< 1 Samuel 2 >

1 And Hannah prayed, and said, Mine heart reioyceth in the Lord, mine horne is exalted in the Lord: my mouth is enlarged ouer mine enemies, because I reioyce in thy saluation.
Hana aliomba akasema, “moyo wangu wamtukuza BWANA. Pembe yangu imejulikana katika BWANA. Kinywa changu kinatamba dhidi ya maadui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
2 There is none holy as the Lord: yea, there is none besides thee, and there is no god like our God.
Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA, kwa kuwa hakuna mwingine zaidi yako; hakuna mwamba kama Mungu wetu.
3 Speake no more presumptuously: let not arrogancie come out of your mouth: for the Lord is a God of knowledge, and by him enterprises are established.
Msijivune sana hivyo kwa kiburi; vinywa vyenu visitoke majivuno. Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa; yeye huyapima matendo kwa mizani.
4 The bow and the mightie men are broken, and the weake haue girded themselues with strength.
Pinde za mashujaa zimevunjika, bali wale wanaojikwaa hujivika nguvu kama mshipi.
5 They that were full, are hired foorth for bread, and the hungrie are no more hired, so that the barren hath borne seuen: and shee that had many children, is feeble.
Wale walio na shibe ya kutosha wamejikodisha ili wapate chakula; wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Hata yule aliye kuwa tasa amezaa watoto saba, bali mwanamke mwenye watoto wengi amenyong'onyea.
6 The Lord killeth and maketh aliue: bringeth downe to the graue and raiseth vp. (Sheol h7585)
BWANA huua na huuisha. Hushusha kuzimu na huleta tena juu. (Sheol h7585)
7 The Lord maketh poore and maketh rich: bringeth lowe, and exalteth.
BWANA humfanya maskini, na yeye ndiye humtajirisha mtu. Yeye hudhili, lakini pia hukweza
8 He raiseth vp ye poore out of the dust, and lifteth vp the begger from the dunghill, to set them among princes, and to make them inherite the seate of glory: for the pillars of the earth are the Lordes, and he hath set the world vpon them.
Yeye humwinua juu maskini toka mavumbini: Huwainua wahitaji toka jalalani na kuwaketisha pamoja na wakuu na kuwarithisha kiti cha enzi cha utukufu. Kwa kuwa nguzo za dunia ni za BWANA na ameukalisha ulimwengu juu yake.
9 Hee will keepe the feete of his Saintes, and the wicked shall keepe silence in darkenes: for in his owne might shall no man be strong.
Yeye atazilinda nyayo za watu wake waaminifu, bali waovu watanyamazishwa gizani, kwa maana hakuna atayeshinda kwa nguvu zake.
10 The Lordes aduersaries shall be destroyed, and out of heauen shall he thunder vpon them: the Lord shall iudge the endes of the worlde, and shall giue power vnto his King, and exalt the horne of his Anoynted.
Wale wampingao BWANA watavunjwa vipande vipande; atawapiga radi kutokea mbinguni. BWANA atahukumu miisho ya dunia; atampa nguvu mfalme wake na kuinua pembe ya mtiwa mafuta wake.”
11 And Elkanah went to Ramah to his house, and the childe did minister vnto the Lord before Eli the Priest.
Nndipo Elikana akenda Rama, nyumbani kwake. Na yule mtoto akamtumikia BWANA machoni pa Eli, kuhani.
12 Now the sonnes of Eli were wicked men, and knewe not the Lord.
Basi, watoto wa Eli walikuwa wakorofi. Wao hawakumheshimu BWANA.
13 For the Priestes custome towarde the people was this: when any man offered sacrifice, the Priestes boy came, while the flesh was seething, and a fleshhooke with three teeth, in his hand,
Desturi ya makuhani na watu ilikuwa kwamba endapo mtu yeyote ametoa dhabihu, mtumishi wa kuhani angekuja akiwa na uma wa meno matatu mkononi mwake, nyama ilipokuwa inatokoswa.
14 And thrust it into the kettle, or into the caldron, or into the panne, or into the potte: all that the fleshhooke brought vp, the Priest tooke for himselfe: thus they did vnto all the Israelites, that came thither to Shiloh.
