< 1 Timothy 4 >
1 Now the Spirit speaketh euidently, that in the latter times some shall depart from the faith, and shall giue heede vnto spirits of errour, and doctrines of deuils,
Sasa Roho anasema waziwazi kwamba katika nyakati zijazo baadhi ya watu wataiacha imani na kuwa makini kusikiliza roho zidanganyazo na mafundisho ya kipepo yatakayofundishwa
2 Which speake lies through hypocrisie, and haue their cosciences burned with an hote yron,
katika uongo na unafiki. Dhamiri zao zitabadilishwa.
3 Forbidding to marrie, and commanding to abstaine from meates which God hath created to be receiued with giuing thankes of them which beleeue and knowe the trueth.
Watawazuia kuoa na kupokea vyakula ambavyo Mungu aliviumba vitumiwe kwa shukrani miongoni mwao waaminio na wenye kuijua kweli.
4 For euery creature of God is good, and nothing ought to be refused, if it be receiued with thankesgiuing.
Kwa sababu kila kitu ambacho Mungu amekiumba ni chema. Hakuna ambacho tunapokea kwa shukrani kinastahili kukataliwa.
5 For it is sanctified by the worde of God, and prayer.
Kwa sababu kinatakaswa kupitia neno la Mungu na kwa njia ya maombi.
6 If thou put the brethren in remembrance of these things, thou shalt be a good minister of Iesus Christ, which hast bene nourished vp in the wordes of faith, and of good doctrine, which thou hast continually followed.
Kama utayaweka mambo haya mbele ya ndugu, utakuwa mtumishi mzuri wa Yesu Kristo. Kwa sababu umestawishwa kwa maneno ya imani na kwa mafundisho mazuri ambayo umeyafuata.
7 But cast away prophane, and olde wiues fables, and exercise thy selfe vnto godlinesse.
Lakini zikatae hadithi za kidunia ambazo zinapendwa na wanawake wazee. Badala yake, jifunze mwenyewe katika utaua.
8 For bodily exercise profiteth litle: but godlinesse is profitable vnto all things, which hath the promise of the life present, and of that that is to come.
Kwa maana mazoezi ya mwili yafaa kidogo, bali utauwa wafaa sana kwa mambo yote. Hutunza ahadi kwa maisha ya sasa na yale yajayo.
9 This is a true saying, and by all meanes worthie to be receiued.
Ujumbe huu ni wakuaminiwa na unastahili kukubaliwa kabisa.
10 For therefore we labour and are rebuked, because we trust in the liuing God, which is the Sauiour of all men, specially of those that beleeue.
Kwa kuwa ni kwa sababu hii tunataabika na kufanya kazi kwa bidii sana. Kwa kuwa tunao ujasiri katika Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, lakini hasa kwa waaminio.
11 These things warne and teache.
Uyaseme na kuyafundisha mambo haya.
12 Let no man despise thy youth, but be vnto them that beleeue, an ensample, in worde, in conuersation, in loue, in spirit, in faith, and in purenesse.
Mtu yeyote asiudharau ujana wako. Badala yake, uwe mfano kwa wote waaminio, katika usemi, mwenendo, upendo, uaminifu, na usafi.
13 Till I come, giue attendance to reading, to exhortation, and to doctrine.
Mpaka nitakapokuja, dumu katika kusoma, katika kuonya, na katika kufundisha.
14 Despise not the gift that is in thee, which was giuen thee by prophecie with the laying on of the hands of the companie of the Eldership.
Usiipuuze karama iliyomo ndani yako, ambayo ulipewa kupitia unabii, kwa kuwekewa mikono na wazee.
15 These things exercise, and giue thy selfe vnto them, that it may be seene howe thou profitest among all men.
Uyajali mambo haya. Ishi katika hayo ili kukua kwako kuwe dhahiri kwa watu wote. Zingatia sana mwenendo wako na mafundisho.
16 Take heede vnto thy selfe, and vnto learning: continue therein: for in doing this thou shalt both saue thy selfe, and them that heare thee.
Dumu katika mambo haya. Maana kwa kufanya hivyo utajiokoa mwenyewe na wale wanaokusikiliza.