< 2 Samuel 21 >
1 Then there was a famine in the dayes of Dauid, three yeeres together: and Dauid asked counsell of the Lord, and the Lord answered, It is for Saul, and for his bloodie house, because hee slewe the Gibeonites.
Wakati wa utawala wa Daudi kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu mfululizo, kwa hiyo Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, “Ni kwa sababu ya Sauli na nyumba yake iliyotiwa madoa ya damu, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”
2 Then ye King called the Gibeonites and said vnto them. (Now the Gibeonites were not of the children of Israel, but a remnant of the Amorites, vnto whom ye children of Israel had sworne: but Saul sought to slay them for his zeale toward the children of Israel and Iudah)
Mfalme akawaita Wagibeoni na kuzumgumza nao. (Wagibeoni hawakuwa wa wana wa Israeli, ila walikuwa mabaki ya Waamori. Waisraeli walikuwa wameapa kuwaacha hai, lakini Sauli katika wivu wake kwa ajili ya Israeli na Yuda, alikuwa amejaribu kuwaangamiza.)
3 And Dauid said vnto the Gibeonites, What shall I doe for you, and wherewith shall I make the atonement, that ye may blesse the inheritance of the Lord?
Daudi akawauliza Wagibeoni, “Niwatendee nini? Nitawaridhishaje ili mbariki urithi wa Bwana?”
4 The Gibeonites then answered him, Wee will haue no siluer nor golde of Saul nor of his house, neither for vs shalt thou kill any man in Israel. And he said, What ye shall say, that will I doe for you.
Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
5 Then they answered the King, The man that consumed vs and that imagined euill against vs, so that we are destroyed from remaining in any coast of Israel,
Wakamjibu mfalme, “Kwa habari ya mtu aliyetuangamiza na kufanya hila mbaya dhidi yetu ili kwamba tuangamizwe na tusiwe na yeyote katika Israeli,
6 Let seuen men of his sonnes be deliuered vnto vs, and we will hang them vp vnto the Lord in Gibeah of Saul, the Lordes chosen. And the King said, I will giue them.
tupatieni wazao wake saba wa kiume tuwaue hadharani mbele za Bwana huko Gibea ya Sauli, aliyekuwa amechaguliwa na Bwana.” Basi mfalme akasema, “Nitawakabidhi kwenu.”
7 But the King had compassion on Mephibosheth the sonne of Ionathan the sonne of Saul, because of the Lordes othe, that was betweene them, euen betweene Dauid and Ionathan the sonne of Saul.
Mfalme akamhifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa sababu ya kile kiapo mbele za Bwana kati ya Daudi na Yonathani.
8 But the King tooke the two sonnes of Rizpah the daughter of Aiah, whome shee bare vnto Saul, euen Armoni and Mephibosheth and the fiue sonnes of Michal, the daughter of Saul, whome shee bare to Adriel the sonne of Barzillai the Meholathite.
Lakini mfalme akamchukua Armoni na Mefiboshethi, wana wawili wa Rispa binti Aiya, ambao alikuwa amemzalia Sauli, pamoja na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliokuwa amemzalia Adrieli mwana wa Barzilai, Mmeholathi.
9 And hee deliuered them vnto the handes of the Gibeonites, which hanged them in the mountaine before the Lord: so they died all seuen together, and they were slaine in the time of haruest: in the first dayes, and in the beginning of barly haruest.
Akawakabidhi kwa Wagibeoni, ambao waliwaua na kuwaweka wazi juu ya kilima mbele za Bwana. Wote saba walianguka kwa pamoja; waliuawa katika siku za kwanza za mavuno, mara tu uvunaji wa shayiri ulipokuwa unaanza.
10 Then Rizpah the daughter of Aiah tooke sackecloth and hanged it vp for her vpon the rocke, from the beginning of haruest, vntill water dropped vpon them from the heauen, and suffered neither the birdes of the aire to light on the by day, nor beasts of the fielde by night.
