< Psalms 46 >
1 For the music director by the sons of Korah. According to alamoth, a song. God is our protection and our strength; always ready to help when troubles come.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
2 So we will not be afraid though the earth shakes, though the mountains fall into the depths of the sea,
Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
3 though the waters roar and foam, though the mountains tremble as the waters surge violently! (Selah)
Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
4 A river flows to bring happiness to those in God's city, the holy place where the Most High lives.
Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
5 God is in the midst of the city; it will never fall. God protects it as soon as it is light.
Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
6 Nations are in turmoil, kingdoms collapse. God raises his voice and the earth melts.
Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
7 The Lord Almighty is with us; the God of Jacob protects us. (Selah)
Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
8 Come and see what the Lord has achieved! See the amazing things he has done on the earth!
Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
9 He stops wars all over the world. He smashes the bow; he breaks the spear; he sets shields on fire.
Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
10 Stop fighting! Recognize I am God! I am the ruler of the nations; I am the ruler of the earth.
“Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
11 The Lord Almighty is with us; the God of Jacob protects us. (Selah)
Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.