< 2 Corinthians 10 >
1 Nowe I Paul my selfe beseech you by the meekenes, and gentlenes of Christ, which when I am present among you am base, but am bolde toward you being absent:
Mimi Paulo mwenyewe ambaye naonekana kuwa mpole nikiwa pamoja nanyi, lakini mkali wakati nikiwa mbali nanyi, nawasihini kwa huruma na wema wake Kristo.
2 And this I require you, that I neede not to be bolde when I am present, with that same confidence, wherewith I thinke to bee bolde against some, which esteeme vs as though wee walked according to the flesh.
Nawaombeni msinisababishe kuwa mkali wakati nitakapokuja, maana nina hakika naweza kuwa mkali kwa wote wale wanaotudhania kwamba tunaishi kidunia.
3 Neuerthelesse, though wee walke in the flesh, yet we doe not warre after the flesh.
Kweli tunaishi duniani, lakini hatupigani vita kidunia.
4 (For the weapons of our warrefare are not carnall, but mightie through God, to cast downe holdes)
Maana, silaha tunazotumia katika vita vyetu si silaha za kidunia, ila ni nguvu za Mungu zenye kuharibu ngome zote. Tunaharibu hoja zote za uongo,
5 Casting downe the imaginations, and euery high thing that is exalted against the knowledge of God, and bringing into captiuitie euery thought to the obedience of Christ,
na kubomoa kila kizuizi cha majivuno kilichowekwa kuipinga elimu ya Mungu; tunaziteka fikira zote na kuzifanya zimtii Kristo.
6 And hauing ready the vengeance against all disobedience, when your obedience is fulfilled.
Mkisha kuwa wakamilifu katika kutii, sisi tuko tayari kuadhibu kila namna ya kutotii.
7 Looke yee on things after the appearance? If any man trust in himselfe that hee is Christes, let him consider this againe of himself, that as he is Christes, euen so are we Christes.
Ninyi hutazama mambo kwa nje tu. Je, yupo mtu yeyote anayedhani kwamba yeye ni wa Kristo? Sawa! Basi, afikirie vilevile kwamba sisi pia ni wa Kristo kama yeye alivyo wa Kristo.
8 For though I shoulde boast somewhat more of our authoritie, which the Lord hath giuen vs for edification, and not for your destruction, I should haue no shame.
Hata kama nimezidi katika kujivuna kwangu juu ya ule uwezo aliotupa—uwezo wa kuwajenga na sio wa kubomoa—hata hivyo sijutii hata kidogo.
9 This I say, that I may not seeme as it were to feare you with letters.
Sipendi mfikiri kwamba nataka kuwatisha ninyi kwa barua zangu.
10 For the letters, sayeth hee, are sore and strong, but his bodily presence is weake, and his speache is of no value.
Mtu anaweza kusema: “Barua za Paulo ni kali na zenye maneno mazito, lakini yeye mwenyewe anapokuwa pamoja nasi ni mtu dhaifu, na hata anapoongea maneno yake ni kama si kitu.”
11 Let such one thinke this, that such as wee are in woorde by letters, when we are absent, such wil we be also in deede, when we are present.
Mtu asemaye hivyo heri akumbuke kwamba hakuna tofauti ya yale tunayoandika katika barua wakati tuko mbali, na yale tutakayofanya wakati tutakapokuwa nanyi.
12 For wee dare not make our selues of the nomber, or to compare our selues to them, which praise themselues: but they vnderstand not that they measure themselues with themselues, and compare themselues with themselues.
Kwa vyovyote hatungethubutu kujiweka au kujilinganisha na wale watu wanaojisifia wenyewe. Watu wenye kujifanya wao kuwa kipimo cha kujipimia, na watu wanaojilinganisha wenyewe kwa wenyewe, ni wapumbavu.
13 But we wil not reioyce of things, which are not within our measure, but according to the measure of the line, whereof God hath distributed vnto vs a measure to attaine euen vnto you.
Lakini sisi hatutajivuna kupita kiasi; kujivuna huko kutabaki katika kile kipimo cha kazi aliyotukabidhi Mungu, kazi ambayo tunaifanya pia kwenu.
14 For we stretche not our selues beyonde our measure, as though wee had not attained vnto you: for euen to you also haue we come in preaching the Gospel of Christ,
Na kwa vile ninyi mu katika mipaka hiyo, hatukuipita tulipokuja kwenu, tukiwaleteeni Habari Njema juu ya Kristo.
15 Not boasting of things which are without our measure: that is, of other mens labours: and we hope, when your faith shall increase, to bee magnified by you according to our line aboundantly,
Basi, hatujivunii kazi waliyofanya wengine zaidi ya kipimo tulichopewa; ila tunatumaini kwamba imani yenu itazidi miongoni mwenu kufuatana na kipimo alichotuwekea Mungu.
16 And to preache the Gospel in those regions which are beyonde you: not to reioyce in another mans line, that is, in the thinges that are prepared alreadie.
Hapo tutaweza kuihubiri Habari Njema katika nchi nyingine, mbali nanyi; na haitakuwa shauri la kujivunia kazi waliyofanya watu wengine mahali pengine.
17 But let him that reioyceth, reioyce in the Lord.
Lakini kama yasemavyo Maandiko: “Mwenye kuona fahari na aone fahari juu ya alichofanya Bwana.”
18 For hee that praiseth himselfe, is not alowed, but he whome the Lord praiseth.
Anayekubaliwa si yule anayejisifu mwenyewe, bali yule anayesifiwa na Bwana.