< 1 Kings 5 >

1 And Hiram King of Tyrus sent his seruants vnto Salomon, (for he had heard, that they had anoynted him King in the roume of his father) because Hiram had euer loued Dauid.
Hiramu mfalme wa Tiro aliposikia kuwa Solomoni ametiwa mafuta awe mfalme mahali pa Daudi baba yake, akatuma wajumbe kwa Solomoni, kwa sababu Hiramu siku zote alikuwa na uhusiano mzuri wa kirafiki na Daudi.
2 Also Salomon sent to Hiram, saying,
Solomoni akapeleka ujumbe huu kwa Hiramu:
3 Thou knowest that Dauid my father could not build an house vnto the Name of the Lord his God, for the warres which were about him on euery side, vntill the Lord had put them vnder the soles of his feete.
“Unajua kwamba kwa sababu ya vita vilivyopiganwa dhidi ya baba yangu Daudi kutoka pande zote, hakuweza kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana Mungu wake, hadi Bwana alipowaweka adui zake chini ya miguu yake.
4 But now the Lord my God hath giuen me rest on euery side, so that there is neither aduersarie, nor euill to resist.
Lakini sasa Bwana Mungu wangu amenipa utulivu kila upande hakuna adui wala maafa.
5 And beholde, I purpose to build an house vnto ye Name of the Lord my God, as the Lord spake vnto Dauid my father, saying, Thy sonne, whom I wil set vpon thy throne for thee, he shall build an house vnto my Name.
Kwa hiyo, ninakusudia kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wangu, kama Bwana alivyomwambia baba yangu Daudi, wakati aliposema, ‘Mwanao nitakayemweka kwenye kiti cha ufalme mahali pako, ndiye atajenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
6 Now therefore commaund, that they hewe me cedar trees out of Lebanon, and my seruants shall be with thy seruants, and vnto thee will I giue the hire for thy seruants, according to all that thou shalt appoynt: for thou knowest that there are none among vs, that can hewe timber like vnto the Sidonians.
“Hivyo toa amri ili mierezi ya Lebanoni ikatwe kwa ajili yangu. Watu wangu watafanya kazi na watu wako, nami nitawalipa watu wako kwa ujira wowote utakaoupanga. Unajua kwamba hatuna mtu yeyote mwenye ustadi katika kukata miti kama Wasidoni.”
7 And when Hiram heard the wordes of Salomon, he reioyced greatly, and sayde, Blessed be the Lord this day, which hath giuen vnto Dauid a wise sonne ouer this mightie people.
Hiramu aliposikia ujumbe wa Solomoni, akafurahishwa sana akasema, “Ahimidiwe Bwana leo, kwa kuwa amempa Daudi mwana mwenye hekima kutawala juu ya taifa hili kubwa.”
8 And Hiram sent to Salomon, saying, I haue considered the things, for the which thou sentest vnto me, and will accomplish all thy desire, concerning the cedar trees and firre trees.
Hiramu akatuma neno kwa Solomoni: “Nimepokea ujumbe ulionipelekea na nitafanya yote unayohitaji katika kukupatia magogo ya mierezi na misunobari.
9 My seruants shall bring them downe from Lebanon to the sea: and I will conuey them by sea in raftes vnto the place that thou shalt shew me, and wil cause them to be discharged there, and thou shalt receiue them: nowe thou shalt doe mee a pleasure to minister foode for my familie.
Watu wangu watayakokota kutoka Lebanoni hadi kwenye bahari, nami nitayafunga mafungu mafungu yaelee juu ya maji hadi utakapoelekeza. Huko nitayatenganisha, nawe utaweza kuyachukua. Wewe utakidhi haja yangu kwa kunipatia chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwangu.”
10 So Hiram gaue Salomon cedar trees and firre trees, euen his full desire.
Kwa njia hii Hiramu akampa Solomoni miti yote ya mierezi na magogo ya misunobari kama alivyohitaji,
11 And Salomon gaue Hiram twentie thousand measures of wheate for foode to his householde, and twentie measures of beaten oyle. Thus much gaue Salomon to Hiram yere by yere.
naye Solomoni akampa Hiramu kori 20,000 za ngano kama chakula kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, pamoja na mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa bathi 20,000. Solomoni aliendelea kumfanyia Hiramu hivyo mwaka baada ya mwaka.
12 And the Lord gaue Salomon wisedome as he promised him. And there was peace betweene Hiram and Salomon, and they two made a couenant.
Bwana akampa Solomoni hekima, kama alivyomwahidi. Palikuwepo na uhusiano wa amani kati ya Hiramu na Solomoni, na wote wawili wakafanya mkataba.
13 And King Salomon raised a summe out of all Israel, and the summe was thirtie thousand men:
Mfalme Solomoni akakusanya wafanyakazi 30,000 kutoka Israeli yote.
14 Whome he sent to Lebanon, ten thousand a moneth by course: they were a moneth in Lebanon, and two moneths at home. And Adoniram was ouer the summe.
Akawapeleka Lebanoni kwa zamu za watu 10,000 kwa mwezi, hivyo walikaa Lebanoni kwa mwezi mmoja na miezi miwili nyumbani. Adoniramu ndiye alikuwa kiongozi wa shokoa.
15 And Salomon had seuentie thousand that bare burdens, and fourescore thousand masons in the mountaine,
Solomoni alikuwa na wachukuzi wa mizigo 70,000 na wachonga mawe 80,000 huko vilimani,
16 Besides the princes, whome Salomon appoynted ouer the worke, euen three thousande and three hundreth, which ruled the people that wrought in the worke.
pamoja na wasimamizi 3,300 ambao walisimamia kazi hiyo na kuwaongoza wafanyakazi.
17 And the King commanded them, and they brought great stones and costly stones to make the foundation of the house, euen hewed stones.
Kwa amri ya mfalme walitoa kwenye machimbo ya mawe, mawe makubwa, yaliyo bora kwa kujengea msingi wa nyumba yaliyochongwa kwa ajili ya Hekalu.
18 And Salomons workemen, and the workemen of Hiram, and the masons hewed and prepared timber and stones for the buylding of the house.
Mafundi wa Solomoni, wa Hiramu na watu wa Gebali walikata na kuandaa mbao na mawe kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.

< 1 Kings 5 >