< 1 Kings 13 >

1 And beholde, there came a man of God out of Iudah (by the commandement of the Lord) vnto Beth-el, and Ieroboam stoode by the altar to offer incense.
Mtu wa Mungu alikuja tokea Yuda kwa neno la BWANA kule Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa amesimama karibu na madhabahu ili kufukiza uvumba.
2 And he cryed against the altar by the comandement of the Lord, and said, O altar, altar, thus saith the Lord, Beholde, a child shalbe borne vnto the house of Dauid, Iosiah by name, and vpon thee shall he sacrifice the Priestes of the hie places that burne incense vpon thee, and they shall burne mens bones vpon thee.
Akalia kinyume na zile madhabahu kwa neno la BWANA: “Ee madhabahu, madhabahu” hivi ndivyo asemavyo BWANA, 'Tazama, mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika familia ya Daudi, na juu yenu atawachinja makuhani ambao sasa wanafukiza uvumba mahali hapa pa juu kwa ajili yako. Juu yako watachoma mifupa ya watu.'”
3 And he gaue a signe the same time, saying, This is the signe, that the Lord hath spoken, Behold, the altar shall rent, and the ashes that are vpon it, shall fall out.
Kisha mtu wa Mungu akatoa ishara siku hiyohiyo, akisema, “Hii ndiyo isharaya kwamba BWANA amesema: 'Tazama, madhabahu zitavuunjika, na majivu yaliyo juu yatamwagika.”
4 And when the King had heard the saying of the man of God, which he had cryed against the altar in Beth-el, Ieroboam stretched out his hand from the altar, saying, Lay holde on him: but his hande which he put foorth against him, dryed vp, and he could not pull it in againe to him.
Naye mfalme aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, kwamba amelia kinyume cha zile madhabahu kule Betheli, Yeroboamu akanyosha mkono wake kutoka madhabahuni, akisema, “mkamateni.” Ndipo ule mkono aliokuwa ameunyosha dhidi ya mtu wa Mungu ukakauka, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha mwenyewe.
5 The altar also claue asunder, and the ashes fell out from the altar, according to the signe, which the man of God had giuen by the commandement of the Lord.
Na ile madhabahu ikavunjika vipande vipande, na yale majivu yakamwagika kutoka madhabahuni, kama ilivyokuwa imefafanuliwa kuwa ndiyo ishara ya kwamba mtu wa Mungu alikuwa amepewa kwa neno la BWANA.
6 Then the King answered, and saide vnto the man of God, I beseeche thee, pray vnto ye Lord thy God, and make intercession for me, that mine hand may bee restored vnto me. And the man of God besought the Lord, and the Kings hand was restored, and became as it was afore.
Mfalme Yeroboamu akajibu akimwambia mtu wa Mungu, “Msihi BWANA, Mungu wako akupe neema ili uniombee, ili kwamba mkono wangu urejee kwangu tena.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwomba BWANA, na mkono wa mfalme ukarejea katika hali yake tena, na ukawa kama ulivyokuwa mwanzoni.
7 Then the King sayde vnto the man of God, Come home with mee, that thou mayest dyne, and I will giue thee a reward.
Yule mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
8 But the man of God saide vnto the King, If thou wouldest giue me halfe thine house, I would not goe in with thee, neither woulde I eate bread nor drinke water in this place.
Yule mtu wa Mungu akamwambia mfalme, “Hata kama utanipa nusu ya miliki yako. staende na wewe, wala sitakula au kunywa maji mahali hapa,
9 For so was it charged mee by the worde of the Lord, saying, Eate no bread nor drinke water, nor turne againe by the same way that thou camest.
kwa sababu BWANA ameniamuru kwa neno lake, 'hutakula mkate wala kunywa maji, wala kurudi kwa njia ulioijia.'”
10 So he went another way and returned not by the way that he came to Beth-el.
Kwa hiyo mtu wa Mungu akaondoka na hakurudi nyumbani kwa njia aliyokuja nayo huko Betheli.
11 And an olde Prophet dwelt in Beth-el, and his sonnes came and tolde him all ye woorkes, that the man of God had done that day in Beth-el, and the wordes which he had spoken vnto the King, tolde they their father.
