< 1 Kings 19 >
1 Now Ahab tolde Iezebel all that Eliiah had done, and how he had slaine all the prophets with the sword.
Ahabu akamwambia Yezebeli mambo yote ambayo Eliya amefanya na jinsi alivyowaua manabii wote kwa upanga.
2 Then Iezebel sent a messenger vnto Eliiah, saying, The gods doe so to me and more also, if I make not thy life like one of their liues by to morowe this time.
Ndipo Yezebeli alipotuma mjumbe kwa Eliya, akisema, “miungu wanifanye hivyo na mimi, na zaidi yake, kama kesho muda kama huu sitayafanya maisha yako kuwa kama mmoja wa hao manabii waliokufa.”
3 When he sawe that, he arose, and went for his life, and came to Beer-sheba, which is in Iudah, and left his seruant there.
Eliya aliposikia hayo, akaiinuka na akakimbia kwa ajili ya kuokoa maisha yake akaja mpaka Beerisheba, ambao ni mji wa Yuda, na akamwacha mtumishi wake huko.
4 But he went a dayes iourney into the wildernesse, and came and sate downe vnder a iuniper tree, and desired that he might die, and sayde, It is now ynough: O Lord, take my soule, for I am no better then my fathers.
Lakini yeye mwenyewe akaenda mwendo wa siku moja huko jangwani, akaja akakaa chini ya mti wa mretemu. Akajiombea mwenyewe kufa, akasema, “Sasa yatosha, BWANA, ichukue roho yangu, kwa kuwa mimi si mzuri kuliko mababu zangu waliokufa.”
5 And as he lay and slept vnder the iuniper tree, behold now, an Angel touched him, and said vnto him, Vp, and eate.
Kwa hiyo akalala chini ya mretemu. Ghafula malaika akamgusa na akamwambia, “Inuka ule.”
6 And when he looked about, behold, there was a cake baken on the coles, and a pot of water at his head: so he did eate and drinke, and returned and slept.
Eliya akatazama, karibu na kichwa chake kulikuwa na mkate uliokuwa umeokwa kwa mkaa na gudulia la maji. Kwa hiyo akala na kunywa na kulala tena.
7 And the Angel of the Lord came againe the second time, and touched him, and sayd, Vp, and eate: for thou hast a great iourney.
Malaika wa BWANA akaja tena mara ya pili akamgusa na kumwambia, “Inuka ule, kwa sababu safari bado ndefu kwako.”
8 Then he arose, and did eate and drinke, and walked in the strength of that meate fourtie dayes and fourtie nights, vnto Horeb the mount of God.
Kwa hiyo akainuka na kula na kunywa, naye akasafiri kwa nguvu ya chakula hicho kwa siku arobaini mchana na usiku hata akafika Horebu, mlima wa Mungu.
9 And there he entred into a caue, and lodged there: and beholde, the Lord spake to him, and said vnto him, What doest thou here, Eliiah?
Akaingia kwenye pango akakaa humo. Kisha neno la BWANA likamjia likimwambia, “Unafanya nini hapa, Eliya?”
10 And he answered, I haue bene very ielous for the Lord God of hostes: for the children of Israel haue forsaken thy couenant, broken downe thine altars, and slayne thy Prophets with the sword, and I onely am left, and they seeke my life to take it away.
Eliya akajibu, “Nimeona wivu mwingi kwa BWANA, Mungu wa majeshi, kwa kuwa watu wa Israeli wameliacha agano lako, wameziharibu madhabahu zako, na wamewaua manabii wako kwa upanga. Sasa ni mimi, pekee yangu, nimebaki na wanataka kuichukua roho yangu.
11 And he saide, Come out, and stand vpon the mount before the Lord. And beholde, the Lord went by, and a mightie strong winde rent the mountaines, and brake the rockes before the Lord: but the Lord was not in the winde: and after the wind came an earthquake: but the Lord was not in the earthquake:
BWANA akamwambia, “Nenda nje ukasimame kwenye mlima mbele yangu.” Kisha BWANA akapita, na upepo mkali ukaupiga mlima ukavunja miamba katika vipande vipande mbele ya BWANA, lakini BWANA hakuwemo kwenye huo mlima. Kisha baada ya upepo, tetemeko lakaja, lakini BWANA hakuwemo kwenye hilo tetemeko.
