< Psalms 74 >

1 A psalm (maskil) of Asaph. God, why have you rejected us? Is it forever? Why does your anger burn so hot against the sheep of your own field?
Mungu, kwa nini umetukataa milele? Kwa nini hasira yako inawaka dhidi ya kondoo wa malisho yako?
2 Remember the people you made your own long ago, the tribe you redeemed and made your own. Remember too Mount Zion, the place where you live.
Wafikilie watu wako, ambao uliwanunua siku nyingi zilizopita, kabila ambalo wewe umelikomboa liwe urithi wako, na Milima Sayuni, mahali uishipo.
3 Come and walk through the complete devastation. The enemy has totally destroyed your Temple.
Uje utazame uharibifu kamili, uharibifu ambao umefanywa na adui mahali patakatifu.
4 The enemy shouted in triumph right where you met with us. There they set up their war banners as signs of their victory.
Washindani wako walivamia katikati ya mahali pako maalumu; walipandisha bendera zao za vita.
5 They acted like men chopping down a forest with axes.
Walipakatakata kwa shoka kama katika msitu mnene.
6 With axes and hammers they smashed in the carved wooden panels.
Walipaharibu na kuvunja sanaa zilizonakshiwa zote; walizivunja kwa shoka na nyundo.
7 Then they set fire to your Temple, burning it to the ground. They defiled the place where you live, the place that bears your name.
Walipachoma patakatifu pako; walipanajisi mahari unapoishi, wakigongagonga kwenye ardhi.
8 They said to themselves, “Let's destroy it all!” So they burned down every place where God was worshiped throughout the land.
Walisema mioyoni mwao, “Tutawaharibu wote.” Walichoma sehemu zako zote za kukutania katika nchi.
9 We no longer see any signs. There are no prophets left. And no one among us knows how long this will last.
Sisi hatuoni tena ishara; hakuna tena nabii, na hakuna yeyote miongoni mwetu ajuaye haya yatadumu kwa muda gani.
10 How long will the enemy ridicule you, God? Will they insult your character forever?
Mpaka lini, Mungu, adui atakurushia wewe matusi? Je, atalitukana jina lako milele?
11 Why do you hold back from doing something? Take action and destroy them!
Kwa nini umerudisha nyuma mkono wako, mkono wako wa kuume? Utoe mkono wako kwenye mavazi yako na uwaangamize.
12 But you, God, are our king from long ago. You have saved us many times in the land.
Lakini Mungu amekuwa mfalme wangu tangu enzi, akileta wokovu tuniani.
13 You were the one who split apart the sea by your strength; you broke the heads of the sea monsters.
Wewe uliigawa bahari; ulishambulia vichwa vya majitu ya kutisha baharini majini.
14 You were the one who crushed the heads of Leviathan, and you gave its body to the desert animals to eat.
Wewe ulishambulia vichwa vya lewiathani; na kumfanya awe chakula cha viumbe hai jangwani.
15 You were the one who made springs and rivers flow with water. You made permanent rivers dry up.
Ulizifungulia chemchem na vijito; uliikausha mito itiririkayo.
16 You created the day, and also the night; you made the moon and the sun.
Mchana ni wako, na usiku ni wako pia; uliweka jua na mwezi mahari pake.
17 You set the boundaries of the earth; you made summer and winter.
Umeiweka mipaka ya nchi; umeumba majira ya joto na majira ya baridi.
18 So keep in mind how the enemy ridiculed you, Lord, and how irreverent people insulted your reputation.
Kumbula vile adui alivyo vurumisha matusi kwako, Yahwe, na kwamba watu wapumbavu wamelitukana jina lako.
19 Don't let wild animals kill your turtledoves! Don't abandon your people forever!
Usimtoe njiwa afe kwa mnyama wa porini. Usiusahau milele uhai wa watu wako walio onewa.
20 Remember your promises in the agreement, because the land is full of dark places and violence.
Kumbuka agano lako, maana majimbo ya giza ya nchi yamejaa maeneo ya vurugu.
21 Don't let those who suffer be mistreated again. Let the poor and needy praise you for you who are.
Usiwaache walioonewa warudishwe kwa aibu; uwaache maskini na walioonewa walisifu jina lako.
22 Stand up, God, and plead your case. Don't forget how these foolish people insulted you all the time.
Inuka Mungu, itetee heshima yako; kumbuka wajinga wanavyokutukana machana kutwa.
23 Don't ignore what your enemies have said, for their loud accusations against you are getting worse and worse!
Usisahau sauti ya adui zako au kelele za wale wanaoendelea kukuchafua.

< Psalms 74 >