< Zephaniah 2 >

1 Come together, yes, gather together, you worthless nation—
Kusanyikeni pamoja, kusanyikeni pamoja, enyi taifa lisilo na aibu,
2 before the decree is issued, before you wither and die like a flower, before the burning anger of the Lord falls on you, before the day of the Lord's anger comes on you.
kabla ya wakati ulioamriwa haujafika na siku ile inayopeperusha kama makapi, kabla hasira kali ya Bwana haijaja juu yenu, kabla siku ya ghadhabu ya Bwana haijaja juu yenu.
3 Look to the Lord, all you people of the land who are humble and who follow his commands. Look to do what is right; look to live in humility. Perhaps you will be protected on the day of the Lord's anger.
Mtafuteni Bwana, enyi nyote wanyenyekevu wa nchi, ninyi ambao hufanya lile analoamuru. Tafuteni haki, tafuteni unyenyekevu; labda mtahifadhiwa siku ya hasira ya Bwana.
4 Gaza will be abandoned, Ashkelon will become desolate, Ashdod will be emptied by noon, Ekron will be ripped up.
Gaza utaachwa na Ashkeloni utaachwa magofu. Wakati wa adhuhuri Ashdodi utaachwa mtupu na Ekroni utangʼolewa.
5 What disaster is coming to you Philistines, you sea-people who live along the coast and in the land of Canaan! The Lord has passed judgment on you. I will destroy you—there will be no survivors.
Ole wenu ninyi ambao mnaishi kando ya bahari, enyi Wakerethi; neno la Bwana liko dhidi yenu, ee Kanaani, nchi ya Wafilisti. “Mimi nitawaangamiza, na hakuna atakayebaki.”
6 Your seacoast will become pastures, with meadows for shepherds and sheep pens for flocks.
Nchi kando ya bahari, mahali ambapo wanaishi Wakerethi, patakuwa mahali pa wachungaji na mazizi ya kondoo.
7 It will belong to those who remain of the people of Judah. They will graze their flocks there, and the shepherds will sleep in the abandoned houses of Ashkelon. For the Lord their God will be with them and make them prosperous again.
Itakuwa mali ya mabaki ya nyumba ya Yuda, hapo watapata malisho. Wakati wa jioni watajilaza chini katika nyumba za Ashkeloni. Bwana Mungu wao atawatunza, naye atawarudishia wafungwa wao.
8 I have heard the mocking taunts of the Moabites and the scornful derision of the Ammonites who have insulted my people and made threats against their territory.
“Nimeyasikia matukano ya Moabu nazo dhihaka za Waamoni, ambao waliwatukana watu wangu na kutoa vitisho dhidi ya nchi yao.
9 Consequently, as I live, declares the Lord Almighty, the God of Israel, the Moabites will become like Sodom, and the Ammonites like Gomorrah. Their land will become a place of weeds and salt pits and ruins forever. Those who remain of my people will plunder them and occupy their land.
Hakika, kama niishivyo,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, “hakika Moabu itakuwa kama Sodoma, Waamoni kama Gomora: mahali pa magugu na mashimo ya chumvi, nchi ya ukiwa milele. Mabaki ya watu wangu watawateka nyara; mabaki ya taifa langu watarithi nchi yao.”
10 This is what they will receive for their pride because they mocked and threatened the people of the Lord Almighty.
Hiki ndicho watarudishiwa kwa ajili ya kiburi chao, kwa kutukana na kudhihaki watu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.
11 The Lord will make them terribly afraid as he starves to death all the gods of the land. Every nation will worship the Lord wherever they are—all around the world.
Bwana atakuwa wa kuhofisha kwao atakapoangamiza miungu yote ya nchi. Mataifa katika kila pwani yatamwabudu, kila moja katika nchi yake.
12 You Ethiopians will be killed by the sword.
“Ninyi pia, ee Wakushi, mtauawa kwa upanga wangu.”
13 The Lord will strike the Assyrians in the north and destroy them. He will make Nineveh desolate, a dry wasteland like the desert.
Mungu atanyoosha mkono wake dhidi ya kaskazini na kuangamiza Waashuru, akiiacha Ninawi ukiwa na pakame kama jangwa.
14 Herds will lie down in the middle of the city. It will become the home for every kind of wild animal. Eagle owls and screech owls will roost on its columns. Their calls will echo through the windows. Rubble will block the doors, and the cedar woodwork will be exposed.
Makundi ya kondoo na ngʼombe yatajilaza pale, viumbe vya kila aina. Bundi wa jangwani na bundi waliao kwa sauti nyembamba wataishi juu ya nguzo zake. Mwangwi wa kuita kwao utapita madirishani, kifusi kitakuwa milangoni, boriti za mierezi zitaachwa wazi.
15 This is what will happen to this triumphant city that thought it was so secure. “Look at me!” it said proudly to itself. “There is no city as great as me!” But it has become a desolate place—just a home for wild animals. Everyone who passes by will point their finger and laugh in derision.
Huu ndio mji uliotukuka na kuishi kwa furaha wakijisikia salama. Ulisema moyoni mwako, “Mimi ndimi, na wala hapana mwingine ila mimi.” Jinsi gani umekuwa gofu, mahali pa kulala wanyama pori! Wote wanaopita kando yake wanauzomea na kutikisa mkono kwa dharau.

< Zephaniah 2 >