< 2 Samuel 2 >

1 After this, Dauid asked counsel of the Lord, saying, Shall I go vp into any of the cities of Iudah? And the Lord sayd vnto him, Goe vp. And Dauid sayd Whither shall I goe? Hee then answered, Vnto Hebron.
Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
2 So Dauid went vp thither, and his two wiues also, Ahinoam the Izreelite, and Abigail Nabals wife the Carmelite.
Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
3 And Dauid brought vp the men that were with him, euery man with his houshold, and they dwelt in the cities of Hebron.
Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
4 Then the men of Iudah came, and there they anoynted Dauid King ouer the house of Iudah. And they tolde Dauid, saying, that the men of Iabesh Gilead buried Saul.
Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
5 And Dauid sent messengers vnto the men of Iabesh Gilead, and said vnto them, Blessed are ye of the Lord, that yee haue shewed such kindenes vnto your lord Saul, that you haue buried him.
akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
6 Therefore now the Lord shewe mercie and trueth vnto you: and I will recompence you this benefite, because ye haue done this thing.
Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
7 Therefore nowe let your handes be strong, and be you valiant: albeit your master Saul bee dead, yet neuerthelesse the house of Iudah hath anoynted me King ouer them.
Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
8 But Abner the sonne of Ner that was captaine of Sauls hoste, tooke Ish-bosheth the sonne of Saul, and brought him to Mahanaim,
Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
9 And made him King ouer Gilead, and ouer the Ashurites, and ouer Izreel, and ouer Ephraim, and ouer Beniamin, and ouer al Israel.
Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
10 Ish-bosheth Sauls sonne was fourtie yeere olde when he began to reigne ouer Israel, and reigned two yeere: but the house of Iudah followed Dauid.
Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
11 (And the time which Dauid reigned in Hebron ouer the house of Iudah, was seuen yeere and sixe moneths)
Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
12 And Abner the sonne of Ner, and the seruantes of Ish-bosheth the sonne of Saul went out of Mahanaim to Gibeon.
Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
13 And Ioab the sonne of Zeruiah, and the seruants of Dauid went out and met one another by the poole of Gibeon: and they sate downe, the one on the one side of the poole, and the other on the otherside of the poole.
Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
14 Then Abner saide to Ioab, Let the yong men nowe arise, and play before vs. And Ioab said, Let them arise.
Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
15 Then there arose and went ouer twelue of Beniamin by number, which perteined to Ish-bosheth the sonne of Saul, and twelue of the seruants of Dauid.
Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
16 And euery one caught his fellowe by the head, and thrust his sword in his fellowes side, so they fell downe together: wherefore ye place was called Helkath-hazzurim, which is in Gibeon.
Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
17 And the battel was exceeding sore that same day: for Abner and the men of Israel fell before the seruants of Dauid.
Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
18 And there were three sonnes of Zeruiah there, Ioab, and Abishai, and Asahel. And Asahel was as light on foote as a wilde roe.
Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
19 And Asahel followed after Abner, and in going he turned neither to the right hand nor to the left from Abner.
Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
20 Then Abner looked behind him, and said, Art thou Asahel? And he answered, Yea.
Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
21 Then Abner said, Turne thee either to the right hande, or to the left, and take one of the yong men, and take thee his weapons: and Asahel would not depart from him.
Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
22 And Abner saide to Asahel, Depart from me: wherefore shoulde I smite thee to the grounde? howe then shoulde I be able to holde vp my face to Ioab thy brother?
Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
23 And when he woulde not depart, Abner with the hinder ende of the speare smote him vnder the fift ryb, that the speare came out behind him: and he fell downe there, and dyed in his place. And as many as came to the place where Asahel fell downe and dyed, stoode still.
Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
24 Ioab also and Abishai pursued after Abner: and the sunne went downe, when they were come to the hill Ammah, that lieth before Giah, by the way of the wildernesse of Gibeon.
Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
25 And the children of Beniamin gathered them selues together after Abner, and were on an heape and stoode on the top of an hill.
Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
26 Then Abner called to Ioab, and said, Shall the sworde deuoure for euer? knowest thou not, that it will be bitternesse in the latter ende? howe long then shall it be, or thou bid the people returne from following their brethren?
Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
27 And Ioab sayde, As God liueth, if thou haddest not spoken, surely euen in the morning the people had departed euery one backe from his brother.
Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
28 So Ioab blew a trumpet, and all the people stoode still, and pursued after Israel no more, neither fought they any more.
Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
29 And Abner and his men walked all that night through the plaine, and went ouer Iorden, and past through all Bithron till they came to Mahanaim.
Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
30 Ioab also returned backe from Abner: and when he had gathered all the people together, there lacked of Dauids seruants nineteene men and Asahel.
Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
31 But the seruants of Dauid had smitten of Beniamin, and of Abners men, so that three hundreth and threescore men dyed.
Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
32 And they tooke vp Asahel, and buried him in the sepulchre of his father, which was in Bethlehem: and Ioab and his men went all night, and when they came to Hebron, the day arose.
Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.

< 2 Samuel 2 >