< Psalms 120 >
1 A song for pilgrims going up to Jerusalem. I called out to the Lord for help in all my troubles, and he answered me.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 Lord, please save me from liars and cheats!
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 What will the Lord do to you, you liars? How will he punish you?
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 With the sharp arrows of a warrior and burning coals made from a broom tree.
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 I'm sorry for myself, because I live as a foreigner in Meshech, or among the tent-dwellers of Kedar.
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 I have lived for far too long among people who hate peace.
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 I want peace, but when I talk of peace, they want war.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.