Rispa binti Aiya akachukua nguo ya gunia, akajitandikia juu ya mwamba. Kuanzia mwanzo wa mavuno mpaka mvua ziliponyesha juu ya miili ya hao waliouawa, Rispa hakuruhusu ndege wa angani kuwagusa wakati wa mchana, wala wanyama wa mwitu wakati wa usiku.
11 And it was told Dauid, what Rizpah the daughter of Aiah ye concubine of Saul had done.
Daudi alipoambiwa kile Rispa binti Aiya, suria wa Sauli, alichokuwa amekifanya,
12 And Dauid went and tooke the bones of Saul and the bones of Ionathan his sonne from the citizens of Iabesh Gilead, which had stollen them from the streete of Beth-shan, where the Philistims had hanged them, when the Philistims had slaine Saul in Gilboa.
alikwenda akachukua mifupa ya Sauli na mwanawe Yonathani kutoka kwa watu wa Yabeshi-Gileadi. (Walikuwa wameichukua kwa siri kutoka uwanja wa watu wote huko Beth-Shani, mahali ambapo Wafilisti walikuwa wamewatundika baada ya kumuua Sauli huko Gilboa.)
13 So hee brought thence the bones of Saul and the bones of Ionathan his sonne, and they gathered the bones of them that were hanged.
Daudi akaileta mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani kutoka huko, pia mifupa ya wale waliokuwa wameuawa na kutupwa ilikusanywa.
14 And the bones of Saul and of Ionathan his sonne buried they in the coutrey of Beniamin in Zelah, in the graue of Kish his father: and when they had perfourmed all that the King had commanded, God was then appeased with the land.
Wakazika mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani katika kaburi la Kishi, babaye Sauli, huko Sela katika nchi ya Benyamini, nao wakafanya kila kitu mfalme alichoagiza. Baada ya hayo, Mungu akajibu maombi kwa ajili ya nchi.
15 Againe the Philistims had warre with Israel: and Dauid went downe, and his seruants with him, and they fought against the Philistims, and Dauid fainted.
Kwa mara nyingine tena kulikuwa na vita kati ya Wafilisti na Israeli. Daudi akashuka pamoja na watu wake ili kupigana dhidi ya Wafilisti, naye akawa amechoka sana.
16 Then Ishi-benob which was of the sonnes of Haraphah (the head of whose speare wayed three hundreth shekels of brasse) euen he being girded with a newe sword, thought to haue slaine Dauid.
Naye Ishbi-Benobu, mmoja wa wazao wa Warefai, ambaye mkuki wake ulikuwa na uzito wa shekeli 300 za shaba, alikuwa amejifunga upanga mpya, naye alisema angemuua Daudi.
17 But Abishai the sonne of Zeruiah succoured him, and smote the Philistim, and killed him. Then Dauids men sware vnto him, saying, Thou shalt goe no more out with vs to battell, lest thou quench the light of Israel.
Lakini Abishai mwana wa Seruya akaja kumwokoa Daudi; akampiga huyo Mfilisti, akamwangusha chini na kumuua. Ndipo watu wakamwapia Daudi, wakisema, “Kamwe hutakwenda tena nasi vitani, ili kwamba taa ya Israeli isije ikazimwa.”
18 And after this also there was a battell with the Philistims at Gob, then Sibbechai the Hushathite slewe Saph, which was one of ye sonnes of Haraphah.
Baada ya muda, kukawa na vita nyingine na Wafilisti, huko Gobu. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Safu, mmoja wa wazao wa Warefai.
19 And there was yet another battel in Gob with the Philistims, where Elhanah the sonne of Iaare-oregim, a Bethlehemite slewe Goliath the Gittite: the staffe of whose speare was like a weauers beame.
Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
20 Afterward there was also a battel in Gath, where was a man of a great stature, and had on euerie hand sixe fingers, and on euerie foote sixe toes, foure and twentie in nomber: who was also the sonne of Haraphah.
Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita kila mguu, jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
21 And when hee reuiled Israel, Ionathan the sonne of Shima the brother of Dauid slewe him.
Alipowadhihaki Israeli, Yonathani mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
22 These foure were borne to Haraphah in Gath, and died by the hande of Dauid and by the hands of his seruants.
Hawa wanne walikuwa wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.