Sasa kulikuwa na nabii mwingine mzee aliyekuwa akiishi Betheli, na mmoja wa wana wake akaja kumwambia mambo yote ambayo mtu wa Mungu amefanya siku hiyo kule Betheli. Wana wake wakamwambia pia maneno ambayo Yule mtu wa Mungu alimwambia mfalme.
12 And their father sayde vnto them, What way went he? and his sonnes shewed him what waye the man of God went, which came from Iudah.
Baba yao akawaambia, “Alienda kwa njia gani?” Wale wanawe walikuwa wamemwona yule mtu wa Mungu kutoka Yuda njia aliyotumia kurudi.
13 And hee saide vnto his sonnes, Saddle mee the asse. Who sadled him the asse, and hee rode thereon,
Kwa hiyo akawaambia wanawe, “Nitandikeni punda.” Kwa hiyo wakamtandikia punda naye akampanda.
14 And went after the man of God, and found him sitting vnder an oke: and he saide vnto him, Art thou the man of God that camest from Iudah? And he sayd, Yea.
Yule nabii mzee akamfuata yule mtu wa Mungu na akamkuta amekaa chini ya mti wa mwaloni; akamwambia, “Je, wewe ndiye mtu wa Mungu aliyetoka Yuda?” Naye akamjibu, “Mimi ndiye.”
15 Then he said vnto him, Come home with me, and eate bread.
Kisha yule nabii mzee akamwambia, “twende nyumbani kwangu ukale chakula.”
16 But he answered, I may not returne with thee, nor go in with thee, neither wil I eate bread nor drinke water with thee in this place.
Yule mtu wa Mungu akamjibu, “Siwezi kurudi na wewe wala kuingia ndani na wewe, tena sitakula chakula wala kunywa maji pamoja na wewe mahali hapa,
17 For it was charged me by the word of the Lord, saying, Thou shalt eate no bread, nor drinke water there, nor turne againe to goe by the way that thou wentest.
kwa sababu niliamuriwa hivyo kwa neno la BWANA, 'Hautakula chakula wala kunywa maji kule, wala kurudi kwa njia utakayokuja nayo.'”
18 And he said vnto him, I am a Prophet also as thou art, and an Angel spake vnto me by the worde of the Lord, saying, Bring him againe with thee into thine house, that hee may eate bread and drinke water: but he lyed vnto him.
Kwa hiyo yule nabii mzee akamwambia, “Mimi pia ni nabii kama ulivyo, na malaika amesema na mimi neno la BWANA, akisema, 'Mrudishe aje na wewe katika nyumba yako, ili aweze kula chakula na kunywa maji.'” Lakini alikuwa anamdanganya mtu wa Mungu.
19 So he went againe with him, and did eate bread in his house, and dranke water.
Kwa hiyo yule mtu wa Mungu akarudi pamoja na yule nabii mzee na akala chakula nyumbani kwake na akanywa maji.
20 And as they sate at the table, the worde of the Lord came vnto the Prophet, that brought him againe.
Walipokuwa wamekaa mezani, neno la BWANA likamjia yule nabii aliyemrudisha,
21 And hee cried vnto the man of God that came from Iudah, saying, Thus sayeth the Lord, Because thou hast disobeyed the mouth of the Lord, and hast not kept the commandement which the Lord thy God commanded thee,
naye akalia kwa mtu wa Mungu aliyetoka Yuda, akisema “BWANA anasema, 'Kwa kuwa umeshindwa kutii nenola BWANA na umeshindwa kuishika amri ya BWANA ambayo Mungu wako alikupa,
22 But camest backe againe, and hast eaten bread and drunke water in the place (whereof he did say vnto thee, Thou shalt eate no bread nor drinke any water) thy carkeis shall not come vnto the sepulchre of thy fathers.
bali umerudi na umekula chakula na kunywa maji mahali ambapo BWANA alikwambia usile chakula wala kunywa maji, basi mwili wako hautazikwa kwenye makaburi ya baba zako.'”
23 And when he had eaten bread and drunke, he sadled him the asse, to wit, to the Prophet whome he had brought againe.
Baada ya kula chakula na kunywa maji, Yule nabii akatandika punda wa mtu wa Mungu, yule mtu aliyerudi naye.
