< 1 Samuel 31 >
1 Now the Philistims fought against Israel, and the me of Israel fled away from ye Philistims, and they fell downe wounded in mount Gilboa.
Basi Wafilisti wakapigana na Israeli. Waisraeli wakawakimbia, na wengi wakauawa katika Mlima Gilboa.
2 And the Philistims preassed sore vpon Saul and his sonnes, and slewe Ionathan, and Abinadab, and Malchishua Sauls sonnes.
Wafilisti wakawafuatia kwa bidii Sauli na wanawe, wakawaua Yonathani, Abinadabu na Malki-Shua.
3 And when the battel went sore against Saul, the archers and bowmen hit him, and hee was sore wounded of the archers.
Mapigano yakawa makali sana kumzunguka Sauli, nao wapiga upinde wakampata na kumjeruhi vibaya.
4 Then saide Saul vnto his armour bearer, Drawe out thy sworde, and thrust mee through therewith, lest the vncircumcised come and thrust me through and mocke me: but his armour bearer would not, for hee was sore afraid. Therefore Saul tooke a sworde and fell vpon it.
Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Futa upanga wako unichome nao, la sivyo hawa watu wasiotahiriwa watakuja wanichome na kunidhalilisha.” Lakini mbeba silaha wake akaogopa sana wala hakuweza kufanya hivyo. Kwa hiyo Sauli akachukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia.
5 And when his armour bearer sawe that Saul was dead, he fell likewise vpon his sword, and dyed with him.
Mchukua silaha wake alipoona Sauli amekufa, naye pia akaangukia upanga wake akafa pamoja naye.
6 So Saul dyed, and his three sonnes, and his armour bearer, and all his men that same day together.
Basi Sauli, wanawe watatu, mbeba silaha wake na watu wake wote wakafa pamoja siku ile ile.
7 And when the men of Israel that were on the other side of the valley, and they of the other side Iorden saw that the men of Israel were put to flight, and that Saul and his sonnes were dead, then they left the cities, and ran away: and the Philistims came and dwelt in them.
Waisraeli waliokuwa kandokando ya bonde na wale waliokuwa ngʼambo ya Yordani walipoona kuwa jeshi la Waisraeli limekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, wakaacha miji yao na kukimbia. Nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.
8 And on the morowe when the Philistims were come to spoyle them that were slaine, they founde Saul and his three sonnes lying in mount Gilboa,
Kesho yake Wafilisti walipokuja kuwavua maiti silaha, walimkuta Sauli na wanawe watatu wameanguka katika Mlima Gilboa.
9 And they cut off his head, and stripped him out of his armour, and sent into the land of ye Philistims on euery side, that they should publish it in the temple of their idoles, and among the people.
Wakamkata Sauli kichwa na kumvua silaha zake, nao wakatuma wajumbe katika nchi yote ya Wafilisti kutangaza habari katika hekalu la sanamu zao na miongoni mwa watu wao.
10 And they layed vp his armour in the house of Ashtaroth, but they hanged vp his body on the wall of Beth-shan.
Wakaweka silaha zake katika hekalu la Maashtorethi, na kukifunga kiwiliwili chake katika ukuta wa Beth-Shani.
11 When the inhabitants of Iabesh Gilead heard, what the Philistims had done to Saul,
Watu wa Yabeshi-Gileadi waliposikia yale Wafilisti walichomfanyia Sauli,
12 Then they arose (as many as were strong men) and went all night, and tooke the body of Saul, and the bodies of his sonnes, from the wall of Beth-shan, and came to Iabesh, and burnt them there,
mashujaa wao wote wakaenda usiku hadi Beth-Shani. Wakauchukua mwili wa Sauli na miili ya wanawe kutoka kwenye ukuta wa Beth-Shani na kurudi hadi Yabeshi, mahali ambapo waliiteketeza kwa moto.
13 And tooke their bones and buried them vnder a tree at Iabesh, and fasted seuen dayes.
Kisha wakachukua mifupa yao na kuizika chini ya mti wa mkwaju huko Yabeshi, nao wakafunga siku saba.