< Psalms 48 >
1 For the music director. A psalm of the sons of Korah. The Lord is supreme! He deserves praise in the city of our God on his holy mountain.
Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
2 Mount Zion is high and beautiful, bringing happiness to all the earth; on the northern side is the city of the great King.
Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
3 God himself is in the city's fortresses; he is recognized as its defender.
Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
4 Look at what happened when foreign kings joined forces and came to attack the city.
Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
5 As soon as they saw it they were astonished and ran away terrified.
Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
6 They shook all over, and were in agonizing pain like a woman giving birth,
Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
7 just as the strong east wind wrecks the ships from Tarshish.
Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
8 Just as we had heard, but now we have seen the city of the Lord Almighty. This is the city of our God; he makes it secure forever. (Selah)
Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
9 God, we recall your trustworthy love as we worship in the Temple.
Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
10 As is fitting for your reputation, God, praises to you stretch all around the world. What you do is always right!
Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
11 Let the people of Mount Zion be glad; let the people of Judah celebrate because your judgments are always fair!
Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
12 Go and take a look at Zion. Count the towers as you walk around.
Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
13 Inspect the fortifications. Examine the citadels, so you can describe everything to the next generation, telling them:
mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
14 “This is who our God is. He is our God forever and ever. He himself will lead us until the very end.”
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.