< Psalms 141 >
1 A psalm of David. Lord, I'm calling out to you! Please hurry up and help me! Please listen to me when I cry out to you!
Ee Yahwe, ninakulilia wewe; uje upesi kwangu. Unisikilize nikuitapo.
2 May my prayer be like incense before you, my uplifted hands like an evening offering.
Maombi yangu na yawe kama uvumba mbele zako; mikono yangu iliyoinuliwa na iwe kama dhabihu ya jioni.
3 Lord, make sure I don't say anything I shouldn't—keep a watch over my conversations.
Ee Yahwe, uweke mlinzi kinywani mwangu; mngojezi malangoni pa midomo yangu.
4 Don't let me think about evil things or take part in doing anything wrong with wicked people. I won't join in eating fancy food at their feasts.
Usiruhusu tamaa ya moyo wangu kutamani uovu wowote wala kushiriki katika matendo ya dhambi na watu waishio maovuni. Nisile vyakula vyao vya anasa.
5 Let a good person punish me in love—let them correct me. It will be like an anointing—I won't refuse it. But I still pray against those who do evil.
Mwenye haki na anipige; nao utakuwa ni wema kwangu. Anirudi; itakuwa kama mafuta kichwani pangu; kichwa changu na kisikatae kupokea. Lakini maombi yangu siku zote yatakuwa dhidi ya matendo yao mauvu.
6 They shall be thrown down by the power of the rock that judges them, and then they will recognize what I said was true!
Viongozi wao watatupwa chini toka juu mlimani; watayasikia maneno yangu kuwa ni matamu.
7 Just as the earth is broken up by the plough, so shall their bones be scattered at the mouth of Sheol. (Sheol )
Watalazimika kusema, “Kama vile jembe moja livunjapo ardhi, hivyo mifupa yetu imesambaratishwa kinywani pa kuzimu.” (Sheol )
8 But I'm looking to you, Lord God, for I find protection in you. Don't let me die!
Hakika macho yangu yanakutazama wewe, Yahwe, Bwana; katika wewe napata kimbilio; usiiache nafsi yangu.
9 Keep me safe from the traps they have set to catch me, from the snares of evil people.
Unilinde dhidi ya mitego waliyoiweka kwa ajili yangu, na matanzi yao watendao maovu.
10 Let them fall into their own traps while I pass by unharmed.
Waovu na waangukie kwenye nyavu zao wenywe pindi mimi nitorokapo.