< 2 Peter 1 >
1 Simon Peter a seruant and an Apostle of Iesus Christ, to you which haue obteined like precious faith with vs by the righteousnesse of our God and Sauiour Iesus Christ:
Simoni Petro, mtumishi na mtume wa Yesu Kristo: Kwa wale ambao kwa njia ya haki ya Mungu na Mwokozi wetu Yesu Kristo mmepokea imani iliyo na thamani kama yetu:
2 Grace and peace be multiplied to you, through the acknowledging of God, and of Iesus our Lord,
Neema na amani iwe kwenu kwa wingi katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu.
3 According as his diuine power hath giuen vnto vs all things that perteine vnto life and godlinesse, through the acknowledging of him that hath called vs vnto glory and vertue.
Uweza wake wa uungu umetupatia mambo yote tunayohitaji kwa ajili ya uzima na uchaji wa Mungu, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.
4 Whereby most great and precious promises are giuen vnto vs, that by them ye should be partakers of the diuine nature, in that ye flee the corruption, which is in the worlde through lust.
Kwa sababu hiyo, ametukirimia ahadi zake kuu na za thamani kupitia mambo haya, ili kupitia hayo mpate kuwa washiriki wa asili ya uungu, na kuokoka kutoka upotovu ulioko duniani unaosababishwa na tamaa mbaya.
5 Therefore giue euen all diligence thereunto: ioyne moreouer vertue with your faith: and with vertue, knowledge:
Kwa sababu hii hasa, jitahidini sana katika imani yenu kuongeza wema; na katika wema, maarifa;
6 And with knowledge, temperance: and with temperance, patience: and with patience, godlines:
katika maarifa, kiasi; katika kiasi, saburi; katika saburi, utauwa;
7 And with godlines, brotherly kindnes: and with brotherly kindnes, loue.
katika utauwa, upendano wa ndugu; na katika upendano wa ndugu, upendo.
8 For if these things be among you, and abound, they will make you that ye neither shalbe idle, nor vnfruitfull in the acknowledging of our Lord Iesus Christ:
Kwa maana haya yakiwa ndani yenu kwa wingi na kuzidi kuongezeka, yanawasaidia msikose bidii wala kutozaa matunda katika kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.
9 For he that hath not these things, is blinde, and can not see farre off, and hath forgotten that he was purged from his olde sinnes.
Lakini mtu yeyote asipokuwa na mambo haya haoni mbali, na ni kipofu, naye amesahau kule kutakaswa kutoka dhambi zake za zamani.
10 Wherefore, brethren, giue rather diligence to make your calling and election sure: for if ye doe these things, ye shall neuer fall.
Kwa hiyo, ndugu zangu, fanyeni bidii zaidi kuuthibitisha wito wenu na uteule wenu. Kwa maana mkifanya hivyo, hamtajikwaa kamwe,
11 For by this meanes an entring shalbe ministred vnto you aboundantly into the euerlasting kingdome of our Lord and Sauiour Iesus Christ. (aiōnios )
na mtajaliwa kwa ukarimu mwingi kuingia katika ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. (aiōnios )
12 Wherefore, I will not be negligent to put you alwayes in remembrance of these things, though that ye haue knowledge, and be stablished in the present trueth.
Hivyo nitawakumbusha mambo haya siku zote, hata ingawa mnayajua na mmethibitishwa katika kweli mliyo nayo.
13 For I thinke it meete as long as I am in this tabernacle, to stirre you vp by putting you in remembrance,
Naona ni vyema kuwakumbusha mambo haya wakati wote niwapo katika hema hili ambalo ni mwili wangu,
14 Seeing I knowe that the time is at hand that I must lay downe this my tabernacle, euen as our Lord Iesus Christ hath shewed me.
kwa sababu najua ya kwamba hivi karibuni nitaliweka kando, kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyoliweka wazi kwangu.
15 I will endeuour therefore alwayes, that ye also may be able to haue remembrance of these things after my departing.
Nami nitafanya kila juhudi kuona kwamba baada ya kuondoka kwangu mtaweza kuyakumbuka mambo haya siku zote.
16 For we followed not deceiuable fables when we opened vnto you the power, and comming of our Lord Iesus Christ, but with our eyes we saw his maiestie:
Tulipowafahamisha juu ya uweza na kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo, hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, bali tulishuhudia kwa macho yetu ukuu wake.
17 For he receiued of God the Father honour and glory, when there came such a voyce to him from that excellent glory, This is my beloued Sonne, in whom I am well pleased.
Alipewa heshima na utukufu kutoka kwa Mungu Baba, sauti ilipomjia katika Utukufu Mkuu, ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa naye sana.”
18 And this voyce we heard when it came from heauen, being with him in the Holy mount.
Sisi wenyewe tuliisikia sauti hii ambayo ilitoka mbinguni, wakati tulipokuwa pamoja naye kwenye ule mlima mtakatifu.
19 We haue also a most sure worde of the Prophets, to the which ye doe well that yee take heede, as vnto a light that shineth in a darke place, vntill the day dawne, and the day starre arise in your hearts.
Nasi tunalo pia neno la hakika zaidi la unabii, ambalo mtafanya vyema mkiliangalia kwa bidii, kama vile nuru inavyongʼaa gizani, hadi kupambazuka na nyota ya asubuhi izuke mioyoni mwenu.
20 So that yee first knowe this, that no prophecie of the Scripture is of any priuate interpretation.
Zaidi ya yote, yawapasa mjue kwamba hakuna unabii katika Maandiko uliofasiriwa kama alivyopenda nabii mwenyewe.
21 For the prophecie came not in olde time by the will of man: but holy men of God spake as they were moued by the holy Ghost.
Kwa maana unabii haukuja kamwe kwa mapenzi ya mwanadamu, bali watu walinena yaliyotoka kwa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu.