< Psalms 57 >

1 For the music director. According to “Do Not Destroy.” A psalm (miktam) of David concerning the time he fled from Saul and hid in the cave. Please be kind to me, God! Be kind to me because I come to you for protection. I will shelter under the shadow of your wings until the danger is past.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
2 I cry out for help to God Most High, to God who vindicates me.
Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
3 From heaven he sends his help, and he saves me. He defeats those who persecute me. (Selah) God sends me his unfailing love, showing he is completely trustworthy.
Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
4 I am surrounded by man-eating lions—I am forced to live with them! Their teeth are spears and arrows, and their tongues are swords.
Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
5 God, your greatness is above the highest heavens; and your glory covers the whole earth!
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 They set a trap to catch me. I was so depressed. They dug a pit on my path but they were the ones who fell into it. (Selah)
Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
7 I have confidence in you, God, I have confidence in you. I will sing songs of praise to you.
Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
8 I say to myself, “Wake up!” Wake up, harp and lyre! I will wake up the dawn!
Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
9 I will thank you among the peoples, Lord; I will sing your praises among the nations.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
10 Your faithful love reaches to the heavens; your trustworthiness to the clouds.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
11 God, your greatness is above the highest heavens; and your glory covers the whole earth!
Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.

< Psalms 57 >