< Titus 3 >
1 Remind them to follow what rulers tell them to do, and to obey authorities. They should always be ready to do what is good.
Wakumbushe watu kuwastahi watawala na wenye mamlaka, kuwatii na kuwa tayari kwa kila namna kutenda mambo yote mema.
2 They should not speak badly about anyone, and they should not be argumentative. Tell them to show gentleness and kindness to everyone.
Waambie wasimtukane mtu yeyote; bali waishi kwa amani na masikizano, wawe daima wapole kwa kila mtu.
3 For there was a time when we too were foolish and disobedient. We were deceived and slaves to various desires and pleasures. We lived wicked lives full of jealousy, hateful people hating one another.
Maana, wakati mmoja sisi tulikuwa wapumbavu, wakaidi na wapotovu. Tulikuwa watumwa wa tamaa na anasa za kila aina. Tuliishi maisha ya uovu na wivu; watu walituchukia nasi tukawachukia.
4 But when the goodness and love of God our Savior was revealed, he saved us,
Lakini wakati wema na upendo wa Mungu, Mwokozi wetu, ulipofunuliwa,
5 not because of anything good that we've done, but because of his mercy. He did this through the cleansing of rebirth and renewal of the Holy Spirit,
alituokoa. alituokoa si kwa sababu ya jambo lolote jema tulilotenda sisi, bali alituokoa kwa sababu ya huruma yake, kwa njia ya Roho Mtakatifu anayetujalia tuzaliwe upya na kuwa na maisha mapya kwa kutuosha kwa maji.
6 which he poured out on us abundantly through Jesus Christ our Savior.
Mungu alitumiminia Roho Mtakatifu bila kipimo kwa njia ya Yesu Kristo, Mwokozi wetu,
7 Now that we are set right by his grace we have become heirs having the hope of eternal life. (aiōnios )
ili kwa neema yake tupate kukubaliwa kuwa waadilifu na kuupokea uzima wa milele tunaoutumainia. (aiōnios )
8 You can trust what I'm saying, and I want you to emphasize these instructions so that those who trust in God will think seriously about them and continue to do good. They are excellent and helpful for everyone.
Jambo hili ni kweli. Ninakutaka uyatilie mkazo mambo haya, ili wale wanaomwamini Mungu, wawe na hamu ya kuutumia wakati wao katika kutenda mema, ambayo ni mambo mazuri na ya manufaa kwa watu.
9 Avoid pointless discussions, and obsessions about ancestry. Don't get into arguments, and avoid fights over the Jewish laws—they're useless and don't help at all.
Lakini jiepushe na ubishi wa kipumbavu, ugomvi na mabishano juu ya Sheria. Mambo hayo hayana faida yoyote na ni ya bure tu.
10 Warn someone who is divisive once, and then again—after that don't pay them any attention,
Mtu anayesababisha mafarakano mpe onyo la kwanza na la pili, kisha achana naye.
11 realizing that they're perverse and sinful and have condemned themselves.
Wajua kwamba mtu wa namna hiyo amepotoka kabisa, na dhambi zake zathibitisha kwamba amekosea.
12 As soon as I send Artemas or Tychicus to you, try and come to me at Nicopolis because I'm planning to spend the winter there.
Baada ya kumtuma kwako Artema au Tukiko, fanya bidii kuja Nikopoli unione, maana nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
13 Do all you can to help Zenas the lawyer and Apollos on their way so that they have everything they need.
Jitahidi kumsaidia mwana sheria Zena na Apolo ili waweze kuanza ziara zao na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji.
14 May our people learn the habit of doing good in providing for the daily needs of others. They need to be productive!
Ni lazima watu wetu wajifunze kuutumia wakati wao katika kutenda mema ili wasaidie katika mahitaji ya kweli, na maisha yao yawe ya kufaa.
15 Everyone here with me sends their greetings. Give our best wishes to those who love us, those who trust in God. May grace be with you all.
Watu wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu katika imani. Nawatakieni nyote neema ya Mungu.