< 1 John 3 >
1 Behold, what loue the Father hath giuen to vs, that we should be called the sonnes of God: for this cause this world knoweth you not, because it knoweth not him.
Oneni basi, jinsi Baba alivyotupenda mno hata tunaitwa watoto wa Mungu! Na kweli, ndivyo tulivyo. Ndiyo maana ulimwengu haututambui sisi, kwani haumjui Mungu.
2 Dearely beloued, nowe are we the sonnes of God, but yet it is not made manifest what we shall be: and we know that when he shalbe made manifest, we shalbe like him: for we shall see him as he is.
Wapenzi wangu, sisi ni watoto wa Mungu sasa, lakini bado haijaonekana wazi jinsi tutakavyokuwa. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwani tutamwona vile alivyo.
3 And euery man that hath this hope in him, purgeth himselfe, euen as he is pure.
Basi, kila mtu aliye na tumaini hili katika Kristo, hujiweka safi kama vile Kristo alivyo safi kabisa.
4 Whosoeuer committeth sinne, transgresseth also the Law: for sinne is the transgression of the Lawe.
Kila mtu atendaye dhambi anavunja sheria ya Mungu, maana dhambi ni uvunjaji wa sheria.
5 And ye knowe that hee was made manifest, that he might take away our sinnes, and in him is no sinne.
Mnajua kwamba Kristo alikuja kuziondoa dhambi zetu, na kwamba kwake hamna dhambi yoyote.
6 Whosoeuer abideth in him, sinneth not: whosoeuer sinneth, hath not seene him, neither hath knowen him.
Basi, kila aishiye katika muungano na Kristo hatendi dhambi; lakini kila mtu atendaye dhambi hakupata kamwe kumwona, wala kumjua Kristo.
7 Litle children, let no man deceiue you: he that doeth righteousnes, is righteous, as hee is righteous.
Basi, watoto wangu, msikubali kupotoshwa na mtu yeyote. Mtu atendaye matendo maadilifu ni mwadilifu kama vile Kristo alivyo mwadilifu kabisa.
8 He that comitteth sinne, is of the deuil: for the deuill sinneth from the beginning: for this purpose was made manifest that Sonne of God, that he might loose the workes of the deuil.
Lakini atendaye dhambi ni wa Ibilisi, maana Ibilisi ametenda dhambi tangu mwanzo. Lakini Mwana wa Mungu alikuja duniani kuiharibu kazi ya Ibilisi.
9 Whosoeuer is borne of God, sinneth not: for his seede remaineth in him, neither can hee sinne, because he is borne of God.
Kila aliye mtoto wa Mungu hatendi dhambi, maana anayo hali ya kimungu ndani yake; hawezi kutenda dhambi kwa sababu yeye ni mtoto wa Mungu.
10 In this are the children of God knowen, and the children of the deuil: whosoeuer doeth not righteousnesse, is not of God, neither he that loueth not his brother.
Lakini yeyote asiyetenda mambo maadilifu, au asiyempenda ndugu yake, huyo si mtoto wa Mungu. Hiyo ndiyo tofauti iliyoko kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi.
11 For this is the message, that ye heard from the beginning, that we should loue one another,
Na, ujumbe mliousikia tangu mwanzo ndio huu: Tunapaswa kupendana!
12 Not as Cain which was of that wicked one, and slewe his brother: and wherefore slewe he him? because his owne workes were euill, and his brothers good.
Tusiwe kama Kaini ambaye, kwa kuongozwa na yule Mwovu, alimuua ndugu yake. Na, kwa nini alimuua? Kwa sababu matendo yake yalikuwa maovu, lakini yale ya ndugu yake yalikuwa mema!
13 Marueile not, my brethren, though this world hate you.
Basi, ndugu zangu, msishangae kama ulimwengu unawachukia ninyi.
14 We know that we are translated from death vnto life, because we loue the brethren: he that loueth not his brother, abideth in death.
Sisi tunajua kwamba tumekwisha pita kutoka katika kifo na kuingia katika uzima kwa sababu tunawapenda ndugu zetu. Mtu asiye na upendo hubaki katika kifo.
15 Whosoeuer hateth his brother, is a manslayer: and ye know that no manslayer hath eternall life abiding in him. (aiōnios )
Kila anayemchukia ndugu yake ni muuaji; nanyi mnajua kwamba muuaji yeyote yule hana uzima wa milele ndani yake. (aiōnios )
16 Hereby haue we perceiued loue, that he layde downe his life for vs: therefore we ought also to lay downe our liues for the brethren.
Sisi tumepata kujua upendo ni nini, kwani Kristo aliyatoa maisha yake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kuyatoa maisha yetu kwa ajili ya ndugu zetu.
17 And whosoeuer hath this worlds good, and seeth his brother haue neede, and shutteth vp his compassion from him, howe dwelleth the loue of God in him?
Basi, mtu akiwa na mali za hapa duniani, halafu akamwona ndugu yake ana shida, lakini akawa na moyo mgumu bila kumwonea huruma, anawezaje kusema kwamba anampenda Mungu?
18 My litle children, let vs not loue in worde, neither in tongue onely, but in deede and in trueth.
Watoto wangu, upendo wetu usiwe maneno matupu, bali uwe upendo wa kweli na wa vitendo.
19 For thereby we know that we are of the trueth, and shall before him assure our hearts.
Hivyo ndivyo tuwezavyo kuwa na hakika kwamba sisi ni watu wa ukweli; na hatutakuwa na wasiwasi mbele ya Mungu.
20 For if our heart condemne vs, God is greater then our heart, and knoweth all things.
Kwa maana, hata kama dhamiri yetu yatuhukumu, twajua kwamba Mungu ni mkuu zaidi kuliko dhamiri, na kwamba yeye ajua kila kitu.
21 Beloued, if our heart condemne vs not, then haue we boldnes toward God.
Wapenzi wangu, kama dhamiri yetu haina lawama juu yetu, basi, twaweza kuwa na uthabiti mbele ya Mungu,
22 And whatsoeuer we aske we receiue of him, because we keepe his commandements, and do those things which are pleasing in his sight.
na twaweza kupokea kwake chochote tunachoomba, maana tunazitii amri zake na kufanya yale yanayompendeza.
23 This is then his commandement, That we beleeue in the Name of his Sonne Iesus Christ, and loue one another as hee gaue commandement.
Na, amri yake ndiyo hii: Kumwamini Mwanae Kristo, na kupendana kama alivyotuamuru.
24 For hee that keepeth his commandements, dwelleth in him, and he in him: and hereby we knowe that hee abideth in vs, euen by that Spirit which he hath giuen vs.
Anayezitii amri za Mungu anaishi katika muungano na Mungu na Mungu anaishi katika muungano naye. Kwa njia ya Roho ambaye Mungu ametujalia, sisi twajua kwamba Mungu anaishi katika muungano nasi.