< Psalms 137 >
1 When we sat down by the rivers of Babylon we wept as we remembered Zion.
Kando ya mito ya Babeli tuliketi na tulilia tulipokumbuka kuhusu Sayuni.
2 We hung up our harps on the willow trees.
Tulitundika vinubi vyetu kwenye miti ya Babylon.
3 For those who had taken us captive asked us for a song—our tormentors wanted us to sing a happy song from Jerusalem.
Huko watekaji wetu walitaka tuwaimbie, na wale walio tudhihaki walitutaka sisi tufurahi, wakisema, “Tuimbieni moja ya nyimbo za Sayuni.”
4 But how could we sing a song dedicated to the Lord in a pagan land?
Tungewezaje kuimba wimbo unaomuhusu Yahwe katika nchi ya ugeni?
5 If I forget Jerusalem, may my right hand forget how to play;
Kama nikikusahau wewe, Yerusalemu, basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
6 May my tongue stick to the roof of my mouth if I don't remember you—if I don't consider Jerusalem my greatest joy.
Ulimi wangu na ushikamane juu ya kinywa changu kama nisipokufikiria tena, na kama sipendelei zaidi Yerusalemu kuliko furaha yangu kuu.
7 Lord, please remember what the people of Edom did on the day Jerusalem fell, the ones who said “Tear it down! Destroy it down to its foundations!”
Kumbuka, Ee Yahwe, kile walichofanya Waedomu siku ya anguko la Yerusalemu. Walisema, “Ibomoeni, ibomoeni mpaka chini kwenye misingi yake.”
8 Daughter of Babylon, you will be destroyed! Happy is the one who pays you back, who does to you what you did to us!
Binti za Babeli, hivi karibuni wataharibiwa- mtu na abalikiwe, yeyote atakaye walipizia yale mliotufanyia sisi.
9 Happy is the one who grabs your children and smashes them against the rocks!
Mtu na abarikiwe, yeyote achukuaye na kusambaratisha watoto wenu juu ya jiwe.