< 1 Kings 1 >

1 Now when King Dauid was olde, and striken in yeeres, they couered him with clothes, but no heate came vnto him.
Mfalme Daudi alipokuwa mzee sana, walimfunika kwa nguo, lakini hakupata joto.
2 Wherefore his seruants saide vnto him, Let there be sought for my lord ye King a yong virgin, and let her stand before the king, and cherish him: and let her lie in thy bosome, that my lord the King may get heate.
Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia, “Na tutafute msichana bikra kwa ajili ya mfalme bwana wetu. Ili amtumikie na kumtunza. Naye atalala kwenye mikono yake ili bwana mfalme wetu apate joto.
3 So they sought for a faire young maide thoroughout all the coastes of Israel, and founde one Abishag a Shunamite, and brought her to the king.
Kwa hiyo wakatafuta msichana mrembo katika mipaka yote ya Israeli. Wakampata Abishagi Mshunami wakamlte kwa mfalme.
4 And the maid was exceeding faire, and cherished the king, and ministred to him, but the King knew her not.
Yule msichana alikuwa mrembo sana. Naye akamtumikia mfalme na kumtunza, Lakini mfalme hakumjua.
5 Then Adoniiah the sonne of Haggith exalted himselfe, saying, I will be king. And he gate him charets and horsemen, and fiftie men to run before him.
Wakati huo, Adoniya mwana wa Hagithi alijiinua akisema, “Nitakuwa mfalme.” Kwa hiyo akajiandalia magari na wapanda farasi hamsini ili wapige mbio mbele yake.
6 And his father would not displease him from his childehood, to say, Why hast thou done so? And hee was a very goodly man, and his mother bare him next after Absalom.
Baba yake alikuwa hajawahi kumsumbua, kwa kusema, “kwa nini umefanya hili na lile?” Adoniya allikuwa mwanamume mzuri sana aliyezaliwa baada ya Absalomu.
7 And he tooke counsel of Ioab the sonne of Zeruiah, and of Abiathar the Priest: and they helped forward Adoniiah.
Akashauriana na Yoabu mwana wa Seruya na Abiathari kuhani. Wakamfuata Adoniya wakamsaidia.
8 But Zadok the Priest, and Benaiah the sonne of Iehoiada, and Nathan the Prophet, and Shimei, and Rei, and the men of might, which were with Dauid, were not with Adoniiah.
Lakini Sadoki kuhani, Benaya mwana wa Yehoyada, nabii Nathani, Shimei, Rei, na watu mashujaa wa Daudi hawakumfuata Adoniya.
9 Then Adoniiah sacrificed sheepe and oxen, and fat cattel by the stone of Zoheleth, which is by En-rogel, and called all his brethren the kings sonnes, and al the men of Iudah ye Kings seruants,
Adoniya akataoa dhabihu za Kondoo, na ndama walionona kwenye jiwe la Sohelethi, ambalo liko karibu na Eni Rogeli. Akawakaribisha ndugu zake wote, watoto wa mfalme, wanaume wote wa Yuda, na watumishi wa mfalme.
10 But Nathan the Prophet, and Benaiah, and the mightie men, and Salomon his brother hee called not.
Lakini hakumkaribisha nabii Nathan, Benaya, wanaume mashujaa, au ndugu yake Sulemani.
11 Wherefore Nathan spake vnto Bath-sheba the mother of Salomon, saying, Hast thou not heard, that Adoniiah ye sonne of Haggith doeth reigne, and Dauid our lord knoweth it not?
Kisha Nathani akamwambia Bethisheba mama wa Sulemani, akaisema, “Je, haujasikia kuwa Adoniya mwana wa Hagathi amekuwa mfalme, na Daudi bwana wetu halijui hilo?
12 Now therefore come, and I will now giue thee counsell, howe to saue thine owne life, and the life of thy sonne Salomon.
Kwa hiyo sasa nakupa ushauri, ili kwamba uweze kuokoa maisha yako na maisha ya mwanao Suleimani.
13 Go, and get thee in vnto King Dauid, and say vnto him, Didest not thou, my lorde, O King, sweare vnto thine handmaide, saying, Assuredly Salomon thy sonne shall reigne after me, and he shall sit vpon my throne? why is then Adoniiah King?
Nenda kwa mfalme Daudi; ukamwambie, 'Bwana wangu mfalme, Je, haukumwapia mtumishi wako, ukisema, “Hakika Sulemani mwanao atatawala baada yangu, na ataketi kwenye kiti changu cha enzi?” Kwa nini basi Adoniya anatawala?'