Naye angeutia uma huo sufuriani, au birikani au chomboni au chunguni; nyama yote ambayo ingeinuliwa na uma huo ingetwaliwa na kuhani mwenyewe. Ndivyo walivyofanya huko Shilo kwa Waisraeli wote waliokwenda huko.
15 Yea, before they burnt the fat, the priests boy came and saide to the man that offered, Giue me flesh to rost for the priest: for he wil not haue sodden flesh of thee, but rawe.
Tena, kabla ya kuteketeza mafuta, mtumishi wa kuhani alikuja, na kumwambia aliyekuwa akitoa dhabihu, “Tenga nyama ya kuchoma kwa ajili ya kuhani; kwa sababu hataikubali ile ya kutokosa kutoka kwako, bali tu ile mbichi.”
16 And if any man saide vnto him, Let them burne the fatte according to the custome, then take as much as thine heart desireth: then hee would answere, No, but thou shalt giue it nowe: and if thou wilt not, I will take it by force.
Ikiwa mtu atamwambia, “Wachome mafuta kwanza, na kisha uchukue kiasi utakacho.” Ndipo angesema, “Hapana, utanipatia sasa hivi; la sivyo; Nitaichukua kwa lazima.”
17 Therefore the sinne of the yong men was very great before the Lord: for men abhorred the offering of the Lord.
Dhambi ya vijana hawa ilikuwa mbaya sana mbele za BWANA, kwa sababu waliidharau dhabihu ya BWANA.
18 Now Samuel being a yong childe ministred before the Lord, girded with a linen Ephod.
Lakini Samweli alimtumikia BWANA akiwa mdogo akivaa nguo ya naivera ya kitani.
19 And his mother made him a litle coat, and brought it to him from yeere to yeere, when she came vp with her husband, to offer the yerely sacrifice.
Kila mwaka mama yake alimtengenezea kanzu dogo na kumletea, wakati wakija na mmewe kutoa dhabihu ya kila mwaka.
20 And Eli blessed Elkanah and his wife, and said, The Lord giue thee seede of this woman, for the petition that she asked of the Lord: and they departed vnto their place.
Eli aliwabariki Elikana na mke wake na kusema, “BWANA akupatie watoto zaidi kwa mwanamke huyu kwa sababu ya ahadi yake aliyoitoa kwa BWANA.” Baadaye walirudi nyumbani kwao.
21 And the Lord visited Hannah, so that she conceiued, and bare three sonnes, and two daughters. And the childe Samuel grewe before the Lord.
BWANA alimsaidia tena Hana, akawa amebeba mimba nyingine. Akazaa watoto watatu wa kiume na wa kike wawili. Wakati huo huo mtoto Samweli akakua akiwa mbele za BWANA.
22 So Eli was very olde, and heard all that his sonnes did vnto all Israel, and howe they laye with the women that assembled at the doore of the tabernacle of the Congregation.
Basi Eli alikuwa mzee sana, akayasikia yote ambayo watoto wake walikuwa wakiwafanyia Waisraeli wote, na jinsi walivyotembea na mwanamke aliyekuwa akitumika katika lango la hema ya kukutania.
23 And hee saide vnto them, Why doe ye such things? for of all this people I heare euill reportes of you.
Akawaambia, “Kwa nini mnafanya mambo hayo? Kwa maana nasikia matendo yenu maovu kutoka kwa watu hawa wote.”
24 Do no more, my sonnes, for it is no good report that I heare, which is, that ye make the Lords people to trespasse.
Sivyo hivyo, watoto wangu, maana hii ninayoisikia siyo taarifa njema. Mnawakosesha watu wa BWANA.
25 If one man sinne against another, the Iudge shall iudge it: but if a man sinne against the Lord, who will pleade for him? Notwithstanding they obeyed not the voyce of their father, because the Lord would slay them.
“Kama mtu mmoja akimkosea mwenzake, Mungu atamhukumu; Lakini mtu akimkosea BWANA, ni nani atakayemtetea mtu huyo?” Lakini hawakuitii sauti ya baba yao, sababu BWANA alinuia kuwaua.
26 (Nowe the childe Samuel profited and grewe, and was in fauour both with the Lord and also with men)
Yule mtoto Samweli aliongezeka umri, na kupata kibali kwa BWANA na kwa watu pia.
27 And there came a man of God vnto Eli, and said vnto him, Thus saith the Lord, Did not I plainely appeare vnto the house of thy father, when they were in Egypt in Pharaohs house?
