< Psalms 56 >
1 For the music director. According to “Dove on Distant Oaks.” A psalm (miktam) of David concerning the time the Philistines captured him in Gath. God, please be gracious to me, for people are persecuting me; my attackers fight against me all day long.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
2 My enemies chase me down all the time—there are many of them, attacking me in their arrogance.
Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
3 But when I'm afraid, I trust in you.
Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
4 I thank God for his promises. I trust in God, so why should I be fearful? What can mere human beings do to me?
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
5 They constantly twist my words against me; they spend all their time thinking of evil things to do to me.
Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
6 They gather together in their hiding places to keep watch on me, hoping to kill me.
Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
7 Will they escape when they do so much evil? God, in anger bring these people down!
Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
8 You've kept track of all my wanderings. You've collected all my tears in your bottle. You've kept a record of each one.
Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
9 Then those who hate me will run away when I call for your help. For I know this: God is for me!
Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
10 I thank God for his promises. I thank the Lord for his promises.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
11 I trust in God, so why should I be fearful? What can mere human beings do to me?
katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
12 God, I will keep my promises to you. I will give thank offerings to you,
Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
13 for you have saved me from death and kept me from falling. Now I walk in the presence of God, in the light that gives life.
Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.