< Revelation 20 >

1 I saw an angel descending from heaven, holding the key of the Abyss and a large chain in his hand. (Abyssos g12)
Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, akiwa ameshika ufunguo wa lile Shimo na mnyororo mkubwa mkononi mwake. (Abyssos g12)
2 He seized the dragon, the ancient serpent, who is the Devil and Satan, and bound him in chains for one thousand years.
Akalishika lile joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ndiye ibilisi au Shetani, naye akamfunga kwa muda wa miaka 1,000.
3 The angel threw him into the Abyss and shut it and sealed it over him, so that he would no longer be able to deceive the nations until the thousand years were over. After that he has to be set free for a little while. (Abyssos g12)
Akamtupa katika lile Shimo, akamfunga humo na kulitia lakiri, ili kumzuia asiendelee kudanganya mataifa mpaka hiyo miaka 1,000 itimie. Baada ya hayo lazima afunguliwe kwa muda mfupi. (Abyssos g12)
4 I saw people sitting on thrones who had been given the responsibility to judge, and the souls of those who had been beheaded for their testimony about Jesus and for sharing the word of God. They had not worshiped the beast or his image, nor had they received the mark on their foreheads or their hands. They lived and reigned with Christ for a thousand years.
Kisha nikaona viti vya enzi vilivyokuwa vimekaliwa na hao waliopewa mamlaka ya kuhukumu, na nikaona roho za wale waliokatwa vichwa kwa sababu ya ushuhuda wa Yesu na kwa sababu ya neno la Mungu. Hawakuwa wamemsujudu huyo mnyama wala sanamu yake wala hawakupokea ile chapa yake kwenye vipaji vya nyuso zao au kwenye mikono yao. Wakawa hai na kutawala pamoja na Kristo miaka 1,000.
5 This is the first resurrection. (The rest of the dead did not live again until the thousand years had ended.)
(Wafu waliosalia hawakufufuka mpaka ilipotimia hiyo miaka 1,000.) Huu ndio ufufuo wa kwanza.
6 Blessed and holy are those who take part in the first resurrection! The second death has no power over them. They will be priests of God, and of Christ, and they will reign with him for one thousand years.
Waliobarikiwa na walio watakatifu ni wale walio na sehemu katika ufufuo wa kwanza. Hao mauti ya pili haina nguvu juu yao, bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye kwa muda wa miaka 1,000.
7 Once the thousand years are over, Satan will be set free from his prison,
Hiyo miaka 1,000 itakapotimia, Shetani atafunguliwa kutoka kifungoni mwake,
8 and will go out to deceive the nations, symbolized by Gog and Magog, to gather them together for battle from the four corners of the world. Their number is as uncountable as sand on the seashore.
naye atatoka ili kuyadanganya mataifa yaliyopo katika pembe nne za dunia, yaani, Gogu na Magogu apate kuwakusanya tayari kwa vita. Idadi yao ni kama mchanga ulioko pwani.
9 They marched over the earth on a broad front and encircled the camp of the believers, the beloved city. But fire rained down from heaven and burned them up.
Nao walitembea katika eneo lote la dunia, wakaizunguka kambi ya watakatifu na ule mji unaopendwa. Lakini moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza.
10 The devil, who had deceived them, was thrown into the lake of fire and sulfur where the beast and the false prophet had also been thrown, and they will suffer in anguish day and night for ever and ever. (aiōn g165, Limnē Pyr g3041 g4442)
Naye ibilisi aliyewadanganya akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti walikokuwa wametupwa yule mnyama na yule nabii wa uongo. Watateswa humo usiku na mchana, milele na milele. (aiōn g165, Limnē Pyr g3041 g4442)
11 Then I saw a large white throne with the one who sits on it. Heaven and earth vanished, and they were never seen again.
Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha enzi pamoja na yeye aliyeketi juu yake. Dunia na mbingu zikaukimbia uso wake wala mahali pao hapakuonekana.
12 I saw the dead, great and small, standing before the throne, and the books were opened. Another book, the Book of Life, was opened and the dead were judged based on what was written in the books about what they had done.
Nami nikawaona wafu wakubwa na wadogo, wakiwa wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi na vitabu vikafunguliwa. Pia kitabu kingine kikafunguliwa ambacho ni kitabu cha uzima. Hao wafu wakahukumiwa sawasawa na matendo yao kama yalivyoandikwa ndani ya hivyo vitabu.
13 The sea handed over the dead in it, and death and Hades handed over the dead that were in them, and everyone was judged according to what they had done. (Hadēs g86)
Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake, nayo mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Kila mtu akahukumiwa kulingana na yale aliyoyatenda. (Hadēs g86)
14 Then death and Hades were thrown into the lake of fire. The lake of fire is the second death. (Hadēs g86, Limnē Pyr g3041 g4442)
Kisha mauti na Kuzimu zikatupwa katika ziwa la moto. Hii ndio mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. (Hadēs g86, Limnē Pyr g3041 g4442)
15 Anyone whose name was not found written in the book of life was thrown into the lake of fire. (Limnē Pyr g3041 g4442)
Iwapo mtu jina lake halikuonekana katika kile kitabu cha uzima, alitupwa ndani ya lile ziwa la moto. (Limnē Pyr g3041 g4442)

< Revelation 20 >