Kisha mtu wa Mungu akamwendea Eli na kumwambia, “BWANA asema, 'Je, sikujifunua mwenyewe kwa nyumba ya baba zako, walipokuwa Misri utumwani nyumbani mwa Farao?
28 And I chose him out of all the tribes of Israel to be my Priest, to offer vpon mine altar, and to burne incense, and to weare an Ephod before me, and I gaue vnto the house of thy father all the offrings made by fire of the children of Israel.
Mimi nilimchagua yeye kutoka makabila yote ya Israeli awe kuhani wangu, apande madhabahuni kwangu, na kufukiza uvumba, na kuvaa kanzu ya naivera mbele yangu. Niliwapa nyumba ya baba zako dhabihu zote za wana wa Israeli zilizotolewa kwa moto.
29 Wherefore haue you kicked against my sacrifice and mine offering, which I commanded in my Tabernacle, and honourest thy children aboue mee, to make your selues fatte of the first fruites of all the offerings of Israel my people?
Kwanini basi, unaidharau dhabihu yangu na sadaka ambazo ninazitaka mahali ninapoishi? Kwanini unawaheshimu watoto wako kuliko mimi, kwa kujinenepesha ninyi wenyewe kwa uzuri wa kila sadaka ya watu wangu Israeli?'
30 Wherefore the Lord God of Israel saith, I saide, that thine house and the house of thy father should walke before mee for euer: but nowe the Lord saith, It shall not be so: for them that honour me, I will honour, and they that despise me, shall be despised.
Maana, BWANA, Mungu wa Isareli, asema, niliahidi kwamba nyumba yako, na nyumba ya baba yako, yawapasa kwenda mbele zangu milele,' Lakini sasa BWANA asema. 'Mambo haya yapishe mbali. nami nisifanye hivi, maana nitawaheshimu wanaoniheshimu, bali wanaonidharau mimi hawatakuwa na thamani.
31 Beholde, the dayes come, that I will cut off thine arme, and the arme of thy fathers house, that there shall not be an olde man in thine house.
Tazama, siku zinakuja nitakapoondoa nguvu zako na nguvu za nyumba za baba yako, ili kwamba pasije kuwepo mtu mzee katika nyumba yako.
32 And thou shalt see thine enemie in the habitation of the Lord in all thinges wherewith God shall blesse Israel, and there shall not be an olde man in thine house for euer.
Nawe utalitazama hangaiko katika makao yangu. Ingawa Israeli watapewa jambo jema, hapatakuwapo tena mtu yeyote mzee katika nyumba yako.
33 Neuerthelesse, I will not destroy euery one of thine from mine altar, to make thine eyes to faile, and to make thine heart sorowfull: and all ye multitude of thine house shall die when they be men.
Yeyote miongoni mwenu nisiye mwondoa kutoka madhabahuni pangu, Nitasababisha macho yenu yaanguke, na ita nitasababisha huzuni maishani mwenu. Wanaume wote waliozaliwa katika familia yako watakufa.
34 And this shalbe a signe vnto thee, that shall come vpon thy two sonnes Hophni and Phinehas: in one day they shall die both.
Hii ndiyo itakuwa ishara kwako ambayo itawaijia watoto wako wakiume wawili, juu ya Hofni na Finehasi: Wote wawili watakufa siku moja.
35 And I will stirre me vp a faithfull Priest, that shall do according to mine heart and according to my minde: and I wil build him a sure house, and he shall walke before mine Anointed for euer.
Nami nitamwinua juu kuhani wangu mwaminifu atakaye fanya kile kilichomo moyoni mwangu na nafisini mwangu. Nami nitamjengea nyumba madhubuti; naye atakwenda mbele ya mfalme wangu mbarikiwa milele.
36 And all that are left in thine house, shall come and bowe downe to him for a piece of siluer and a morsell of bread, and shall say, Appoint me, I pray thee, to one of the priestes offices, that I may eate a morsell of bread.
Kila mmoja aliyebakia nyumbani mwako atakuja na kusujudu mbele ya mtu huyo, akiomba kipande cha fedha na mkate mmoja, naye atasema, “Tafadhali uniajiri katika moja ya nafasi za kuhani ili niweze kula kipande cha mkate'”'

< 1 Samuel 2 >