< Psalms 45 >

1 For the music director. To the tune “Lilies.” A psalm (maskil) of the sons of Korah. A love song. I am moved to write about this wonderful subject. Let me share what I have written for the king. What I say comes from the pen of a skilled author.
Moyo wangu unafurika kwa neno zuri; nitasoma kwa sauti maneno niliyo yaandika kuhusu mfalme; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mwenye ustadi.
2 You are more handsome than anyone else. You always speak graciously, for God has blessed you forever.
Wewe u mzuri sana kuliko mwanadamu yeyote; neema imemiminwa midomoni mwako; Kwa hiyo tunajua ya kuwa Mungu amekubariki milele.
3 Strap on your sword, mighty warrior, stride out in glory and majesty!
Weka upanga wako upande wako, wewe uliye mwenye nguvu, katika utukufu wako na enzi yako.
4 In your majesty ride out to victory, in the defense of truth, humility, and right, because you are strong and act powerfully.
Katika enzi yako enenda katika ushindi kwa sababu ya uaminifu, upole, na haki; mkono wako wa kuume utakufundisha mambo ya kutisha.
5 Your sharp arrows pierce the hearts of your enemies; the nations fall under you.
Mishale yako ni mkali; watu huanguka chini yako; mishale yako imo ndani ya mioyo ya adui za mfalme.
6 Your throne comes from God, and lasts forever and ever. The scepter with which you rule is a scepter of fairness.
Kiti chako cha enzi, Mungu ni cha milele na milele; na fimbo ya haki ni fimbo ya utawala wako.
7 You love what is right and hate what is wrong. That is why God, your God, has placed you above everyone else by anointing you with the oil of joy.
Umeipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupaka mafuta ya furaha kuliko wenzako.
8 Your robes are perfumed with aloes, myrrh, and cassia; music played on stringed instruments in palaces decorated with ivory makes you happy.
Mavazi yako yote hunukia manemane, udi, na mdalasini; kukoka katika majumba ya pembe vyombo vya muziki wa nyuzi vimekufurahisha.
9 The daughters of kings are among the noblewomen; the queen stands beside you on your right, wearing jewelry made of gold from Ophir.
Binti za wafalme ni kati ya wake zako waheshimiwa; na mkono wako wa kuume amesimama malikia aliye vaa mavazi ya dhahabu ya Ofiri.
10 Listen to what I have to say, daughter; please pay attention. Don't pine for your people and your family.
Sikiliza, mwanangu, tafakari na utege sikio lako; uwasahahu watu wako na watu wa nyumba ya baba yako.
11 May the king desire you in your beauty; respect him, for he is your lord.
Hivyo mfalme atautamani uzuri wako; yeye ni Bwana wako; umstahi.
12 The people of Tyre will come with gifts; rich people will look for your favor.
Binti wa Tiro atakuwepo akiwa na zawadi; matajiri kati wa watu watajipendekeza kwako.
13 Inside her preparation room the princess bride looks wonderful in her golden gown.
Binti mfalme katika jumba la kifahari ana utukufu wote; mavazi yake yametengenezwa kwa dhahabu.
14 Wearing her beautiful clothes she is brought to the king, followed by her bridesmaids.
Naye ataongozwa kwa mfalme akiwa katika mavazi ya dhahabu; mabikra, wenzake wanoumfuata, wataletwa kwako mafalme.
15 What a happy, joyful procession enters the king's palace!
Wao wataongozwa kwa furaha na shangwe; wataingia mahali pa mfalme.
16 Your sons will take the place of your fathers; as princes you will make them rulers throughout the land.
Katika mahali pa baba zako watoto wako watakuwepo, ambao wewe utawafanya kuwa wakuu katika nchi yote.
17 Through my words you will be famous through all generations, and nations will praise you forever and ever.
Nami nitalifanya jina lako kukumbukwa katika uzao wote; kwa hiyo watu watakushukuru milele na milele.

< Psalms 45 >