< Revelation 14 >

1 I looked, and saw the Lamb standing on Mount Zion. With him were 144,000 who had his name, and the name of his Father, written on their foreheads.
Kisha nikatazama na hapo mbele yangu alikuwepo Mwana-Kondoo, akiwa amesimama juu ya Mlima Sayuni. Pamoja naye walikuwa wale 144,000 wenye Jina la Mwana-Kondoo na Jina la Baba yake likiwa limeandikwa kwenye vipaji vya nyuso zao.
2 I heard a voice from heaven that sounded like rushing water and loud thunder and many harps being played.
Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi yaendayo kwa kasi na sauti kama ngurumo ya radi. Sauti hiyo niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi wakipiga vinubi vyao.
3 They sang a new song in front of the throne and the four living creatures and the elders. Nobody could learn the song except the 144,000, those who had been redeemed from the earth.
Nao wakaimba wimbo mpya mbele ya hicho kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe wanne wenye uhai na wale wazee. Hakuna mtu yeyote aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao 144,000 waliokuwa wamekombolewa kutoka duniani.
4 They have not become morally impure by sinning with women; spiritually they are virgins. They follow the Lamb wherever he goes. They were redeemed from humankind as the firstfruits to God and the Lamb.
Hawa ndio wale ambao hawakujitia unajisi kwa wanawake, kwa kuwa wao ni bikira. Wao humfuata Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamekombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu wakawa malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.
5 They speak no lies; they are without fault.
Vinywani mwao hapakuonekana uongo, wala hawakuwa na hatia yoyote.
6 Then I saw another angel flying in mid-heaven. He had the eternal good news to announce to those who lived on the earth, to every nation, tribe, language, and people. (aiōnios g166)
Kisha nikamwona malaika mwingine akiruka juu angani, naye alikuwa na Injili ya milele ya kuwatangazia wale waishio duniani, yaani, kwa kila taifa, kabila, lugha na jamaa. (aiōnios g166)
7 He cried out in a loud voice, “Give God reverence and glory, for the time of his judgment has come. Worship the one who made heaven and earth and sea and springs of water.”
Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumpa utukufu, kwa maana saa ya hukumu yake imewadia. Mwabuduni yeye aliyeziumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji.”
8 A second angel followed, calling out, “Babylon the great has collapsed into ruins! She made all the nations drink the wine of her sexual immorality that brings God's furious opposition.”
Malaika wa pili akafuata akisema, “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu, ule uliyafanya mataifa yote kulewa kwa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake.”
9 A third angel followed the first two, and cried out in a loud voice, “If anyone worships the beast and his image and receives a mark on their forehead or on their hand,
Malaika wa tatu akawafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Kama mtu yeyote anamwabudu huyo mnyama na sanamu yake na kutiwa chapa yake kwenye kipaji chake cha uso au kwenye mkono wake,
10 they will also drink of the wine of God's furious opposition that is poured undiluted into the cup of his anger, and they will suffer anguish in fire and burning sulfur before the holy angels and the Lamb.
yeye pia atakunywa mvinyo wa hasira kali ya Mungu ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake pasipo kuchanganywa na maji. Naye atateswa kwa moto uwakao na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele za Mwana-Kondoo.
11 The smoke of their anguish ascends for ever and ever. They don't have any relief day or night, those who worship the beast and his image and who receive the mark of his name.” (aiōn g165)
Nao moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele. Hakuna mapumziko, mchana wala usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake, au kwa yeyote anayepokea chapa ya jina lake.” (aiōn g165)
12 This means the believers must patiently endure, keeping God's commandments and trusting in Jesus.
Hapa ndipo penye wito wa subira na uvumilivu wa watakatifu; wale wanaozishika amri za Mungu na kudumu katika uaminifu kwa Yesu.
13 Then I heard a voice from heaven that told me, “Write this down! Blessed are the dead who die in the Lord from now on. Yes, says the Spirit, because they can rest from their troubles. What they have accomplished will speak for them.”
Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika: Wamebarikiwa wafu wafao katika Bwana tangu sasa.” “Naam,” asema Roho, “watapumzika kutoka taabu zao, kwa kuwa matendo yao yatawafuata.”
14 I looked and I saw a white cloud. Sitting on the cloud was someone that looked like the Son of man, wearing a golden crown on his head and holding a sharp sickle in his hand.
Nikatazama, hapo mbele yangu palikuwa na wingu jeupe, na aliyekuwa ameketi juu ya hilo wingu alikuwa “kama Mwana wa Adamu” mwenye taji ya dhahabu kichwani mwake na mundu mkali mkononi mwake.
15 Another angel came out of the Temple and shouted in a loud voice to the one sitting on the cloud, “Take your sickle and start reaping, for it is harvest-time, and earth's harvest is ripe.”
Kisha malaika mwingine akaja kutoka hekaluni naye akamwita kwa sauti kubwa yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akasema, “Chukua mundu wako ukavune kwa kuwa wakati wa mavuno umewadia, kwa maana mavuno ya dunia yamekomaa.”
16 The one sitting on the cloud swung his sickle towards the earth, and reaped earth's harvest.
Hivyo yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akauzungusha mundu wake duniani, nayo dunia ikavunwa.
17 Another angel came out of the Temple in heaven. He also had a sharp sickle.
Malaika mwingine akatoka katika hekalu lililoko mbinguni, naye pia alikuwa na mundu mkali.
18 He was followed by an angel coming from the altar that was in charge of the fire, who called in a loud voice to the angel with the sharp sickle, “Take your sharp sickle and harvest the bunches of grapes from the earth's vine, because its grapes are ripe.”
Kisha malaika mwingine, aliyekuwa na mamlaka juu ya moto, akatoka kwenye madhabahu, naye akamwita yule malaika mwenye mundu mkali kwa sauti kubwa, akisema, “Chukua mundu wako mkali ukakusanye vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva.”
19 The angel swung his sickle on the earth and harvested the grapes from the vine, and threw them into the great winepress of God's judgment.
Hivyo yule malaika akauzungusha mundu wake duniani na kukusanya zabibu za dunia na kuzitupa kwenye shinikizo kubwa la ghadhabu ya Mungu.
20 They were trampled in the winepress outside the city. Blood flowed out of the winepress to the height of a horse's bridle, and to a distance of 1,600 stadia.
Lile shinikizo likakanyagwa nje ya mji, nayo damu ikatiririka kama mafuriko kutoka hilo shinikizo kufikia kimo cha hatamu za farasi, kwa umbali wa maili 200.

< Revelation 14 >