< Psalms 68 >

1 For the music director. A psalm of David. A song. Stand up, God, and scatter your enemies. Let those who hate him run away from him!
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
2 Blow them away as if they were smoke; melt them like beeswax in a fire. Let the wicked die in God's presence.
Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
3 But those who are right with God are happy, and they celebrate in God's presence, full of joy.
Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
4 Sing praises to God! Sing praises to his wonderful reputation! Praise the rider of the clouds—his name is the Lord! Be happy in his presence!
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
5 He is a father to the orphans, a protector of widows. This is who God is, who lives in his holy place.
Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
6 God gives those who are abandoned a family to live with. He sets prisoners free with celebration. But those who rebel live in a desert wasteland.
Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
7 God, when you led your people out, when you marched through the desert, (Selah)
Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
8 the earth quaked, and the heavens shook before God, the one of Sinai; before God, the God of Israel.
dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
9 You sent plenty of rain to water the promised land; refreshing it when it was dry.
Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
10 Your people settled there, and because of your kindness, God, you looked after the poor. (Selah)
Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
11 The Lord gives the command, and a great army of women spread the good news.
Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
12 The kings of the foreign armies are quick to run away, and the women who stayed at home divide the plunder!
“Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
13 Why are you staying at home? There are ornaments in the shape of a dove with wings of silver and feathers of fine gold to be taken.
Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
14 The Almighty scattered the foreign kings like a snowstorm on Mount Zalmon.
Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
15 “Mountain of God,” Mount Bashan, with your many high peaks, Mount Bashan,
Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
16 why do you look enviously, mountain with many peaks, at the mountain God chose as his home, where the Lord will live forever?
Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
17 God's chariots can't be counted; there are thousands and thousands of them. He comes among them from Sinai into his Temple.
Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
18 As you ascended to your high throne you led a procession of prisoners. You received gifts from the people, even from those who had rebelled against the home of the Lord God.
Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
19 May the Lord be blessed, for every day he carries our burdens. God is our salvation. (Selah)
Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
20 For us, God is a God who saves. The Lord God provides our escape from death.
Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
21 But God will crush the heads of his enemies, the hairy heads of those who continue to sin.
Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
22 The Lord says, “I will drag them down from Bashan; I will drag them up from the depths of the sea,
Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
23 so that you may walk in their blood. Even your dogs will have their share of your enemies.”
ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
24 People watch your processions, God—the processions of my God and King as they go into the Temple.
Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
25 The singers are at the front, the musicians at the back, and in the middle girls playing tambourines.
Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
26 Praise God, everyone who has come to worship; praise the Lord, everyone who belongs to Israel.
Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
27 There is the little tribe of Benjamin, followed by the many leaders from Judah; then come the leaders of Zebulun and Naphtali.
Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
28 Display your power, God! Reveal your strength, Lord, as you have done for us in the past.
Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
29 Because of your Temple in Jerusalem, kings bring tribute to you.
Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
30 Condemn the beasts of the reeds, the bulls and calves! May they be humbled and bring bars of silver in tribute! Scatter the war-loving nations!
Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
31 Let Egypt come with bronze gifts; let Ethiopia come quickly and hand over their tributes to God!
Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
32 Sing to God, kingdoms of the earth, sing praises to the Lord. (Selah)
Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
33 Sing to the rider of the ancient heavens, his strong voice sounding like thunder!
mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
34 Let everyone know of God's power: how his majesty extends over Israel, how his strength is revealed in the heavens.
Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
35 How awesome is God in his Temple! The God of Israel gives strength and power to his people! Praise God!
Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!

< Psalms 68 >