< Psalms 63 >
1 A psalm of David, when he was in the Judean desert. God, you are my God, I eagerly look for you. I am thirsty for you; all that I am longs for you in this dry, weary, waterless land.
Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
2 I see you in the Temple; I watch your power and glory.
Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
3 Your trustworthy love is better than life itself; I will praise you.
Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
4 I will thank you as long as I live; I lift up my hands as I celebrate your wonderful character.
Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
5 You satisfy me more than the richest food; I will praise you with joyful songs.
Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
6 I think of you all night long as I lie on my bed meditating about you.
Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
7 For you are the one who helps me; I sing happily from under your wings.
Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
8 I hold on to you; your strong arms lift me up.
Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
9 Those who are trying to destroy me will go down into the grave.
Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa, watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.
10 They will be killed by the sword; they will become food for jackals.
Watatolewa wafe kwa upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 But the king will be happy for what God has done. All who follow God will praise him, but those who tell lies will be silenced.
Bali mfalme atafurahi katika Mungu, wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu, bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.