14 Behold, while thou yet talkest there with the King, I also will come in after thee, and confirme thy wordes.
Wakati ukiwa pale ukiongea na mfalme, Nitaingia baada yako na kuthibitisha hayo.
15 So Bath-sheba went in vnto the King into the chamber, and the King was verie olde, and Abishag the Shunammite ministred vnto ye King.
Kwa hiyo Bathisheba akaingia chumbani kwa mfalme. Wakati huo mfalme alikuwa mzee sana, na Abishagi Mshunami alikuwa akimtunza mfalme.
16 And Bath-sheba bowed and made obeisance vnto the King. And the King saide, What is thy matter?
Bathisheba akaiinama kifudifudi mbele ya mfalme. Na kisha mfalme akasema, “Una haja gani?”
17 And shee answered him, My lorde, thou swarest by the Lord thy God vnto thine handmaide, saying, Assuredly Salomon thy sonne shall reigne after me, and he shall sit vpon my throne.
Naye akamwambia, “Bwana wangu, ulimwapia mtumishi wako kwa jina la BWANA, Mungu wako, ukisema, 'Hakika Sulemani mwanao atatawala, baada yangu, naye ataketi kwenye kiti changu cha enzi.'
18 And beholde, nowe is Adoniiah king, and now, my lord, O King, thou knowest it not.
Sasa, tazama, Adoniya ni mfalme, na bwana wangu mfalme hajui jambo hili.
19 And he hath offred many oxen, and fatte cattel, and sheepe, and hath called all the sonnes of the King, and Abiathar the Priest, and Ioab the captaine of the hoste: but Salomon thy seruant hath he not bidden.
Ametoa dhabihu ya makisai, ndama walionona, na kondoo wengi, na amewakaribisha wana wote wa mfalme, Abiathari kuhani, na Yoabu jemedari wa jeshi, lakini hajamkaribisha Sulemani mtumishi wako.
20 And thou, my lorde, O King, knowest that the eyes of all Israel are on thee, that thou shouldest tell them, who shoulde sit on the throne of my lord the King after him.
Mfalme bwana wangu, macho yote ya Israeli yako kwako, yakisubiri usemi wako juu ya nani atakayeti kwenye kiti cha enzi baada yako, bwana wangu.
21 For els when my lord the King shall sleepe with his fathers, I and my sonne Salomon shalbe reputed vile.
Vinginevyo itatokea, wakati bwana wangu atakapolala na baba zake, kwamba Mimi na mwanangu Sulemani kuhesabiwa wahaini.”
22 And lo, while she yet talked with the King, Nathan also the Prophet came in.
Wakati alipokuwa akiendelea na mfalme, nabii Nathani aliingia.
23 And they tolde the King, saying, Beholde, Nathan the Prophet. And when he was come in to the King, hee made obeisance before the King vpon his face to the ground.
Watumshi wakamwambia mfalme, “Nabii Nathani yuko hapa,” Naye alipoingia mbele ya mfalme, akalala kifudifudi mbele ya mfalme na uso wake ukielekea chini.
24 And Nathan saide, My lorde, O King, hast thou said, Adoniiah shall reigne after mee, and he shall sit vpon my throne?
Nathani akamwambia, “Mfalme bwana wangu, Je, umesema, Adoniya atatawala baada yangu, na ataketi kwenye kiti changu cha enzi?
25 For hee is gone downe this day, and hath slaine many oxen, and fat cattel, and sheepe, and hath called al the Kings sonnes, and the captaines of the hoste, and Abiathar the Priest: and behold, they eate and drinke before him, and say, God saue King Adoniiah.
kwani leo ameshuka na ametoa dhabihu ya makisai, ndama walionona, na kondoo wengi, na amewakaribisha wana wote wa mfalme, jemedari wa jeshi, na Abiatahari kuhani. Nao wanakuka na kunywa mbele zake, na kusema, 'Mfalme Adoniya na aishi milele!'
26 But me thy seruant, and Zadok the Priest, and Benaiah the sonne of Iehoiada, and thy seruant Salomon hath he not called.
Lakini mimi, mtumishi wako, Sadoki kuhani, Benaya mwana wa Yehoyada, na mtumishi wako Suleimani, hajatukaribisha.
27 Is this thing done by my lord the King, and thou hast not shewed it vnto thy seruant, who should sitte on the throne of my lorde the King after him?
Je, bwana wangu mfalme amefanya haya pasipo kutuambia sisi, watumishi wako, ni nani atakayeketi kwenye kiti cha enzi baada yake?”
