< 1 Kings 10 >

1 And the Queene of Sheba hearing ye fame of Salomon (concerning the Name of the Lord) came to proue him with hard questions.
Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni na uhusiano wake na jina la Bwana, akaja kumjaribu kwa maswali magumu.
2 And she came to Ierusalem with a verie great traine, and camels that bare sweete odours, and golde exceeding much, and precious stones: and shee came to Salomon, and communed with him of all that was in her heart.
Alifika Yerusalemu akiwa na msafara mkubwa sana: pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani; alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
3 And Salomon declared vnto her all her questions: nothing was hid from the King, which he expounded not vnto her.
Solomoni akamjibu maswali yake yote, hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwa mfalme asiweze kumwelezea.
4 Then the Queene of Sheba sawe all Salomons wisedome, and the house that he had built,
Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
5 And the meate of his table, and the sitting of his seruants, and the order of his ministers, and their apparel, and his drinking vessels, and his burnt offrings, that he offered in the house of the Lord, and she was greatly astonied.
chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika hekalu la Bwana, alipatwa na mshangao.
6 And shee sayde vnto the King, It was a true worde that I heard in mine owne lande of thy sayings, and of thy wisedome.
Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
7 Howebeit I beleeued not this report till I came, and had seene it with mine eyes: but lo, ye one halfe was not tolde mee: for thou hast more wisedome and prosperitie, then I haue heard by report.
Lakini sikuamini mambo haya hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana ile taarifa niliyoisikia.
8 Happy are the men, happie are these thy seruants, which stande euer before thee, and heare thy wisedome.
Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
9 Blessed be the Lord thy God, which loued thee, to set thee on the throne of Israel, because the Lord loued Israel for euer and made thee King to doe equitie and righteousnesse.
Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe na kukuweka juu ya kiti cha ufalme cha Israeli. Kwa sababu ya upendo wake Bwana wa milele ajili ya Israeli, amekufanya mfalme, ili kudumisha haki na uadilifu.”
10 And she gaue the King sixe score talents of golde, and of sweete odours exceeding much, and precious stones. There came no more such aboundance of sweete odours, as the Queene of Sheba gaue to King Salomon.
Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa sana cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa tena vikolezi vingi hivyo kuletwa kama vile malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
11 The nauie also of Hiram (that caried gold from Ophir) brought likewise great plentie of Almuggim trees from Ophir and precious stones.
(Meli za Hiramu zilileta dhahabu kutoka Ofiri; tena kutoka huko zilileta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
12 And the King made of ye Almuggim trees pillars for the house of the Lord, and for ye Kings palace, and made harpes and psalteries for singers. There came no more such Almuggim trees, nor were any more seene vnto this day.
Mfalme akatumia miti ya msandali kuwa nguzo ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa au kuonekana humo tangu siku ile.)
13 And King Salomon gaue vnto the Queene of Sheba, whatsoeuer she would aske, besides that, which Salomon gaue her of his kingly liberalitie: so she returned and went to her owne countrey, both shee, and her seruantes.
Mfalme Solomoni akampa malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, kando na vile mfalme alivyokuwa amempa kwa ukarimu wake wa kifalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
14 Also the weight of golde, that came to Salomon in one yeere, was sixe hundreth three score and six talents of gold,
Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
15 Besides that he had of marchant men and of the marchandises of them that solde spices, and of all the Kinges of Arabia, and of the princes of the countrey.
mbali na mapato kutoka kwa wafanyabiashara na wachuuzi, na kutoka kwa wafalme wote wa Kiarabu na watawala wa nchi.
16 And King Salomon made two hundreth targets of beaten golde, sixe hundreth shekels of gold went to a target:
Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa; kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
17 And three hundreth shieldes of beaten golde, three pound of gold went to one shielde: and the King put them in the house of the wood of Lebanon.
Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
18 Then the King made a great throne of yuorie, and couered it with the best golde.
Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
19 And the throne had six steps, and the top of the throne was round behind, and there were stayes on either side on the place of the throne, and two lions standing by the stayes.
Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na egemeo la nyuma lilikuwa la mviringo kwa juu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
20 And there stoode twelue lions on the sixe steps on either side: there was not the like made in any kingdome.
Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
21 And all King Salomons drinking vessels were of golde, and all the vessels of the house of the woode of Lebanon were of pure golde, none were of siluer: for it was nothing esteemed in the dayes of Salomon.
Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo siku za Solomoni.
22 For the King had on the sea the nauie of Tharshish with the nauie of Hiram: once in three yere came the nauie of Tharshish, and brought golde and siluer, yuorie, and apes and peacockes.
Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizokuwa zikiandamana na meli za Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
23 So King Salomon exceeded all the kings of the earth both in riches and in wisedome.
Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
24 And al the world sought to see Salomon, to heare his wisedome, which God had put in his heart,
Dunia yote ikatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
25 And they brought euery man his present, vessels of siluer, and vessels of golde, and raiment, and armour, and sweete odours, horses and mules, from yeere to yeere.
Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja alileta zawadi: vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
26 Then Salomon gathered together charrets and horsemen: and he had a thousand and foure hundreth charets, and twelue thousande horsemen, whome hee placed in the charet cities, and with the King at Ierusalem.
Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu.
27 And the King gaue siluer in Ierusalem as stones, and gaue cedars as the wilde figtrees that growe abundantly in the plaine.
Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
28 Also Salomon had horses brought out of Egypt, and fine linen: the Kings marchants receiued the linen for a price.
Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue.
29 There came vp and went out of Egypt some charet, worth sixe hundreth shekels of siluer: that is, one horse, an hundreth and fiftie and thus they brought horses to all the Kings of the Hittites and to the Kings of Aram by their meanes.
Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha na farasi kwa shekeli 150. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.

< 1 Kings 10 >