< 1 Peter 2 >
1 Wherefore, laying aside all maliciousnes, and all guile, and dissimulation, and enuie, and all euill speaking,
Basi, acheni uovu wote; uongo, unafiki, wivu na maneno ya kashfa visiweko tena.
2 As newe borne babes desire that sincere milke of the woorde, that yee may growe thereby,
Kama vile watoto wachanga wanavyotamani maziwa, nanyi pia mnapaswa kuwa na hamu ya maziwa halisi ya kiroho, ili kwa nguvu yake mpate kukua na kukombolewa.
3 Because yee haue tasted that the Lord is bountifull.
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mmegundua kwamba Bwana ni mwema.”
4 To whome comming as vnto a liuing stone disallowed of men, but chosen of God and precious,
Basi, mwendeeni Bwana! Yeye ndiye jiwe hai lililokataliwa na watu; lakini mbele ya Mungu ni jiwe teule, na la thamani kubwa.
5 Yee also as liuely stones, bee made a spirituall house, an holy Priesthoode to offer vp spirituall sacrifices acceptable to God by Iesus Christ.
Mwendeeni yeye kama mawe hai mkajengeke na kuwa nyumba ya kiroho, ambamo mtatumikia kama makuhani watakatifu, kutolea dhabihu za kiroho zenye kumpendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.
6 Wherefore also it is conteyned in the Scripture, Beholde, I put in Sion a chiefe corner stone, elect and precious: and hee that beleeueth therein, shall not be ashamed.
Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Tazama! Naweka huko sioni jiwe kuu la msingi, jiwe la thamani kubwa nililoliteua. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa.”
7 Vnto you therefore which beleeue, it is precious: but vnto them which be disobedient, the stone which the builders disallowed, the same is made the head of the corner,
Kwenu ninyi mnaoamini, jiwe hilo ni la thamani kubwa; lakini kwa wale wasioamini, “Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi.”
8 And a stone to stumble at, and a rocke of offence, euen to them which stumble at the woorde, being disobedient, vnto the which thing they were euen ordeined.
Tena Maandiko yasema: “Jiwe hilo ni jiwe la kujikwaa, mwamba wa kuwaangusha watu.” Watu hujikwaa kwa sababu hawauamini ule ujumbe; na ndivyo walivyopangiwa tangu mwanzo.
9 But yee are a chosen generation, a royall Priesthoode, an holy nation, a people set at libertie, that yee shoulde shewe foorth the vertues of him that hath called you out of darkenesse into his marueilous light,
Lakini ninyi ni ukoo mteule, makuhani wa Mfalme, taifa takatifu; watu wake Mungu mwenyewe, mlioteuliwa kutangaza matendo makuu ya Mungu aliyewaiteni kutoka gizani akawaingizeni katika mwanga wake mkuu.
10 Which in time past were not a people, yet are nowe the people of God: which in time past were not vnder mercie, but nowe haue obteined mercie.
Wakati mmoja ninyi hamkuwa watu wa Mungu, lakini sasa ninyi ni watu wake; wakati mmoja hamkupewa huruma ya Mungu, lakini sasa mmeipokea.
11 Dearely beloued, I beseeche you, as strangers and pilgrims, abstaine from fleshly lusts, which fight against the soule,
Wapenzi wangu, nawasihi ninyi kama wageni na wakimbizi hapa duniani! Achaneni na tamaa za mwili ambazo hupingana na roho.
12 And haue your conuersation honest among the Gentiles, that they which speake euill of you as of euill doers, may by your good woorkes which they shall see, glorifie God in the day of visitation.
Mwenendo wenu kati ya watu wasiomjua Mungu unapaswa kuwa mwema kabisa, ili hata watakapowasingizieni kwamba mnatenda mabaya, waweze kutambua matendo yenu mema na hivyo wamtukuze Mungu Siku ya kuja kwake.
13 Therefore submit your selues vnto all maner ordinance of man for the Lordes sake, whether it be vnto the King, as vnto the superiour,
Basi, jiwekeni chini ya mamlaka yote ya kibinadamu, kwa ajili ya Bwana: utii kwa mfalme aliye mtawala mkuu,
14 Or vnto gouernours, as vnto them that are sent of him, for the punishment of euill doers, and for the praise of them that doe well.
utii kwa wakuu wa mikoa ambao wameteuliwa naye kuwaadhibu wahalifu na kuwasifu watendao mema.
15 For so is the will of God, that by well doing ye may put to silence the ignorance of the foolish men,
Maana Mungu anataka mweze kuyakomesha maneno ya kijinga ya watu wasio na akili kwa matendo mema mnayofanya.
16 As free, and not as hauing the libertie for a cloke of maliciousnesse, but as the seruauntes of God.
Ishini kama watu huru; lakini msiutumie uhuru wenu kuuficha ubaya, bali ishini kama watumishi wa Mungu.
17 Honour all men: loue brotherly fellowship: feare God: honour the King.
Waheshimuni watu wote, wapendeni ndugu zenu waumini, mcheni Mungu, mheshimuni mfalme.
18 Seruaunts, be subiect to your masters with all feare, not onely to the good and courteous, but also to the froward.
Enyi watumishi wa nyumbani, watiini wakuu wenu kwa heshima yote, wawe wema na wapole au wenye kuchukiza.
19 For this is thanke worthie, if a man for conscience toward God endure griefe, suffering wrongfully.
Maana kama mnavumilia maumivu ya mateso msiyostahili kwa sababu mwajua kwamba Mungu anataka hivyo, basi Mungu atawafadhili.
20 For what praise is it, if when ye be buffeted for your faultes, yee take it paciently? but and if when ye doe well, ye suffer wrong and take it paciently, this is acceptable to God.
Maana, mtapata tuzo gani mkivumilia mapigo mnayostahili kwa sababu ya makosa yenu? Lakini kama mnavumilia mateso hata ingawa mmetenda mema, Mungu atawapeni baraka kwa ajili hiyo.
21 For hereunto ye are called: for Christ also suffred for you, leauing you an ensample that ye should follow his steppes.
Hayo ndiyo mliyoitiwa; maana Kristo mwenyewe aliteseka kwa ajili yenu, akawaachieni mfano, ili muufuate mwenendo wake.
22 Who did no sinne, neither was there guile found in his mouth.
Yeye hakutenda dhambi, wala neno la udanganyifu halikusikika mdomoni mwake.
23 Who when hee was reuiled, reuiled not againe: when hee suffered, hee threatned not, but comitted it to him that iudgeth righteously.
Alipotukanwa yeye hakujibu kwa tukano; alipoteseka yeye hakutoa vitisho, bali aliyaweka matumaini yake kwa Mungu, hakimu mwenye haki.
24 Who his owne selfe bare our sinnes in his body on the tree, that we being dead to sinne, should liue in righteousnesse: by whose stripes ye were healed.
Yeye mwenyewe alizibeba dhambi zetu katika mwili wake juu ya msalaba, tupate kufa kuhusu dhambi, na kuishi kwa ajili ya uadilifu. Kwa majeraha yake, ninyi mmeponywa.
25 For ye were as sheepe going astray: but are nowe returned vnto the shepheard and Bishop of your soules.
Ninyi mlikuwa kama kondoo waliokuwa wamepotea; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mlinzi wa roho zenu.