, and is departed vnto Thessalonica. Crescens is gone to Galatia, Titus vnto Dalmatia. (aiōn g165)
Dema ameupenda ulimwengu huu akaniacha na kwenda zake Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia, na Tito amekwenda Dalmatia. (aiōn g165)
11 Onely Luke is with me. Take Marke and bring him with thee: for he is profitable vnto me to minister.
Luka peke yake ndiye aliye hapa pamoja nami. Mpate Marko uje naye, kwa maana ataweza kunisaidia katika kazi yangu.
12 And Tychicus haue I sent to Ephesus.
Nilimtuma Tukiko kule Efeso.
13 The cloke that I left at Troas with Carpus, when thou commest, bring with thee, and the bookes, but specially the parchments.
Utakapokuja niletee koti langu nililoacha kwa Karpo kule Troa; niletee pia vile vitabu, na hasa vile vilivyotengenezwa kwa ngozi.
14 Alexander the coppersmith hath done me much euill: the Lord rewarde him according to his workes.
Yule sonara aitwaye Aleksanda amenitendea maovu mengi; Bwana atamlipa kufuatana na hayo matendo yake.
15 Of whome be thou ware also: for he withstoode our preaching sore.
Jihadhari naye kwa sababu aliupinga ujumbe wetu kwa ukali.
16 At my first answering no man assisted me, but all forsooke me: I pray God, that it may not be laide to their charge.
Wakati nilipojitetea kwa mara ya kwanza hakuna mtu aliyesimama upande wangu; wote waliniacha. Mungu asiwahesabie kosa hilo!
17 Notwithstanding the Lord assisted me, and strengthened me, that by me the preaching might be fully beleeued, and that al the Gentiles should heare: and I was deliuered out of the mouth of the lion.
Lakini, Bwana alikaa pamoja nami, akanipa nguvu, hata nikaweza kuutangaza ujumbe wote, watu wa mataifa wausikie; tena nikaokolewa katika hukumu ya kifo kama kinywani mwa simba.
18 And the Lord will deliuer me from euery euil worke, and will preserue me vnto his heauenly kingdome: to whome be praise for euer and euer, Amen. (aiōn g165)
Bwana ataniokoa na mambo yote maovu, na kunichukua salama mpaka katika Utawala wake wa mbinguni. Kwake uwe utukufu milele na milele! Amina. (aiōn g165)
19 Salute Prisca and Aquila, and the householde of Onesiphorus.
Wasalimu Priska na Akula, pamoja na jamaa ya Onesiforo.
20 Erastus abode at Corinthus: Trophimus I left at Miletum sicke.
Erasto alibaki Korintho, naye Trofimo nilimwacha Mileto kwa sababu alikuwa mgonjwa.
21 Make speede to come before winter. Eubulus greeteth thee, and Pudens, and Linus, and Claudia, and all the brethren.
Fanya bidii kuja kabla ya majira ya baridi. Ebulo, Pude, Lino na Klaudia wanakusalimu; vilevile ndugu wengine wote.
22 The Lord Iesus Christ be with thy spirit. Grace be with you, Amen. ‘The second Epistle written from Rome vnto Timotheus, the first Bishop elected of the Church of Ephesus, when Paul was presented the second time before the Emperour Nero.’
Bwana awe nawe rohoni mwako. Nawatakieni nyote neema.

< 2 Timothy 4 >