< 1 Kings 14 >

1 At that time Abiiah the sonne of Ieroboam fell sicke.
Wakati huo Abiya mwana wa Yeroboamu akawa mgonjwa sana.
2 And Ieroboam saide vnto his wife, Vp, I pray thee, and disguise thy selfe, that they know not that thou art the wife of Ieroboam, and goe to Shiloh: for there is Ahiiah the Prophet, which tolde mee that I shoulde bee King ouer this people,
Yeroboamu akamwambia mke wake, “amka ujibadilishe, ili wasikutambue kuwa wewe ndiye mke wangu, na uende Shilo, kwa sababu nabii Ahiya yuko huko, yeye ndiye aliyeninea mimi kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
3 And take with thee tenne loaues and craknels, and a bottell of honie, and go to him: hee shall tell thee what shall become of the yong man.
Uchukue mikate kumi, na kaki na mtungi wa asali, na uende kwa Ahiya. Naye atakuambia kitakachotokea kwa mtoto.”
4 And Ieroboams wife did so, and arose, and went to Shiloh, and came to the house of Ahiiah: but Ahiiah could not see, for his sight was decayed for his age.
Mke wa Yeroboamu akafanya hivyo; akaenda Shilo mpaka kwenye nyumba ya Ahiya. Wakati huo Ahiya alikuwa hawezi kuona, kwa kuwa macho yake yalikuwa yameishiwa nguvu kwa sababu ya umri wake.
5 Then the Lord saide vnto Ahiiah, Beholde, the wife of Ieroboam commeth to aske a thing of thee for her sonne, for he is sicke: thus and thus shalt thou say vnto her: for when shee commeth in, shee shall feine her selfe to be another.
BWANA akamwambia Ahiya, “Tazama mke wa Ahiya anakuja kutafuta kutaka ushauri toka kwako kuhusiana na mwanae, kwa kuwa ni mgonjwa. Mwambie hivi na hivi, kwa sababu atakapofika atajifanya kuwa ni mwanamke mwingine.”
6 Therefore when Ahiiah heard the sounde of her feete as shee came in at the doore, hee saide, Come in, thou wife of Ieroboam: why feinest thou thus thy selfe to bee an other? I am sent to thee with heauie tidings.
Naye Ahiya aliposikia sauti za miguu yake alipokuwa akiukaribia mlango, akasema, “karibu, mke wa Yeroboamu. Kwa nini unajifanya kuwa mtu mwingine? Nimetumwa kwako nikiwa na habaari mbaya.
7 Goe, tel Ieroboam, Thus saith the Lord God of Israel, Forasmuch as I haue exalted thee from among the people, and haue made thee prince ouer my people Israel,
Nenda ukamwambia Yeroboamu kwamba BWANA, Mungu wa Israeli, anasema, 'Nilikuinua kutoka kati ya watu na kukufanya uwe kiongozi wa watu wangu Israeli.
8 And haue rent the kingdome away from the house of Dauid, and haue giuen it thee, and thou hast not bene as my seruant Dauid, which kept my commandements, and followed mee with all his heart, and did onely that which was right in mine eyes,
Niliugawa ufalme kutoka kwa Daudi na kukupa wewe, lakini bado hutaki kuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye alizishika amri zangu na kunifuata kwa moyo wake wote, na kufanya kilichokuwa sawa mbele ya macho yangu.
9 But hast done euil aboue al that were before thee (for thou hast gone and made thee other gods, and molten images, to prouoke me, and hast cast me behinde thy backe)
Badala yake, umefanya maovu, zaidi ya wote waliokutangulia. Umetengeneza miungu mingine, na umetengeneza sanamu za kuyeyushwa ili kunikasirisha na kunitupa nyuma yako.
10 Therefore beholde, I will bring euill vpon the house of Ieroboam, and will cut off from Ieroboam him that pisseth against the wall, aswell him that is shut vp, as him that is left in Israel, and will sweepe away the remnant of the house of Ieroboam, as a man sweepeth away doung, till it be all gone.
Kwa hiyo, tazama, Nitaleta majanga kwenye familia yako; Nitawatupilia mbali watoto wako wote wa kiume katika Israeli, kama ni mtumwa au ni huru, na nitaiondoa familia yako, kama mtu anayechoma mavi mpaka yaishe.
11 The dogges shall eate him of Ieroboams stocke that dyeth in the citie, and the foules of the aire shall eate him that dyeth in the fielde: for the Lord hath said it.
Yeyote ambaye ni mwanafamilia yako atakayefia mjini ataliwa na mbwa, na yeyote atakayefia shamabani ataliwa na ndege wa angani, kwa kuwa Mimi BWANA, nimesema;
12 Vp therefore and get thee to thine house: for when thy feete enter into the citie, the childe shall die.
Kwa hiyo inuka wewe mke wa Yeroboamu, na uende nyumbani kwako; na mguu wako utakapokanyaga mjini, yule mtoto wa Abiya atakufa.
13 And al Israel shall mourne for him, and burie him: for he onely of Ieroboam shall come to the graue, because in him there is found some goodnes towarde the Lord God of Israel in the house of Ieroboam.
Na Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Ni yeye pekee katika familia ya Abiya atakayepelekwa makaburini, kwa sababu ni yeye pekee yake kutoka kwenye nyumba ya Abiya, ambaye BWANA, Mungu wa Israeli alimwona kuwa ni mwema.
14 Moreouer, the Lord shall stirre him vp a King ouer Israel, which shall destroy the house of Ieroboam in that day: what? yea, euen nowe.
Pia BWANA atainua mfalme katika Israeli ambaye ataifutilia mbali familia ya Yeroboamu katika siku hiyo. Leo ndiyo siku hiyo, sasa hivi.