12 And after the earthquake came fire: but the Lord was not in the fire: and after the fire came a still and soft voyce.
Kisha baada ya tetemeko, moto ukaja, lakini BWANA hakuwemo kwenye moto. Ndipo baada ya moto, sauti ya upole ikaja.
13 And when Eliiah heard it, he couered his face with his mantel, and went out, and stoode in the entring in of ye caue: and behold, there came a voyce vnto him, and sayd, What doest thou here, Eliiah?
Naye Eliya alipoisikia sauti, akafunika uso wake kwa vazi lake, akatoka nje, akasimama kwenye lango la hilo pango. Na sauti ikaja kwake ikisema, “unafanya nini hapa?,
14 And he answered, I haue bene very ielous for the Lord God of hostes, because the children of Israel haue forsaken thy couenant, cast downe thine altars, and slayne thy Prophets with the sworde, and I onely am left, and they seeke my life to take it away.
Eliya akajibu, “nimeona wivu sana kwa ajili ya BWANA, Muungu wa majeshi, kwa kuwa watu wa Israeli wameliacha agano lako, wamezihariibu madhabahu zako, na wamewaua manabii kwa upanga. Sasa, ni mimi pekee yangu, nimebaki na wanajaribu kuichukua roho yangu.”
15 And the Lord said vnto him, Goe, returne by the wildernes vnto Damascus, and when thou commest there, anoint Hazael King ouer Aram.
Kisha BWANA akamwambia, “Nenda, rudi kwa njia yako kwenye jangwa la Dameski, na utakapofika utamtia mafuta Hazaeli awe Mfalme wa Shamu,
16 And Iehu the sonne of Nimshi shalt thou anoynt King ouer Israel: and Elisha the sonne of Shaphat of Abel Meholah shalt thou anoynt to be Prophet in thy roume.
na utamtia mafuta Yehu mwana wa Nimshi kuwa mfalme wa Israeli, na utamtia mafuta Elisha mwana wa Shafeti wa Abeli Mehola kuwa nabii mahali pako.
17 And him that escapeth from the sworde of Hazael, shall Iehu slay: and him that escapeth from the sword of Iehu, shall Elisha slay.
Itakuwa hivi Yehu atamwua kila mmoja atakayejaribu kutoroka upanga wa Hazaeli, na kwamba Elisha atamwua kila atakayejaribu kukwepa upanga wa Yehu.
18 Yet wil I leaue seuen thousand in Israel, euen all the knees that haue not bowed vnto Baal, and euery mouth that hath not kissed him.
Lakini nitawaacha watu elfu saba katika Israeli kwa ajili yangu, ambao magoti yao hayajawahi kupigwa kwa Baali, na ambao midomo yao haijambusu.”
19 So he departed thence, and found Elisha the sonne of Shaphat who was plowing with twelue yoke of oxen before him, and was with the twelft: and Eliiah went towards him, and cast his mantel vpon him.
Kwa hiyo Eliya akaondoka mahali pale na akamkuta Elisha mwana wa Shafati, akilima na jozi za makisai kumi na mbili mbele yake, na yeye mwenyewe alikuwa akilima na ile jozi ya kumi na mbili. Eliya akaenda mpaka kwa Elisha akamtupia vazi lake juu yake.
20 And he left the oxen, and ran after Eliiah, and sayde, Let mee, I pray thee, kisse my father and my mother, and then I wil follow thee. Who answered him, Go, returne: for what haue I done to thee?
Elisha naye akawaacha wale makisai akamkimbilia Eliya; akamwambia, “Tafadhali naomba nikambusu baba yangu na mama yangu kisha nitakufuata.” Naye Eliya akamwambia, “Rudi, lakini fikiria juu ya kile nilichokufanyia.”
21 And when he went backe againe from him, he tooke a couple of oxen, and slewe them, and sod their flesh with the instruments of the oxen, and gaue vnto the people, and they did eate: then he arose and went after Eliiah, and ministred vnto him.
Kwa hiyo Elisha akarudi toka kwa Eliya na akachukua ile jozi ya makisai, akawaua wale wanyama, na akapika ile nyama kwa kuni za ile nira. Kisha akawapa watu wakala. Kisha akaamka, akamfuata Eliya akamtumikia.