< 1 Timothy 2 >
1 I Exhort therefore, that first of all supplications, prayers, intercessions, and giuing of thanks be made for all men,
Kwa hiyo awali ya yote, nahitaji maombi, na dua, na maombezi, na shukrani vifanyike kwa ajili ya watu wote,
2 For Kings, and for all that are in authoritie, that we may leade a quiet and a peaceable life, in all godlinesse and honestie.
kwa ajili ya wafalme na wote ambao wako kwenye mamlaka, ili kwamba tuweze kuishi maisha ya amani na utulivu katika utauwa wote na heshima.
3 For this is good and acceptable in the sight of God our Sauiour,
Hili ni jema na lenye kukubalika mbele za Mungu Mwokozi wetu.
4 Who will that all men shalbe saued, and come vnto the acknowledging of the trueth.
Yeye hutamani kuwa watu wote waokolewe na wapate kuijua kweli.
5 For there is one God, and one Mediatour betweene God and man, which is the man Christ Iesus,
Kwa kuwa kuna Mungu mmoja, na kuna mpatanishi mmoja kati ya Mungu na mwanadamu ambaye ni Kristo Yesu.
6 Who gaue himselfe a ransome for all men, to be that testimonie in due time,
Alijitoa mwenyewe kama fidia kwa wote, kama ushuhuda kwa wakati muafaka.
7 Whereunto I am ordeined a preacher and an Apostle (I speake the trueth in Christ, and lie not) euen a teacher of the Gentiles in faith and veritie.
Kwa sababu hii, mimi mwenyewe nilifanywa kuwa mjumbe wa injili na mtume. Nasema kweli. Sisemi uongo. Mimi ni mwalimu watu Mataifa katika imani na kweli.
8 I will therefore that the men pray, euery where lifting vp pure hands without wrath, or douting.
Kwa hiyo, nataka wanaume kila mahali waombe na kuinua mikono mitakatifu bila ghadhabu na mashaka.
9 Likewise also the women, that they aray themselues in comely apparell, with shamefastnes and modestie, not with broyded heare, or gold, or pearles, or costly apparell,
Vivyo hivyo, nataka wanawake wajivike mavazi yanayokubalika, kwa heshima na kujizuia. Wasiwe na nywele zilizosukwa, au dhahabu, au Lulu, au mavazi ya gharama kubwa.
10 But (as becommeth women that professe the feare of God) with good workes.
Pia nataka wavae mavazi yanayowastahili wanawake wanaokiri uchaji kwa kupitia matendo mema.
11 Let the woman learne in silence with all subiection.
Mwanamke na ajifunze katika hali ya utulivu na kwa utii wote.
12 I permit not a woman to teache, neither to vsurpe authoritie ouer the man, but to be in silence.
Simruhusu mwanamke kufundisha, au kuwa na mamlaka juu ya mwanaume bali aishi katika hali ya ukimya.
13 For Adam was first formed, then Eue.
Kwa kuwa Adamu aliumbwa kwanza, kisha Eva.
14 And Adam was not deceiued, but the woman was deceiued, and was in the transgression.
Adamu hakudanganywa, lakini mwanamke alidanganywa kabisa katika uasi.
15 Notwithstanding, through bearing of children she shalbe saued if they continue in faith, and loue, and holines with modestie.
Hata hivyo, ataokolewa kwa kupitia kuzaa watoto, kama wataendelea katika imani na upendo na katika utakaso na akili njema.