15 For the Lord shall smite Israel, as when a reede is shaken in the water, and hee shall weede Israel out of his good lad, which he gaue to their fathers, and shall scatter them beyond the Riuer, because they haue made them groues, prouoking the Lord to anger.
Kwa kuwa BWANA ataishambulia Israeli kama vile majani yanavyotikiswa majini, na ataing'oa Israeli katika nchi hii njema ambayo aliwpa mababu. Atawatawanya hata ng'ambo ya Mto Frati, kwa sababu wamefanya nguzo za Ashera kumkasirisha BWANA.
16 And he shall giue Israel vp, because of the sinnes of Ieroboam, who did sinne, and made Israel to sinne.
Ataiacha Israeli kwa sababu ya dhambi ya Yeroboamu, dhambi ambazo ametenda, na kwa hizo ameifanya Israeli kufanya dhambi.
17 And Ieroboams wife arose, and departed, and came to Tirzah, and when shee came to the threshold of the house, the yong man dyed,
Kwa hiyo mke wa Yeroboamu akainuka na akaondoka na akaenda mpaka Tirza. Naye alipofika kizingitini kwa nyumba yake, yule mtoto akafa.
18 And they buried him, and all Israel lamented him; according to the word of the Lord, which hee spake by the hand of his seruant Ahiiah the Prophet.
Isareli wote wakamzika na kumwombolezea, kama vile alivyokuwa ameambiwa kwa neno la BWANA ambalo amelisema kupitia mtumishi wake nabii Ahiya.
19 And the rest of Ieroboams actes, how hee warred, and howe hee reigned, beholde, they are written in the booke of the Chronicles of the Kings of Israel.
Na kwa mambo mengine yanayOmhusu Yeroboamu, jinsi alivyopigana vita na jinsi alivyotawala, tazama yameandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli.
20 And the dayes which Ieroboam reigned, were two and twentie yeere: and he slept with his fathers, and Nadab his sonne reigned in his steade.
Yeroboamu alitawala kwa miaka ishirini na mbili naye akalala na babu zake, na Nadabu mwanawe akawa mfalme mahali pake.
21 Also Rehoboam the sonne of Salomon reigned in Iudah. Rehoboam was one and fourtie yere olde, when he began to reigne, and reigned seuenteene yere in Ierusalem, the citie which the Lord did chuse out of al the tribes of Israel, to put his Name there: and his mothers name was Naamah an Ammonite.
Sasa Rehoboamu mwana wa Sulemani alikuwa mtawala wa Yuda. Rehoboamu alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipokuwa mfalme, na akatawala kwa miaka kumi na saba kule Yerusalemu, mji ambao BWANA alikuwa ameuchagua kati ya makabila yote ya Israeli ili aweke jina lake kule. Jina la mama yake alikuwa Naama Mwamori.
22 And Iudah wrought wickednesse in the sight of the Lord: and they prouoked him more with their sinnes, which they had committed, then all that which their fathers had done.
Yuda ikafanya yaliyo maovu mbele ya macho ya BWANA; wakamtia wivu kwa makosa yao, zaidi ya yote ambayo baba zao walikuwa wamefanya
23 For they also made them hie places, and images, and groues on euery hie hill, and vnder euery greene tree.
Kwa kuwa walijijengea wenyewe mahali pa juu, nguzo za mawe, na nguzo za Ashera katika kila mahali pa juu na katika kila mti wenye majani mabichi.
24 There were also Sodomites in the lande, they did according to all the abominations of the nations, which the Lord had cast out before the children of Israel.
Pia kulikuwepo na ukahaba wa kipagani katika nchi. Walifanya machukizo yaleyale kama wa mataifa yale ambayo BWANA alikuwa amewafukuza kutoka kwa watu wa Israeli.
25 And in the fift yere of King Rehoboam, Shishak King of Egypt came vp against Ierusale,
Ilitokea wakati wa mwaka wa tano wa mfalme Rehoboamu wakati Shishaki akiwa mfalme wa Misri, akaja kinyume na Yerusalemu.
26 And tooke the treasures of the house of the Lord, and the treasures of the Kings house, and tooke away all: also he caried away all the shields of golde which Salomon had made.
Akaichukua hazina iliyokuwa kwenye nyumba ya BWANA, na ile hazina iliyokuwa kwenye nyumba ya Mfalme. Akachukua kila kitu; Pia alizichukua zile ngao za dhahabu ambazo Sulemani alikuwa ametengeneza.
27 And King Rehoboam made for them brasen shieldes, and committed them vnto ye hands of the chiefe of the garde, which wayted at the doore of the Kings house.
Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba mahali pake na akazikabidhi kwa wakuu wa walinzi, ambao walilinda malango ya kuingia kwa mfalme.
28 And when the King went into the house of the Lord, the garde bare them, and brought them againe into the gard chamber.
Na ikawa kila mfalme alipoingia kwenye nyumba ya BWANA, wale walinzi walizibeba na baadaye walizirudisha katika chumba cha walinzi.
29 And the rest of the actes of Rehoboam, and all that hee did, are they not written in the booke of the Chronicles of the Kings of Iudah?
Lakini katika mambo mengine kuhusiana na Rehoboamu, na yote yale aliyofanya, je, hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
30 And there was warre betweene Rehoboam and Ieroboam continually.
Kulikuwa na mapigano yasiyokoma kati ya nyumba ya Rehoboamu na nyumba ya Yeroboamu.
31 And Rehoboam slept with his fathers, and was buried with his fathers in the citie of Dauid: his mothers name was Naamah an Ammonite. And Abiiam his sonne reigned in his stead.
Kwa hiyo Rehoboamu akalala na mababu zake naye akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi Jina la mama yake alikuwa Naama Mwamori. Abiya mwanawe akawa mfalme mahali pake

< 1 Kings 14 >