24 And when hee was gone, a lion met him by the way, and slewe him, and his body was cast in the way, and the asse stoode thereby: the lion stood by the corps also.
Baada ya mtu wa Mungu kuondoka, akakutana na simba njiani na kumwua barabarani, na mwili wake uliachwa barabarani. Na yule punda akasimama pembeni yake, na yule simba naye akasimama pembeni ya ule mwili.
25 And beholde, men that passed by, sawe the carkeis cast in the way, and the lion standing by the corps: and they came and tolde it in ye towne where the olde Prophet dwelt.
Watu walipopita na kuuona ule mwili umeachwa barabarani, na yule simba akisimama karibu na ule mwili, walikuja wakaeleza habari hiyo mjini kule ambako yule nabii mzee aliishi.
26 And when the Prophet that brought him backe againe from the waye, hearde thereof, hee sayde, It is the man of God, who hath bene disobedient vnto the commandement of the Lord: therefore the Lord hath deliuered him vnto the lion, which hath rent him and slayne him, according to the worde of the Lord, which hee spake vnto him.
Yule nabii aliyemrudisha toka njiani aliposikia, akasema, “Yeye mtu wa Muugu ndiye aliyeshindwa kutii neno la BWANA. Kwa hiyo BWANA alimtoa kwa simba, ambaye amemrarua katika vipande vipande na kumwua, kama vile neno la BWANA lilivyokuwa limemwonya.”
27 And he spake to his sonnes, saying, Saddle me the asse. And they sadled him.
Kwa hiyo yule nabii mzee akawaamnbia wanawe, akisema, “Tandikeni punda wangu,” nao wakamtandikia.
28 And he went and founde his body cast in the way, and the asse and the lion stoode by the corps: and the lion had not eaten the bodie, nor torne the asse.
Akaenda akaukuta mwili umeachwa barabarani, punda na simba wamesimama pembeni ya ule mwili. Yule simba hakuula ule mwili, wala hakumshambulia yule punda.
29 And the Prophet tooke vp the body of the man of God, and layed it vpon the asse, and brought it againe, and the olde Prophet came to the citie, to lament and burie him.
Yule nabii akauchukua ule mwili wa mtu wa Mungu, akaulaza juu ya punda, na akaurudisha. Akaja kwenye mji wake kuomboleza na kuuzika.
30 And hee layed his bodie in his owne graue, and they lamented ouer him, saying, Alas, my brother.
Akaulaza mwili kwenye kaburi lake, nao wakamwombolezea, wakisema, “Aa! ndugu yangu!”
31 And when he had buried him, hee spake to his sonnes, saying, When I am dead, burie ye mee also in the sepulchre, wherein the man of God is buried: lay my bones beside his bones.
Kisha baada ya kumzika, yule nabii mzee akawaambia wanawe, akasema, “Nitakapokufa, mtanizika kwenye kaburi ambalo tumemzika mtu wa Mungu. Mtalaza mifupa yangu pembeni mwa mifupa yake.
32 For that thing which he cried by the word of the Lord against the altar that is in Beth-el, and against all the houses of the hie places, which are in the cities of Samaria, shall surely come to passe.
Kwa kuwa ule ujumbe uliosemwa na BWANA, dhidi ya madhabahu kule Betheli na dhidi ya nyumba zote za mahali pa juu katika mji wa Samaria, hakika yatatokea.
33 Howbeit after this, Ieroboam conuerted not from his wicked way, but turned againe, and made of the lowest of the people Priests of the hie places. Who would, might consecrate him selfe, and be of the Priestes of the hie places.
Baada ya haya Yeroboamu hakuuacha uovu wake, aliendelea kuchagua makuhani wa kawaida kwa ajili ya mahali pa juu kutoka kwa watu wa kila aina. Yeyote ambaye angeweza kutumika alimtakasa kuwa kuhani.
34 And this thing turned to sinne vnto the house of Ieroboam, euen to roote it out, and destroy it from the face of the earth.
Jambo hili likawa dhambi kwenye familia ya Yeroboamu na kusababisha familia yake kuangamizwa na kuondolewa kabisa katika uso wa dunia.

< 1 Kings 13 >