28 Then King Dauid answered, and saide, Call me Bath-sheba. And shee came into ye Kings presence, and stoode before the King.
Ndipo mfalme Daudi lipojibu na kusema, “Mwiteni Bathisheba arudi.” Naye akaja akasimama mbele ya mfalme.
29 And the King sware, saying, As the Lord liueth, who hath redeemed my soule out of all aduersitie,
Mfalme akafanya kiapo akasema, “Kama BWANA aishivyo, ambaye ameniokoa toka tabu zote,
30 That as I sware vnto thee by the Lord God of Israel, saying, Assuredly Salomon thy sonne shall reigne after me, and hee shall sit vpon my throne in my place, so will I certainely doe this day.
kama nilivyokuapia kwa BWANA, Mungu wa Israeli, nikisema, 'Sulemani mwanao atatawala baada yangu, naye ndiye atakayeketi kwenye kiti changu cha enzi, mahali pangu,' Nitafanya hivi leo.”
31 Then Bath-sheba bowed her face to the earth, and did reuerence vnto the King, and said, God saue my lord King Dauid for euer.
Kisha Bathisheba akalala kifudifudi na sura yake ikielekea chini mbele ya mfalme akasema, “Bwana wangu mfalme Daudi n a aishi milele!”
32 And King Dauid saide, Call mee Zadok the Priest, and Nathan the Prophet, and Benaiah the sonne of Iehoiada. And they came before the King.
Mflme Daudi akasema, “Niitieni Sadoki kuhani, nabii Nathani na Benaya mwana wa Yehoyada.” Nao wakaja mbele ya mfalme.
33 Then the King said vnto them, Take with you the seruants of your lorde, and cause Salomon my sonne to ride vpon mine owne mule, and carie him downe to Gihon.
Mfalme akawaambia, “Uwachukue watumishi wangu, bwana wako, na umfanye Sulemani mwanangu apande juu ya nyumba yangu mimi na mkamtelemshe mpaka chini Gihoni.
34 And let Zadok the Priest and Nathan the Prophet anoint him there King ouer Israel, and blowe ye the trumpet, and say, God saue king Salomon.
Na Sadoki kuhani na nabii Nathani wamtawaze awe mfalme wa Israeli na tarumbeta zipigwe, 'Mfalme Suleimani na uishi milele!'
35 Then come vp after him, that hee may come and sit vpon my throne: and hee shall bee King in my steade: for I haue appointed him to be prince ouer Israel and ouer Iudah.
Kisha njoni mkiwa nyuma yake, naye atakuja na kukaa kwenye kiti changu cha enzi; kwani yeye ndiye atakayekuwa mfalme mahali pangu. Nimemchagua yeye kuwa mtawala wa Israeli na Yuda.”
36 Then Benaiah the sonne of Iehoiada answered the King, and said, So be it, and the Lord God of my lord the King ratifie it.
Benaya mwana wa Yehoyada akamjibu mfalme, akasema, “Na iwe hivyo! Na BWANA, Mungu wa mfalme bwana wangu, alithibitishe hilo.
37 As the Lord hath bene with my lorde the King, so be he with Salomon, and exalt his throne aboue the throne of my lorde king Dauid.
Kama vile BWANA alivyokuwa na mfalme bwana wangu na awe na Sulemani hivyo hivyo, na kuifanya enzi yake kuwa kubwa kuliko zaidi ya enzi ya bwana wangu Daudi.”
38 So Zadok the Priest, and Nathan the Prophet, and Benaiah the sonne of Iehoiada, and the Cherethites and the Pelethites went downe and caused Salomon to ride vpon king Dauids mule, and brought him to Gihon.
Kwa hiyo Sadoki kuhani, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakerethi na Wapelethi wakamfanya Sulemani akapanda juu ya nyumba ya mfalme Daudi; wakamleta Gihoni.
39 And Zadok the Priest tooke an horne of oyle out of the Tabernacle, and anointed Salomon: and they blewe the trumpet, and all the people said, God saue king Salomon.
Naye Sadoki kuhani akachukua pembe lenye mafuta hemani akamtia mafuta Sulemani kisha wakapiga tarumbeta, na watu wote wakasema, 'Mfalme Sulemani na aishi milele!'
40 And all the people came vp after him, and the people piped with pipes, and reioyced with great ioye, so that the earth rang with the sound of them.
Kisha watu wote wakamfuata, na watu wakapiga zomari wakafurahi furaha kubwa mno, kiasi kwamba dunia ikatetemeka kwa sauti zao.
41 And Adoniiah and all the ghestes that were with him, heard it: (and they had made an ende of eating) and when Ioab heard the sound of the trumpet, he said, What meaneth this noise and vprore in the citie?
