< Psalms 142 >

1 A maskil of David, when he was in the cave. A prayer. I call out to the Lord for help; pleading with the Lord for mercy.
Kwa sauti yangu namlilia Yahwe anisaidie; kwa sauti yangu naomba kwa ajili ya neema ya Yahwe.
2 I pour out my complaints before him; I tell him what's troubling me.
Namwaga malalamiko yangu mbele zake; ninamwambia shida zangu.
3 When I'm totally discouraged, you know the direction I should take. But whichever way I go, people set traps for me.
Roho yangu inapokuwa dhaifu ndani yangu, wewe unajua mapito yangu. Kwenye njia niipitayo wamenifichia mtego.
4 I look to my right for someone to support me—but no one pays me any attention. There's no safe place for me—no one cares about me at all.
Natazama kulia kwangu na sioni yeyote anayenijali. Sina pa kukimbilia; hakuna anayejali kuhusu uhai wangu.
5 I cry out to you, Lord, for help, saying, “You are the one who keeps me safe; you are all I need in life.
Nilikuita wewe, Yahwe; nikasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.
6 Please listen to my sad cry, for I'm feeling very low. Please save me from those who are after me, for they're too strong for me.
Sikia kuita kwangu, maana nimeshushwa chini sana; uniokoe dhidi ya watesi wangu, maana wana nguvu kuliko mimi.
7 Release me from my prison so I can praise you for the person you are! Those who live right will gather round me because you have treated me so well.”
Uitoe nafsi yangu kifungoni ili niweze kulishukuru jina lako. Wenye haki watakusanyika karibu nami kwa sababu umekuwa mwema kwangu.”

< Psalms 142 >