Kisha Adoniya na wageni wake waliokuwa pamoja naye wakasikia hayo walipomaliza kula. Yoabu alipozisikia sauti za panda, akasema, “Kwa nini jiji lilko katika hali ya taharuki?”
42 And as he yet spake, beholde, Ionathan the sonne of Abiathar the Priest came: and Adoniiah said, Come in: for thou art a worthie man, and bringest good tidings.
Wakati alipokuwa akiongea, Yonatahani mwana wa Abiathari kuhani alifika. Adoniya akamwambia, “Karibu, 'kwa kuwa wewe wastahili kutuletea habari.”
43 And Ionathan answered, and said to Adoniiah, Verely our lord King Dauid hath made Salomon King.
Naye Yonathani akamjibu Adoniya, “Mfalme bwana wetu Daudi amemfanya Sulemani kuwa mfalme.
44 And the King hath sent with him Zadok the Priest, and Nathan the Prophet, and Benaiah the sonne of Iehoiada, and the Cherethites, and the Pelethites, and they haue caused him to ride vpon the Kings mule.
Na mfalme amemtuma pamoja naye Sadoki, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, na Wakerethi pamoja na Wapelethi. Wamempandisha Sulemani juu ya nyumba ya mfalme.
45 And Zadok the Priest, and Nathan ye Prophet haue anointed him King in Gihon: and they are gone vp from thence with ioy, and the citie is moued: this is the noise that ye haue heard.
Sadoki kuhani na nabii Nathani wamemtawaza kuwa mfalme kule Gihoni, na wametokea huko wakifurahi, ndiyo maana jiji liko katika taharuki. Na hizi ndizo sauti ulizosikia.
46 And Salomon also sitteth on the throne of the kingdome.
Pia, Sulemani ameketi kwenye kiti cha enzi cha ufalme.
47 And moreouer the Kings seruantes came to blesse our lord King Dauid, saying, God make the name of Salomon more famous then thy name, and exalt his throne aboue thy throne: therefore the King worshipped vpon the bed.
Zaidi ya yote, watumishi wa mfalme walikuja kumbariki mfalme bwana wetu Daudi, wakisema, 'Mungu wako na alifanye jina la Sulemani kuwa zuri kuliko jina lako, na kuifanya enzi yako kuwa kubwa kuliko yako.' na mfalme akasujudu mwenyewe kitandani.
48 And thus sayd the King also, Blessed bee the Lord God of Israel, who hath made one to sit on my throne this day, euen in my sight.
Mfalme pia alisema, 'Abarikiwe BWANA, Mungu wa Israeli, ambaye amempa mtu kuketi kwenye enzi yangu siku hii ya leo, na kwamba macho yangu yamejionea hilo.'”
49 Then all the ghestes that were with Adonijah, were afraide, and rose vp, and went euery man his way.
Ndipo wageni wote wa Adoniya walipoogopa sana. Wakasimama na kila mtu akaenda njia yake.
50 And Adonijah fearing the presence of Salomon, arose and went, and tooke holde on the hornes of the altar.
Pia Adoniya alimwaogopa Sulemani na akasimama, na akaondoka, akachukua pembe la madhabahuni.
51 And one tolde Salomon, saying, Beholde, Adonijah doeth feare King Salomon: for lo, he hath caught holde on the hornes of the altar, saying, Let King Salomon sweare vnto me this day, that he will not slay his seruant with the sword.
Kisha Sulemani akaambiwa hilo, wakasema, “Tazama, Adoniya amemwogopa mfalme Sulemani, kwa kuwa ameshikilia pembe la madhabahuni, akisema, 'Mfalme Sulemani na aniapie kwanza kuwa hatamwua mtumishi wake kwa upanga.'”
52 Then Salomon sayd, If he will shewe him selfe a worthy man, there shall not an heare of him fall to the earth, but if wickednes be found in him, he shall dye.
Sulemani akasema, “Kama atajionyesha kuwa ni mtu wa kweli, hakuna hata unywele mmoja utakaoanguka duniani, bali kama uovu utaonekana kwake, atakufa.”
53 Then King Salomon sent, and they brought him from the altar, and he came and did obeisance vnto King Salomon. And Salomon sayde vnto him, Go to thine house.
Kwa hiyo mfalme Sulemani akatuma watu, waliomleta Adoniya kutoka madhabahuni. Naye akaja akapiga magoti kwa Sulemani, na Sulemani akamwambia, “Nenda nyumbani kwako.”

< 1 Kings 1 >